Harmonize ni Moto wa kuotea mbali

othiambo

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2014
Posts
1,995
Reaction score
2,795
Kiukweli wamepita wasanii wengi Tanzania wenye weredi na ubunifu mkubwa walitunga tungo zenye kubamba haswaa ila katika kizazi hichi tulicho sasa wapo wengi wanafanya vizuri Ila huyu mmakonde Harmonize ni mbunifu kwakweli mimi hii wimbo wake wa MTAJE bila kuangalia ujumbe imetulia sana.
 
Wimbo wa Dounia umefanya nijue ana akili kweli. Wimbo mtam sana ila napigilia msumari kauli niliyowai kuskia kwa Diamond kuwa kwa burudan za kimataifa kutoboa usijar tungo busara bali beat na kumiliki jukwaa.

Hapa ndo diamond na squad yake kanawaacha mbali. Wimbo wa Harmo kwa tunzi na beat ni wetu tu. Ni mtazamo wang sina uteam, mana binafs sijawai kuhama kundi la rhumba na sebene!
 
Ni kwellll Kwa hilo sipingi.
 
Hata mimi naupenda na beat yake naipenda. Sema jamaa kuna muda anakuwa na uandishi flani naupenda. Kwenye jeshi, na mtaje napenda maana hakuna vingereza vingi na uandishi umekaa poa sana.

Diamond alikuwaga napenda uandishi wake wa maneno ya kisw kitupu bila kingereza na jinsi alivyokuwa anachagua maneno ya kisw rahisi lakini alikuwa akiyapangilia vizuri.

Ubaya kinachoniumiza maneno neno maneno
Kwa ndugu, majirani kwanini anawapa misemo
Najaribu papasa huenda kwa macho nitaona chochote
Ila ndo kutwa mikasa na nazidi kutafuta huenda niokote

Nilikuwa napenda tungo zake za hivi. Hata zuchu nilipenda uandishi wake wa wimbo wa nisamehe.
 
Mama Paula naona umeanza mdogo mdogo kukubali msamaha.
 
Ni kweli sema haya mambo ya kutaka kwenda international ndio yanauaga mziki mzuri.
 
kabisa hata mimi kuna mtu nilikuwa namwambia kuhusu huu wimbo umetulia sana
 
Jamaa yupo vizur sana ukiisikiliza bakhresa ukiwa umetulia ni bonge la ngoma
 
Kweli anajua kuimba huyu mabangi..nyimbo Kama jeshi..nimtaje na ule wa amapiano alioiga South Africa..Ni nyimbo nzuri Sana.. hata bakresa sio mbaya..
 
MTAJE jamaa aliimba kwa hisia sana. Hizi ni baadhi ya nyimbo za Mmakonde ninazozielewa sana.

1. Mtaje.
2. Matatizo.
3. Niambie.
4. Nishachoka.
5. Atarudi.
6. Mpaka kesho.
7. Mwaka wangu.
8. Kwangwaru.
9. Happy birthday.
10. Mama.
 
1.Aiyola
2.Never give up
3.Uno

4.Ngoja nikadanilodi hiyo ya mama Paula
 
Ni kweli sema haya mambo ya kutaka kwenda international ndio yanauaga mziki mzuri.
Ukilitaka soko la kimataifa lazima ukubaliane na hiyo situation, Diamond ilimlazimu kubadilika huku akilaumiwa na wale waliokuwa wakipenda uandishi wa maishiri yake lakini hakuwa na namna kwani analitamani sana soko la nje kwa ambao Kiswahili hawakifahamu.
Hii ni challenge itakayowakabili wasanii wengi popular pale watakapoamua kupambana ili wavume mbali nje ya mipaka, ni ngumu lakini kila artist apambanie malengo yake.
 
Kazi kwao Ila wasisahau na kwao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…