Cobrahypnosis
JF-Expert Member
- Jul 28, 2021
- 362
- 676
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ujamaa...Naendelea kuwakumbusha kuwa jukumu la uhuru, amani, umoja na mshikamano ndio jadi yetu watanzania na lipo mikononi mwetu.View attachment 2601640
View attachment 2601641
Ujamaa...
"Silence is golden because it can never be repeated."
Ukìitaka amani ya kweli hakikisha panakuwepo haki na usawa kwa wote.
Dhulma inaangamiza.
Ujamaamf,Duniani hapajawahi kuwa na usawa hata siku moja. 50/50 haitakaa kutokea walio wengi ndio washindi.
Ujamaamf,
Waislam tungependa kulisikia jibu hilo kutoka serikalini.
Ujamaa...Waislam wapi hao?. Labda wewe binafsi ila sio waislam hawa tunaoishi nao mtaani, kutaabika nao na kushirikiana nao. Au Labda unawasemea waislam wa msikiti wa manyema!!.
Ujamaamf,Said,
Naona anaesadikika kuwa ni (muisilamu(sijui muisilamu ndio nini))akila kipondo, naunga mkono kuwa wapigwe tu maana hamna namna. Ukifanya vurugu utapigwa tu na daima huwezi pigwa bila sababu.
Necta parokia ndio nini?. Jamii za watu dhaifu hushindwa kujisahihisha, kujisimamia na hufikiri matatizo yao yameletwa na watu fulani.
Shura ya maimamu? Akina sheikh kipozeo na ponda. Hio shura si baraza lao liliikataa kuwa sio msimamo wao. Shura itabadilisha nini.
Serikali ni pana sana, mamlaka ya serikani ni kubwa sana.
Kama ndio waislam hao basi napata shaka kuhusu afya yako ya akili, lakini sishangai kama ulidiriki kuandaa historia ya nchi hii na kina ilunga hassan kapungu huwezi kuwa mwema kwene jamii ya nchi hii. (ilunga hassan kapungu) alipata kutamka kuwa mapadri wa kanisa katoliki wauwawe, Kaishia kufa yeye huku mapadri na walei wakiendelea kuishi.
Naendelea kuwakumbusha kuwa jukumu la uhuru, amani, umoja na mshikamano ndio jadi yetu watanzania na lipo mikononi mwetu.View attachment 2601640
View attachment 2601641
MAHOJIANO NA TBC 1 2022
Ujamaamf,
Umeniuliza Waislam gani?
Nimekupa jibu.
Umekuja na mengine nami nitakujibu.
Naamini unatambua kuwa wapo wanamaombi na wengine mfano wa hao.
Nasi tunao wetu vilevile ambao wanaweza kukodiwa wakanunuliwa kanzu, koti na kofia wakatiwa kwenye basi hadi Dodoma kumsindikiza Gwajima kuapishwa Bungeni lau alisema maneno yasiyopendeza.
Walikuwapo "masheikh" vyombo vya habari vimeandika walitoka Bagamoyo kwenda Dodoma nyumbani kwa Lowassa kumuomba agombee urais wa Tanzania.
Haya kwetu si mageni.
Hatukushangaa kuwaona wengine Channel Ten wakiipiga vita Shura ya Maimamu.
Hawa wote wametusaidia.
Heshima walizokuwanazo hazipo tena.
Unapokuwa kibaraka hata anaekukodisha anakudharau.
Historia ya vipi EAMWS ilivunjwa imetufunza mengi.
Lakini serikali ina wataalamu na wanasoma taarifa tunazoandika na wanatambua ukweli uliomo ndani ya yote.
Maandamano ya mwisho ni yale dhidi ya NECTA.
Waislam walitishwa kuwa watashambuliwa.
Wataalamu ndani ya vyombo vya serikali walishauri vinginevyo wakaeleza ukweli kuwa ni kweli kuna hujuma dhidi ya Waislam taarifa zenye uthibitisho zipo.
Chembelecho hapakuwa na "kipondo."
Serikali iliyaruhusu maandamano kimya kimya kwa FFU kuyasindikiza maandamano hadi Kidongo Chekundu kama ilivyokubalika ingawa hilo halikukubalika lote baadhi walikwenda hadi Wizara ya Mambo ya Ndani.
Picha za maandamano yale nimekuwekea na zipo pia katika taarifa za serikali.
Kwetu haya ni mafanikio makubwa.
NECTA imejua kuwa tunajua na serikali ilikubali ukweli.
Yapo mabadiliko makubwa na tunaungwa mkono na umma mkubwa.
Kauli ya Sheikh Ilunga umeibadili kuhusu aliyosema baada ya Sheikh Rogo kuuliwa Mombasa.
Ukitaka kujua nini alisema utajua.
La kama nia yako ni kutaka kunishinda mimi kwa hoja uwezo huo huna si wewe wala si mwingine mfano wa wewe.
Moyo ndani wa moyo wako unatambua hili.
Ama kuhusu akili yangu hili pili unalitambua na ushahidi unaishinao hapa JF.
Nimepokea nishani mbili kutoka kwa Waislam kwa mchango wangu kwa dini yangu na kwa kuandika historia ya uhuru wa Tanganyika kama ilivyostahili kuandikwa.
Wala usichukulie kuwa haya ni majisifu.
Nakuambia.haya ili ufungue macho yako uone ukweli.
Sisi si wahuni.
Tuna heshima zetu ndani ya jamii ya Waislam wa Tanzania Bara na Visiwani.
Mchango wetu unathaminiwa na jamii.
Hakuna vurugu ila tunataka haki na usawa.
Nipo hapa mwaka wa 10 na zaidi na hamjaacha kunisoma.
Ninachokuomba andika kwa adabu na jiepushe na kejeli.
Unasomwa na watu wengi.
Ujamaamf,Said wa tambo na majisifu naona unajitutumua. Kwa ubishi hakuna anaekufikia ila fitna zako zitakabiliwa vilivyo. Nakukusha tu !! Sipo hapa kushindana na wewe maana hutuna cha kushindana lakini pia hakuna jipya kutoka kwako yote ni yaleyale tu. Tupo awamu ya sita sasa.