TANZIA Hassan Bantu afariki Dunia

TANZIA Hassan Bantu afariki Dunia

Ebu twambie umaarufu wa huyu mtu maana naona unamsifia sifia tuuu

Mmatumbi mwenzetu kuweza kuhesabika ndani ya walioshika wadosi hatamu wa caliber za kina MO si jambo dogo mkuu.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Namuona kama mmatumbi tu kumbe ni mwenye asili ya asia? Mungu aiweke roho yake mahala pema,nimeona wana Morogoro wengi wanamlilia inaonekana alikuwa mtu mwema sana. Tenda wema legacy yako itadumu ,lete maneno matamu legacy yake haitafika hata Manzese!

Umesoma wapi kuwa alikuwa muasia?

Huyu bwana alikuwa mmatumbi kamili.
 
Kwa hyo tupo wimbi la ngapi?
Unazihesabia wapi hizo wimbi 4 jombi? Hivi unajua hata ripoti ya mama kuhusiana na hili gonjwa ilisema nini kweli?

Ila usisahau hii ni awamu ya sita. Vita vya kiuchumi viliondoka na mwendazake.
 
Takatisha sentensi

Hiyo sentensi ni kuntu kabisa haina kelele wala mkwaruzo.

Kumbuka huyu ni mzawa. Pia kumbuka yuko katikati ya wengi wenye asili ya kiasia.

Labda nikuulize kidogo pia. Neno kudemka ulikuwa ulishalisikia kabla ya mama kulitamka?
 
huyu jamaa kweli ni maarufu..mimi nimekaa moro, jina lake ni maarufu lakini sikuwahi kumjua na wala sijui anafanya nini... nimepita hapa nahisi nitapata majibu
Mwana Moro Kitambo huyo,Kuanzia miaka ya 80 mpaka 90 Nguo za Skukuu na Uniform za Shule ni lazima uwaone wao BANTU STORE ndiyo upendeze.Ukija kwenye Soccer Ndiyo Wana JAMAICA chama letu la Moro.Apumzike kwa Amani Mwana.
 
Mwana Moro Kitambo huyo,Kuanzia miaka ya 80 mpaka 90 Nguo za Skukuu na Uniform za Shule ni lazima uwaone wao BANTU STORE ndiyo upendeze.Ukija kwenye Soccer Ndiyo Wana JAMAICA chama letu la Moro.Apumzike kwa Amani Mwana.
Tumeshona sana nguo Bantu store, kweli mdau
 
Back
Top Bottom