Hata nikitumika miaka kumi, Siwezi kuondoka Yanga kwasababu ya kukosekana hela

Hata nikitumika miaka kumi, Siwezi kuondoka Yanga kwasababu ya kukosekana hela

Kumbukeni kasema mwisho wa siku atadai malimbikizo yake hadi fifa.
Akikaa hiyo miaka kumi bila kulipwa ghalama yake itakuwa ni kupewa timu aimiliki.
Ndiyo hesabu zake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wanaJF,ni imani yangu mnaendelea vema na kazi.

Leo katika kipindi cha Kipenga Extra kinachoruka kuvitoa East Africa Radio kuanzia saa 6 mchana hadi saa 7,aliarikwa,head coach mkuu wa Yanga,Papa Mwinyi Zahera katika kipindi ambacho host wake ni Goza Chuma.

Alipoulizwa iwapo ataondoka kwasababu ya kutolipwa,akajibu Siwezi kuondoka Yanga kwasababu ya kutolipwa Maana najua sikumoja nitalipwa cos nina mkataba nao,hata nikikaa miaka kumi najua nilalipwa hata kwakwenda fifa.Alipoulizwa ameijuaje Yanga akasema ameijua kupitia mdogo wake ambaye ni mfanyabiashara mkubwa nchini Kenya na huyo mdogo wake ni rafiki mkubwa wa ndama ambaye ni moja ya wanachama waandamizi wa timu yetu ya wananchi.

Akijibu swali la anawaonaje wachezaji wa Tz alisema wengi wanakosa physical exercise, hivyo aliamua kutoa hela yake mfukoni kununua vifaa vya kusoma work rate ya wachezaji wanapokuwa mazoezi,hivyo kuifanya Yanga kuwa fit na wachezaji kutochoka kwa dakika zote 90.Na Mwinyi anaonyesha kuwa anaishi na wachezaji wake kama familia moja.

Yanga tukiwekeza vema huyu Kocha tukampa muda anaweza kutuvusha na kutufikisha mbali sana.

Daima mbele,Nyuma mwiko💪💪💪💪💪
Njaa ikimuuma vizuri ataongea vizuri
 
Back
Top Bottom