Hashim Rungwe: Kama tatizo ni muda, Rais Samia aongezewe muda ili tupate Katiba Mpya ndio tufanye Uchaguzi

Hashim Rungwe: Kama tatizo ni muda, Rais Samia aongezewe muda ili tupate Katiba Mpya ndio tufanye Uchaguzi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1719215295037.png

Hashim Rungwe

Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Hashim Rungwe amesema hakuna sababu ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu mwakani bila kuwa na Katiba mpya.

Anasema haamini kama Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi pekee inatosha kuufanya uchaguzi kuwa huru na wa haki kama Katiba haitarekebishwa.

Amesema Katiba mpya ndiyo itamaliza sintofahamu ya upande mmoja kuona uchaguzi hautakuwa huru na haki, licha ya Rais Samia mara kadhaa kuwahakikishia Watanzania kwamba uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

“Uchaguzi ujao ufanyike kwa kutumia Katiba mpya, hicho ndicho kitamaliza sintofahamu inayoendelea sasa,” amesema Rungwe katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika ofisini kwake, Makumbusho jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Rungwe anasema kama changamoto ya kupatikana kwa Katiba hiyo ni muda, basi vyama vya siasa wakubaliane Rais Samia aongezewe muda, Bunge liridhie, ili muda huo utumike kukamilisha upatikanaji wa Katiba mpya, ndipo uchaguzi ufanyike.

“Kama tatizo ni muda, bora tukubaliane na Bunge liidhinishe Rais aongezewe muda, lakini kwa masharti kwamba katika kipindi hicho kitakachoongezwa tuwe tumepata Katiba mpya, ndipo twende kwenye uchaguzi,” anasema Rungwe.

==============================================

The Chairman of Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Hashim Rungwe, has said that there is no reason to go to the general elections next year without a new Constitution.

He believes that the Independent National Electoral Commission alone is not enough to ensure that the elections are free and fair if the Constitution is not amended.

He said that a new Constitution will end the uncertainty of one side thinking that the elections will not be free and fair, despite President Samia assuring Tanzanians several times that the elections will be free and fair.

"The next election should be conducted using a new Constitution, that's what will end the current uncertainty," said Rungwe in a special interview with Mwananchi that took place in his office at Makumbusho in Dar es Salaam recently.

Rungwe suggests that if the challenge is the time it takes to obtain the Constitution, then political parties should agree to extend President Samia's term, and Parliament should approve it, so that the time can be used to complete the process of obtaining a new Constitution before the elections take place.

"If time is the problem, it's better for us to agree and let Parliament approve an extension for President Samia," he said.

PIA SOMA
- Deo Sanga aomba Rais Magufuli aongezewe muda hata asipotaka

- Ally Kessy: Katiba sio msaafu, Rais Magufuli akimaliza muda wake tutatengua Katiba aongezewe muda | Spika Ndugai amuunga mkono

- Mzee Mwinyi: Rais Magufuli aongezewe muda wa miaka 5 zaidi kama shukrani

- Zile kelele za Rais Magufuli aongezewe muda mbona hazipingwi kwa Rais Samia?

- Uchaguzi 2020 - Dkt. Magufuli aongezewe muda wa kutawala

- Rais Magufuli akifanya mambo haya, Watanzania watamlilia wenyewe aongezewe muda wa kutawala

- Kuelekea 2025 - CCM Zanzibar wapendekeza Rais Mwinyi atawale kwa miaka 7, wasema kufanya uchaguzi 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya fedha za umma
 
Wakiongeza muda, mtaambiwa miaka mitano inabidi itumike kutoa elimu ya katiba Kwa wananchi,then mwaka wa sita,Rais ateue wajumbe wamalize kazi,ambapo MWAJIRI wa watu wengi atabaki Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama dola.
 
Hata aongezewe miaka 20, bado atazingua tu. Maana ccm wanafikiri hii nchi ni mali yao. Na sisi wananchi wengine wanatuona ni manyani tu. Bila ya matumizi ya nguvu, kamwe tusitegemee mabadiliko ya kweli ya kikatiba kwenye hii nchi ya kusadikika.
 
Hata aongezewe miaka 20, bado atazingua tu. Maana ccm wanafikiri hii nchi ni mali yao. Na sisi wananchi wengine wanatuona ni manyani tu. Bila ya matumizi ya nguvu, kamwe tusitegemee mabadiliko ya kweli ya kikatiba kwenye hii nchi ya kusadikika.
Absolutely true!


"The right cannot be given as a gift by the oppressor, it must be demanded by the oppressed."

Martin Luther King Jr
 
Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Hashim Rungwe amesema hakuna sababu ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu mwakani bila kuwa na Katiba mpya...
Meelezeni Mzee,
muda upo, fedha zipo zakutosha, lakini ni baada ya uchaguzi mkuu 2025, ndipo mchakato utaendelea na tukijaaliwa maridiano mema, basi utakamilika mapema, kabla ya 2030🐒

na huko kwa bunge maalumu wakijaa majambazi wa kukunja mkwanja kijanja na kusingizia kususa, kuzira au kugoma, hiyo ni shauri yako. Mchakato utakamilika bila mbambamba 🐒
 
Meelezeni Mzee,
muda upo, fedha zipo zakutosha, lakini ni baada ya uchaguzi mkuu 2025, ndipo mchakato utaendelea na tukijaaliwa maridiano mema, basi utakamilika mapema, kabla ya 2030🐒

na huko kwa bunge maalumu wakijaa majambazi wa kukunja mkwanja kijanja na kusingizia kususa, kuzira au kugoma, hiyo ni shauri yako. Mchakato utakamilika bila mbambamba 🐒
FYI: Hakuna nchi hata moja hapa duniani ambayo imepata Katiba yake ya nchi iliyo bora na kwa kuzingatia maoni ya wananchi wengi walio ktk nchi husika bila ya Wananchi wenyewe wao kwa kwao kwenye nchi hiyo kuchapana Makonde. Haipo nchi ya namna hiyo. Kama unazifahamu nchi za namna hiyo basi zitaje hapa kwa faida ya wasomaji wa mtandao huu.
 
FYI: Hakuna nchi hata moja hapa duniani ambayo imepata Katiba yake ya nchi iliyo bora na kwa kuzingatia maoni ya wananchi walio ktk nchi husika bila ya Wananchi wenyewe wao kwa kwao kwenye nchi hiyo kuchapana Makonde. Haipo nchi ya namna hiyo. Kama unazifahamu nchi za namna hiyo basi zitaje hapa kwa faida ya wasomaji wa mtandao huu.
Tanzania kisiwa cha Amani, wana katiba ya wanainchi...

usijisahaulishe kwa makusudi tafadhali🐒

hata hiyo ambayo tunategemea kuiunda baada ya uchaguzi wa 2025, itakua ni ya wanainchi licha ya wenye mihemko kususa, kuzira na kugoma 🐒

you should be informed about that gentleman...
 
Tanzania kisiwa cha Amani, wana katiba ya wanainchi...

usijisahaulishe kwa makusudi tafadhali...
Hata majirani zetu Kenya walikuwa katika kisiwa cha amani zaidi kuliko Sisi kabla ya kupata Katiba yao mpya waliyonayo hivi sasa ambayo waliipitisha mwaka 2010.

Lakini Nafikiri unajua kilichotokea huko mwaka 2007 hadi 2008 ambacho kilisababisha upatikanaji wa Katiba yao mpya waliyonayo hivi sasa.
 
Hata majirani zetu Kenya walikuwa katika kisiwa cha amani zaidi kuliko Sisi kabla ya kupata Katiba yao mpya waliyonayo hivi sasa ambayo waliipitisha mwaka 2010. Lakini Nafikiri unajua kilichotokea huko mwaka 2007 hadi 2008 ambacho kilisababisha upatikanaji wa Katiba yao mpya waliyonayo hivi sasa.
nadhan unafahamu pia wanajutia wameuana bure kwa ukabila wao na wakapata katiba ambayo inawatenganisha zaidi kikabila lakini pia kikanda 🐒

Tanzania hatuwezi kukaribia huko wala kufika huko kwenye kuandamana na masufuria kichwani kudai unga wa ugali ikulu 🐒
 
Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Hashim Rungwe amesema hakuna sababu ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu mwakani bila kuwa na Katiba mpya...

Haya ni maneno ya hekima. Kila mwenye dhamira njema atakubaliana na hili wazo.

Maana itasaidia nini kukimbilia kufanya kitu bandia wakati unaweza kusubiri ukafanya kitu halisia?
 
Back
Top Bottom