Hata kama ajira hakuna, bado hatupaswi kuwananga na kuwakatisha tamaa wahitimu na waliopo bado masomoni

Hata kama ajira hakuna, bado hatupaswi kuwananga na kuwakatisha tamaa wahitimu na waliopo bado masomoni

Bob Manson

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2021
Posts
4,158
Reaction score
7,787
Kumekuwa na wimbi kubwa la watu ambao hawaishi kuwasemea vibaya wahitimu wa elimu ya ngazi za juu hapa nchini. Ni kweli tatizo la ajira linazidi kuwa kubwa lakini sio sababu ya kulaumu na kuwasema vibaya wahitimu.

Huwa najiuliza, hao wanaokaa vijiweni na kuanza kuponda wanafunzi wa vyuo kwamba wanapoteza muda, Je majumbani mwao wana watoto? Kama jibu ni ndiyo, mbona wanapambana sana kusisitiza watoto wao waende shule na wasome kwa bidii. Kama wanaona elimu haina maana basi wasiwapeleke watoto wao shuleni.

huwa naumizwa sana na maneno ya watu (hasa ambao hawajasoma) kuhusu hili. Lengo la kusoma siyo kuajiriwa tu, sio lazma wote tuajiriwe wengine watafanya mambo mengine kwa kutumia elimu zao kama kujiajiri na kufanya ubunifu mwingine.
 
Hakuna sababu ya kuwaficha hali halisi. Mambo si kama yalivyokuwa tangu zama za ukoloni, uhuru mpaka sasa. Mkoloni alisomesha wananchi ili apate wafanyakazi wa kufanya kazi za serikali yake, serikali za wazalendo nazo zilirithi mtazamo wa wakoloni wao katika kuwasomesha wananchi wake. Serikali itaendelea kusomesha wananchi wake ili ipate wataalamu wa kufanya kazi zake, wahitimu ni wengi na serikali haiwezi kuwaajiri wote, itabidi wengine wajiajiri wenyewe au wakaajiriwe sekta binafsi. Malengo ya sasa ya kusoma ni kupata ujuzi na maarifa ya kujiajiri na kuajiriwa ni second option. Wahitimu ni wengi mentality ya kuajiriwa tu ndio target goal imepitwa na wakati itabidi serikali na sekta binafsi ziwe zinaweka dau kubwa kupata wafanyakazi wake kwa kuwa wahitimu wanapaswa first of all watasoma ili wakajiajiri kwenye shughuli zao kuliko kutegemea only kuajiriwa na matokeo yake wahitimu wanadoda mitaani wakisubiri job vacancy/opportunity zitangazwe watachakaa nyumbani
 
Hakuna sababu ya kuwaficha hali halisi. Mambo si kama yalivyokuwa tangu zama za ukoloni, uhuru mpaka sasa. Mkoloni alisomesha wananchi ili apate wafanyakazi wa kufanya kazi za serikali yake, serikali za wazalendo nazo zilirithi mtazamo wa wakoloni wao katika kuwasomesha wananchi wake. Serikali itaendelea kusomesha wananchi wake ili ipate wataalamu wa kufanya kazi zake, wahitimu ni wengi na serikali haiwezi kuwaajiri wote, itabidi wengine wajiajiri wenyewe au wakaajiriwe sekta binafsi. Malengo ya sasa ya kusoma ni kupata ujuzi na maarifa ya kujiajiri na kuajiriwa ni second option. Wahitimu ni wengi mentality ya kuajiriwa tu ndio target goal imepitwa na wakati itabidi serikali na sekta binafsi ziwe zinaweka dau kubwa kupata wafanyakazi wake kwa kuwa wahitimu wanapaswa first of all watasoma ili wakajiajiri kwenye shughuli zao kuliko kutegemea only kuajiriwa na matokeo yake wahitimu wanadoda mitaani wakisubiri job vacancy/opportunity zitangazwe watachakaa nyumbani
Kweli kabisa sio lazma wote wapate ajira za serikali ama sekta binafsi. Pia sikuhizi vyuoni kuna masomo mbalimbali ambayo endapo mwanafunzi akizingatia kuyasoma vizuri yanaweza kumsaidia katika kujiajiri.
 
Hivi serikali yetu huwa haijifunzi kwa mataifa kama marekani, china na india wahitimu wake huwa wanalenga nini wanaposoma shuleni/vyuoni? wanasoma ili serikali zao ziwaajiri?
 
Kuambiwa ukweli ni kuwananga?
 
Mentality ya wazazi walioishi maisha yao yote wameajiriwa hawana akili za kujiajiri wala kufanya ujasiriamali na biashara achilia mbali ufundi na kilimo. Soma uje uajiriwe serikalini kuna pensheni uzeeni ndio kauli inayowafubaza akili watoto wao. Watoto wanasoma wakijua wataajiriwa, akili ya kujiajiri haipo, matokeo yake mtoto anagonga miaka 30 hajaajiriwa na ni tegemezi asiyejua kujishughulisha na kuishia kuilalamikia serikali kwa sera zake mbovu za ajira
 
Mentality ya wazazi walioishi maisha yao yote wameajiriwa hawana akili za kujiajiri wala kufanya ujasiriamali na biashara achilia mbali ufundi na kilimo. Soma uje uajiriwe serikalini kuna pensheni uzeeni ndio kauli inayowafubaza akili watoto wao. Watoto wanasoma wakijua wataajiriwa, akili ya kujiajiri haipo, matokeo yake mtoto anagonga miaka 30 hajaajiriwa na ni tegemezi asiyejua kujishughulisha na kuishia kuilalamikia serikali kwa sera zake mbovu za ajira
Wahitimu na wanafunzi wanapaswa kufuta hii mentality ya kusoma ni lazima kuajiriwa, hii itasaidia kuwapunguzia msongo wa mawazo na kukata tamaa pale watakapo hitimu safari yao ya elimu.
 
Back
Top Bottom