Hasheem Rungwe: Wanafunzi na wagonjwa wapewe ubwabwa bure

Hasheem Rungwe: Wanafunzi na wagonjwa wapewe ubwabwa bure

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Uongozi wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) umemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuangalia upya mfumuko wa bei hali ambayo inapelekea ugumu wa maisha kwa wananchi, huku mwenyekiti wa chama hicho Hasheem Rungwe akisisitiza suala la chakula shuleni na hospitali linapaswa kutolewa bure.

Egut-E2XgAIN6zq.jpg

Wakiongea na waandishi wa habari makao makuu ya Chama jijini Dar es Salaam wanawake hao wameonesha kilio chao kwa Rais huku wakimtaka awakumbuke na wao kwenye nafasi mbalimbali za uongozi.

Mwenyekiti wa Baraza Taifa, Fatuma Seleman amesema yapo mambo mengi vanavomuumiza mwanamke wa Kitanzania ukiachilia mbali mfumuko wa bei, amesema hata katika suala zima la uzazi lazima liboreshwe ili wanawake wakimbilie kujifungulia kwenye vituo vya afya na sio nyumbani.

"Chakula kinapaswa kitolewe bure watoto wetu wanaumia ila hawawezi kuongea wanapaswa wapewe ubwabwa bure, hata katika hospitali wagonjwa wapewe bure kwani Serikali inao uwezo kwasababu inakusanya kodi kubwa” amesema Rungwe.

Chanzo: Mwananchi
 
Baraza la Wanawake CHAUMMA wapeleka ujumbe mzito


Viongozi wa Baraza la Wanawake CHAUMMA mwenyekiti taifa Bi. Fatuma Selemani na katibu mkuu Bi. Mary Mpangala wampelekea ujumbe mzito Mh Rais Samia Hassan kuhusu masuala ya mfumuko wa bei, huduma za afya, elimu
 
Baraza la Wanawake CHAUMMA wapeleka ujumbe mzito


Viongozi wa Baraza la Wanawake CHAUMMA mwenyekiti taifa Bi. Fatuma Selemani na katibu mkuu Bi. Mary Mpangala wampelekea ujumbe mzito Mh Rais Samia Hassan kuhusu masuala ya mfumuko wa bei, huduma za afya, elimu

cHAUMA HOYEEEEEEEEEEEEEEE
 
Back
Top Bottom