Hatari ya kuwa na vikosi binafsi katika nchi yaonekana Sudan na Urusi

Hatari ya kuwa na vikosi binafsi katika nchi yaonekana Sudan na Urusi

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Yaliyoikumba nchi ya Sudan na kuingia kwenye vita vibaya vya wenyewe kwa wenyewe sasa yameingia nchini Urusi.

Wakati nchini Sudan kulikuwa na jeshi la RSF linaloongozwa mpaka sasa na Hemedti ambapo jeshi lake linasemekana kuithibiti miji yote mitatu mikubwa ya nchi hiyo. Kule Urusi kuna jeshi la Wagner chini ya Prigozhin na ambaye amepigana sana kuzuia mashambulizi ya Ukraine.

Baada ya kujiona ana nguvu kubwa ya kijeshi ya askari 25000 wengi wakiwa ni wafungwa na kwa kujua vikosi mahiri vya Urusi viko katika vita na jeshi la Ukraine na NATO kwa ujumla, yeye ametumia fursa hiyo kufanya uasi na kudai ana ugomvi na waziri wa ulinzi Shoigu pamoja na makamanda wakuu wa Urusi. Hata hivyo katika hali ya kushangaza ameunda msafara mkubwa wa vifaru kuelekea Moscow iliko Kremlin na aliko rafiki yake wa muda mrefu Putin.

Je, ni nchi gani nyengine Ulimwenguni zenye majeshi ya kujitegemea ambayo hayako chini ya kamanda mkuu moja kwa moja. Na jee kuna haja kweli ya kufanya hivyo.Na jee Tanzania haina vikosi mfano huo wa Urusi na Sudan ?
 
kuna thread niliandika ila Moderator ulifuta na jina lilikuwa mafahari wawili kuishi zizi moja kisa cha sudani.
kwa nini utazarau mawazo yetu.tokea kuanza vita sudani
 
China kajifunza
China mjanja huwa anapiga umbea tu na kusuta na kukata mauno kuhusu vita lakin kuanzisha vita we katu hatothubutu kwanza anajijua ana zana feki za kivita halafu ndo azipige eti na US? uchumi wa china unaitegemea ulaya magharibu na US ndiyo maana katu hawezi wavimbia hao atapiga kelele wee but no action.
 
Je, ni nchi gani nyengine Ulimwenguni zenye majeshi ya kujitegemea ambayo hayako chini ya kamanda mkuu moja kwa moja. Na jee kuna haja kweli ya kufanya hivyo.Na jee Tanzania haina vikosi mfano huo wa Urusi na Sudan ?
DRC
 
China mjanja huwa anapiga umbea tu na kusuta na kukata mauno kuhusu vita lakin kuanzisha vita we katu hatothubutu kwanza anajijua ana zana feki za kivita halafu ndo azipige eti na US? uchumi wa china unaitegemea ulaya magharibu na US ndiyo maana katu hawezi wavimbia hao atapiga kelele wee but no action.

Kwan china hajawai zichapa na marekani?tena enzi izo akiwa hana uchumi mkubwa hana technology kubwa.kama alieza enzi hizo saiv atashindwa nn??Unaongea vitu utazan havijawai tokea
 
Kwan china hajawai zichapa na marekani?tena enzi izo akiwa hana uchumi mkubwa hana technology kubwa.kama alieza enzi hizo saiv atashindwa nn??Unaongea vitu utazan havijawai tokea
Kweli china ya kwa Mpalange ilipigana na US na ikaishinda🤣😂
 
Kwan china hajawai zichapa na marekani?tena enzi izo akiwa hana uchumi mkubwa hana technology kubwa.kama alieza enzi hizo saiv atashindwa nn??Unaongea vitu utazan havijawai tokea
🤣🤣🤣 Chinese vs Super power 😅😅
 
Serikali za kijinga acha zipigwe tuu, hayo majeshi binafsi ni wananchi pia, asilimia kubwa ukiongoza vizuri na kwa haki hakuna mtu atakusumbua
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Chinese vs Super power [emoji28][emoji28]

Usiwachukulie poa kina jet lii [emoji23][emoji23]wanatoa kipigo wakiwa tungi au wazima
Refer to drunken master [emoji28][emoji28][emoji28]
 
Vichina vipo vingi alaf vidoncho doncho afu havikat tamaa marekani alikimbia uwanja wa vita pale mchina alipoingia kumsaidia korea
 
Kweli china ya kwa Mpalange ilipigana na US na ikaishinda[emoji1787][emoji23]

1950 mpk 1953 Korean war...china iliingia kuisapoti Korea na walafanikiwa kutoa majeshi ya us kwenye bwawa la roshin au changjin...nazan mpk china wametoa movie ya hio vita inaitwa battle of lake changjin...ukienda google watakuambia mechi ilitoka draw [emoji28]ila uhalisia unajulikana ...next time fanya research [emoji3166]
 
1950 mpk 1953 Korean war...china iliingia kuisapoti Korea na walafanikiwa kutoa majeshi ya us kwenye bwawa la roshin au changjin...nazan mpk china wametoa movie ya hio vita inaitwa battle of lake changjin...ukienda google watakuambia mechi ilitoka draw [emoji28]ila uhalisia unajulikana ...next time fanya research [emoji3166]
Kumbe movie bado nadaiwa sana
 
Back
Top Bottom