Harmonize kumalizia ujenzi wa Msikiti ulioanzishwa na Diamond mtwara mwaka 2018 na kuuita 'Masjid Naseeb'

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Msanii wa Bongo Fleva, Harmonize, ametangaza kuwa atamalizia ujenzi wa msikiti ambao Diamond Platnumz aliuanzisha kijijini kwao Mtwara mwaka 2018. Kupitia Insta Story yake, Harmonize amesema kuwa msikiti huo ulianzishwa baada ya wao wawili kujadili umuhimu wa kusaidia jamii na kuwekeza mbele za Mungu.

Kwa mujibu wa Harmonize, Diamond alimpatia pesa za kuanzisha msikiti huo, lakini baadaye mradi huo ulisimama kutokana na changamoto mbalimbali. Hata hivyo, Harmonize amesema kuwa wiki iliyopita aliamua kuchukua hatua na tayari ametoa bajeti yote ili msikiti huo ukamilike kabla ya Sikukuu ya Eid.

Aidha, ameeleza kuwa msikiti huo utaitwa Masjid Naseeb kama njia ya kumshukuru Diamond kwa mchango wake wa awali. "Mungu akuzidishie ndugu yangu, hujapoteza," ameandika Harmonize, akiwatakia waumini wote Ramadhani njema.

Your browser is not able to display this video.
 
Mwanamuziki Harmonize ameweka wazi kumalizia Msikiti ulionzishwa kujengwa na Diamond Platnumz kijijini kwao Mtwara.
.
Harmonize anasema kuwa alipewa pesa na DiamondPlatnumz aka Simba ili kujenga msikiti huo lakini baada ya kugombana na ujenzi wa msikiti ulisimama. Sambamba na hilo Harmonize amesema kuwa ameshatoa pesa zote kwaajili ya kumalizia Msikiti huo na amependekeza uitwe jina la Naseeb

Harmonize ameandika ""TULIKUWA NA TABIA YA KUKUMBUSHANA KUWEKEZA MBELE ZA MUNGU IKIWEMO KUTOA SADAKA MWAKA 2018 NILIMSHAURI MY

BROTHER NASEEB TUJENGE MSIKITI HUU KIJJINI KWETU BAADA YA KUTAMBUA WANAKIJIJI WANA UHITAJI WANA KIU YA MAHALA PAZURI KWAJILI YA KUMLILIA MUNGU WETU KUFANYA TOBA DIAMOND ALINIPATIA PESA YA KUANZISHA MSIKITI HUU BAADA YA SHETANI KUSIMAMA ΚΑΤΙ NA MSIKITI HUU UKASIMAMA MPAKA LAST WEEK MUNGU ALIVYOSEMA SHETANI INATOSHA ALHAMDULILAH RIZIKI NINA PATA NIMESHATOA BUDGET YOOOTE MSIKITI UMALIZWE HARAKA IWEZEKANAVYO INSHALLAH MPAKA KUFIKIA SIKU YA EID LETTIR NITAFURAHI KUONA IBADA IKIFANYIKA HAPA NA NIMEWAOMBA WANAKIJLI WENZANGU HUU MSIKITI TUMEUBATIZA JINA AMASJIDNASEEB:

MUNGU AKUZIDISHIE NDUGU YANGU HUJAPOΤΕΖΑ RAMADHAN KAREEM"
 
🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂🤣🤣🤣😂😂😂😂🤣🤣😂🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂
 
🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂🤣🤣🤣😂😂😂😂🤣🤣😂🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂
Unafiki tu ikifika mwezi wa Ramadhan
 
Hawa watu ni hazina kwa Taifa "Mtaani kwetu hakuna msikiti tutawafikiaje watujegee" - Walisema misikiti tanzania hujengwa na mtu
 
Wakristo ifike mahala tusapot wakristo wenzetu imeisha hiyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…