KERO Hatari kwa usalama wa wanafunzi chuo cha Ustawi—DSM: Ratiba ya masomo hadi saa 4 usiku

KERO Hatari kwa usalama wa wanafunzi chuo cha Ustawi—DSM: Ratiba ya masomo hadi saa 4 usiku

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Wanafunzi wa Chuo cha Ustawi— Institute of Social Work, Bamaga, Dar es Salaam wanalalamika ratiba za masomo zinazoenda mpaka Saa 4 Usiku. Hii inahatarisha usalama wao hasa wakati wa kurudi makwao huku wengine wakitokea mbali kama vile Gongo la Mboto, Mbagala, Tegeta; hii inapelekea kufika makwao sio chini ya Saa 6 Usiku.

Kero hii imeleta shida kwa wazazi na baadhi ya wanafunzi wa kike kudai kuwa wanahofia vitendo vya ubakaji na ukatili mwingine ikiwemo uhalifu nyakati za usiku.

Pia, soma: √ - Chuo cha Ustawi wa Jamii: Wanafunzi wanachagua wenyewe kusoma asubuhi au Mchana, tunawashauri wakae karibu na Chuo

Tunaomba uongozi wa chuo hiki kufuatilia jambo hili na kuweka ratiba vizuri. Vyuo vingine muda wa masomo mwisho saa 2 usiku.
1730730343372.png
 

Attachments

Kama chuo kimelemewa na wanafunzi wengi kitafute namna ya kutatua changamoto hiyo sio kuwapa watoto ratiba za usiku. Sasa hivi mambo ni mengi, watoto wengine wanatoka mikoani hawajui kunavigate mji wanaweza wakapata shida kufika wanapoishi ukizingatia chuo hakina nafasi za kutosha (hostel) za watoto kulala hapo hapo.

Uongozi na serikali uangalie hili suala kwa manufaa ya hawa watoto.
 
Wanafunzi wa Chuo cha Ustawi— Institute of Social Work, Bamaga, Dar es Salaam wanalalamika ratiba za masomo zinazoenda mpaka Saa 4 Usiku. Hii inahatarisha usalama wao hasa wakati wa kurudi makwao huku wengine wakitokea mbali kama vile Gongo la Mboto, Mbagala, Tegeta; hii inapelekea kufika makwao sio chini ya Saa 6 Usiku.

Kero hii imeleta shida kwa wazazi na baadhi ya wanafunzi wa kike kudai kuwa wanahofia vitendo vya ubakaji na ukatili mwingine ikiwemo uhalifu nyakati za usiku.

Tunaomba uongozi wa chuo hiki kufuatilia jambo hili na kuweka ratiba vizuri. Vyuo vingine muda wa masomo mwisho saa 2 usiku.
Ukiachana na usalama hii sio ratiba ya masomo ila ni ratiba ya kuhalalisha matumizi ya ada. Vyuo vinadahili wanafunzi wengi kuliko uwezo wa miundombinu ndio sababu ya ratibu kufika usiku. Mamlaka ziingilie kati au ijulikane kama watu wanasoma usiku au mchana. Ukiukaji wa standards za elimu unazidi kuota mizizi kila kukicha ni hatari.
 
Tamaa ya pesa, unachukua wanafunzi wengi kuliko uwezo wa chuo.
 
Nimewahi kusoma kabla chuo hiko. Sio kana kwamba ratiba inaisha usiku bali ni maamuzi ya mwanafunzi mwenyewe kusoma asubuhi ama usiku.. Ratiba hiyo iliweka ili kusave wale wenye kazi zao mchana au majukum mbal mbal nao waweze kupata haki ya kusoma..
Ikiwa mtu angekuwa na tatzo hilo basi angebadilsha mwenyewe.
Mtanikosoa kama sipo sahihi..
 
Kwenye maombi ya kujiunga na chuo,
Mwanafunzi anatakiwa kujaza taarifa mbali mbali zikiwemo za anako ishi.
Kwamba ni rahisi kwa chuo kuangalia wanafunzi wake wengi wanatokea wapi?
je ni wangapi wako hostel? nk nk.

Mwanafunzi atoke saa nne usiku na kisha kuanza safari kurudi Kwao Tegeta, Gongo la mboto, kigamboni, kibaha,Bunju, Mbagala, pugu, Mbezi mwisho.
Halafu kesho yake asb awepo tena darasani!
 
Hao ni wa evining classes acha kukurupuka.hasa wafanyakazi
 
Uvivu tu pumbafu zao kabisa hayo mambo siyo Kuja kulalamika watu tulikuwa tunasoma hadi satano usiku Tena tunaish mburahati waache ujinga
Wanafunzi wa Chuo cha Ustawi— Institute of Social Work, Bamaga, Dar es Salaam wanalalamika ratiba za masomo zinazoenda mpaka Saa 4 Usiku. Hii inahatarisha usalama wao hasa wakati wa kurudi makwao huku wengine wakitokea mbali kama vile Gongo la Mboto, Mbagala, Tegeta; hii inapelekea kufika makwao sio chini ya Saa 6 Usiku.

Kero hii imeleta shida kwa wazazi na baadhi ya wanafunzi wa kike kudai kuwa wanahofia vitendo vya ubakaji na ukatili mwingine ikiwemo uhalifu nyakati za usiku.

Tunaomba uongozi wa chuo hiki kufuatilia jambo hili na kuweka ratiba vizuri. Vyuo vingine muda wa masomo mwisho saa 2 usiku.
 
Nmesoma evening class chuo flani dah ilikuwa bata kweli kweli.

NB: sikushauri umkubalie mkeo awe anasoma evening class
 
Aisee, hawa vijana wana kipindi cha masaa 4! Wanasoma nini exactly muda wote huo? Au wanapokezana!
IMG_20241103_225601.jpg
 
Halafu kesho yake asb awepo tena darasani!

Wanaotoka usiku muda wao wa kuanza vipindi ni saa10 jioni. Darasa la jioni liliwekwa maalum kwa ajili ya watu wanaofanya kazi na kuna utaratibu upo mwanafunzi ana uhuru wa kuchagua either asome jioni ama asubuhi ajabu kuna wanafunzi si wafanyakazi wanachagua masomo ya jioni na ndio shida inaanzia hapo.
 
Back
Top Bottom