KERO Hata ukiwa na pump tabu ya maji iko pale pale kama asiyekuwa nayo kutokana na presha ndogo ya maji. Wizara ya Maji tuambieni ukweli

KERO Hata ukiwa na pump tabu ya maji iko pale pale kama asiyekuwa nayo kutokana na presha ndogo ya maji. Wizara ya Maji tuambieni ukweli

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Nadhani tutakubaliana pande zote kuwa maji sasa hivi ni changamoto. DAWASA walishauri watu wafunge pump, maji hata yasipokuwa na presha sana inaweza kusaidia!

Arooo, sasa hivi kwanza maji hayatoki, yakitoka ni usiku, halafu presha ni ile ya kuchululu, yaani hata pumzi hazifanyi kazi.

Kwa inavyoonekana hali ni mbaya. Maana hata ukiwatafuta DAWASA unaambiwa tu wamepokea changamoto yako, inashughulikiwa, au wanashughulikia tatizo la kutoa upepo, lakini tatizo hili halijawahi kuisha!

Yaani ni kama kuna jambo wanajua limeharibika lakini hawaelezi watu ukweli. Sasa ni bora waendelee kutudanganya au kutuambia ukweli, kama ni ratiba watu wajue siku fulani na fulani maji yatatoka?

Lakini pia waje watuambie yale maji waliyokuwa wanajitapa tumeyavuna mpaka yaanza kumwagika yako wapi? Pia Watanzania wanafidiwa vipi kwa kukosekana kwa huduma hii muhimu? Maana kama nilivyosema hapa kumradhi haitoshi!

DAWASA Wizara ya Maji
 
Naona kuna tatizo kubwa...
Pengine tunasubiri neema ya mvua ndo tupate maji!
Kweli, na kwa jinsi jua linavyowaka saivi naona wanaenda kuaibika soon.. watakuja kuongea wakati hali ikiwa mbaya wakati walikuwa na nafasi ya kuongea mapema
 
...wakati huo kuna maeneo maji yanapasua mabomba kwa pressure kubwa.
 
Ushachoka Mkuu, halafu maji hayatoki lakini bili inatoka!
kama mtu unauwezo unatafuta eneo lenye maji unajenga na unachimba kisima chako unabaki kuangalia watu wakihorojoka!
 
Naomba nieleweshe, hiyo pampu unaiunganisha na mfumo wa dawasa
Au pampu ya kisima ulichochimba ?
 
In Abundance of Water a Fool is Thirsty....

Oh, it's a disgrace, To see the human-race, In a rat race
 
Hamjasikia hata mazao yanakauka huko Kondoa na kwingineko. Kukosekana kwa mvua kwa muda mrefu ndio chanzo Cha Tatizo.
 
Hatuna long term plan ya maji na hasa kwenye mpango mzima wa uhifadhi wa mazingira
 
baadhi ya maeneo maji yanatoka siku mbili au tatu kabla ya usomaji wa mita.
 
Tangu Novemba 2023 ulipoanza ujenzi wa BRT kipande cha Buguruni hadi Karume hakuna maji Barabara ya Uhuru na mitaa ya jirani. Na hakuna anayejali.
 
Kwa uhaba huo wa maji Mara yako ya mwisho kuoga ni lini? Kuwa mkweli mleta uzi
 
Naona kuna tatizo kubwa...
Pengine tunasubiri neema ya mvua ndo tupate maji!
Ikinyesha tu utasikia mpaka takwimu za maji, utasikia maji yaliyopo chini ya ardhi ni kadhaa, yaliypo chini ya ardhi ni trillions kadha. Na ujazo wa maziwa ni lita bilioni kadhaa.

Kwanza hatuisikii ile mitambo ya kuchimba visima yaliyosema itachimba visima kila kona.
 
Back
Top Bottom