Harmonize kusepa WCB: Alibaniwa matamasha mengi ya pesa ndefu kuliko Diamond

Amekurupuka tu akatunga chai yake hata bila kufikiria
 
Ngoja tuone hao kina Jembe ni Jembe na yule Manager wake Ww kike km watamfikisha level anazotaka
 
Hawa ndio wanazidi kumdidimiza huyu hamo
 
Wabongo kama tumerogwa hivi,ni watu tusiojielewa. Ingekuwa nchi za wenzetu hata hapa jirani tu kenya watu wangemsapot sana Diamond kwa mambo anayoyafanya ktk hii. Jambo moja dogo tu la kufikiria,huyo harmo ungemjua wewe bila Diamond?. Ona nyimbo za hao madogo wengine aliowakusanya,zinapigwa kila kona sio Tz tu hata nje ya Tz. Wewe unahisi wasingekuwa huko hizo nyimbo zao zingesikika hata mtu?. Hata kama una gereous na mtu isiyo na sababu,jaribu kujiuliza kwanza kwa nini namchukia? Ksbb tu amefanikiwa? Hiyo ndio gereous ya kipuuzi
 
Uongo mtupu na uchonganishi!

Kamwe mtu mwenye akili timamu awezi kuingia mkenge wa uchonganishi huu ambao mwisho wa siku nina hakika Harmonize ndiye atakaye poteza....

Hivi kweli mtu ambanie mtu ambaye akipiga show na yeye anapata chake? Hivi kweli ina ingia akilini mtu ambanie mtu ambaye alikubali kulipa gharama za kuvunja mkataba kama atakuwa tayari na hadi sasa kila show anayopiga bado Diamond na mameneja wanapata chao?

Hivi kweli kabisa muda na investiment iliyo fanywa na Diamond kwa Harmonize kweli Harmonize anaweza kuongea uongo huu dhidi ya Diamond na mameneja wake kweli? Nitakuwa wa mwisho kuamini haya na hakika kabisa Harmonize hatiweza kuongea haya labda amechanganyikiwa kabisa!

Hivi ni mara ngapi Diamond kalaumiwa ana mpendelea Harmonize pale WCB ?leo hii aje kichaa anasema kuwa alikuwa ana mbania kweli?

Hivi mwaka jana pale WCB kuna mtu alitoa nyimbo nyingi kuzidi Harmonize hadi mwaka huu mwezi wa sita?Kweli Harmonize anaweza ongea haya ya kubaniwa? Hakika huu ni uongo usio vaa chupi...,,

Hivi mnajua kuwa WCB wameona ni vyema wamuache awe huru kufanya atakavyo pamoja bado yuko kwenye mkataba na WCB na anapiga show na anafanya atakavyo pamoja mengi yako kinyume na mkataba wake? Hivi kweli wangekuwa wabaya sasa hivi si tungelikuwa kwenye mahakama au Basata?

Harmonize ameomba kuvunja mkataba na WCB na watu wamekubali na hadi sasa ajarudi kuja kuongea na watu waneona wavumilie tuu na kumsubiri kweli bado kuna kichaa anaona hawa watu ni wabaya?


Ushauri wangu tena kwa Harmonize kama umeamua kuondoka usirudi nyuma na wala usikubali kugombanishwa na WCB hawa watu sio wabaya na hawawezi kuwa wabaya....wamekutoa mbali sana umepiga hatua na umeona una hitaji kupiga hatua zaidi basi ondoka vizuri kama ulivyo ingia ..Usikubali kabisa maneno ya watu kuwa hawa watu ni wabaya maana hata shetani atakushangaa kabisa.


Cha msingi na kazi uliyo nayo ni kuuthibitishia umma unataka kufika sehemu fulani au umefika sehemu fulani ambayo WCB hawakukufikisha kabisa!
 
Ulichokiandika ni sawa na Baby kumbania Weezy ndani ya CMG kisa Weezy atapata umaarufu zaidi ya Baby atapata pesa nyingi kuliko baby.
Baby a.k.a Birdman
Kwa ufupi umeandika takataka.
 
🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️🙆🏽‍♂️
 
Ulichokiandika ni sawa na Baby kumbania Weezy ndani ya CMG kisa Weezy atapata umaarufu zaidi ya Baby atapata pesa nyingi kuliko baby.
Baby a.k.a Birdman
Kwa ufupi umeandika takataka.
Hata me mtoa mada amenishangaza sijui hata masuala ya mziki anayajua?si Bora Ange edit kwanza kuliko kupost upuuzi
 
Amani bila pesa. Kuna amani hapo???

Unataka asiwe na pesa?
Wapi uliona ana pesa akichuma kwenye mti?
Mnapenda watu wawe watumwa wasijitambue.. wengi na madunguli mnawafunika wasijitambue..
 


Mkuu ni "Jealous "
 
Mond ana roho mbaya sana yule jamaa kila kitu anataka awe yy tu
 
Nakumbuka maneno ya Rich Mavoko wanambania wanajua bila ya hivyo atamfunika bosi wake, hivi bila ya aggressive push na promo ya WCB unadhani hizo You Tube views za nyimbo za Harmonise zingeishia wapi?
Time will tell, msije baadaye mkarudi na threads za Harmonise anafanyiwa figisu ndiyo maana anaporomoka kimuziki, manake hamjui ya kuwa alishakataliwa(BSS) na kuambiwa hana kipaji akatafute shughuli nyingine ya kufanya. Huyo mnayemtwisha gunia la lawama ndiyo alimshika mkono mpaka hapo alipofika.
 
Jembe ni Jembe ndo kamlisha hayo maneno harmonize, kuna Matamasha akina Jembe ni Jembe walikuwa wanaandaa pamoja na Yale ya fiesta , harmonize alikuwa akihtajika Ila WCB wanaweka ngumu Kwa sababu walikuwa hawafiki bei, show ya south Sudan Jembe aliplay part pale, na huko ndo alimjaza upepo dogo, pia kitendo cha diarmond kuingilia ft ya Davido kwenye wimbo wa Kwangwaruu, na kutaka ashirikishwe yeye japo hakulazimisha pia ilimuumiza dogo...twendeni taratibu
 
Aliki amekulipa shilingi ngapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…