Hati ya nyumba Imechanwa alafu ikatengenezwa nyingine

Hati ya nyumba Imechanwa alafu ikatengenezwa nyingine

Yaan kwa aliyo yafanya kwenye familia yangu ya kuangamiza ndugu wa baba, baba yangu, Kaka yetu, na kuwafanya wengine vichaa ata sina muda kabisa wakumjua kabila lake.. ninachopambania sasa ni kulinda roho za ndugu zangu na ya mama yangu tusi angamizwe maana Kuna gonjwa moja alituma juzi kwa mama yangu lakutaka kumpofusha na kumfanya aparalize asifuatilie haki za watoto wake. nikaona hii imekuwa Too much.. alafu kuna baba mdogo moja tu kabaki kwenye ukoo ambaye alisomeshwa na baba yangu alikaa na kulelewa na mama yangu yeye ndio anajua siri ya ujenzi wa ile nyumba.. ndio anatupigania.. lakin juzi kafanyiwa jambo laajabu kwenye miguu hawezi kuinuka kutoka ndani anaumwa siyo kawaida.. ndio maana nina waza jinsi ya kumuwahi huyu Mama asiendeelee kuangamiza watu.
Uchawi upo na waganga wapo wazuri wachache waliobaki. Hakika huku jamvini kama una uhakika na mtaalam wa kusaidiwa hii familia tafadhali wasaidie ili wajikomboe. Mkishapata haki yenu mpumzisheni huyo mama maana ataendekea kuwatesa sana. Tit for Tat. Nimesikitika sana.
 
Kesi za kishirikina zina malizwa kishirikina au ki lokole,chagua moja hapo.
Ukiimaliza kwanza kwa njia moja wapo,hilo la hati halitakuwa gumu.
Anza na kushugulikia mzizi wa tatizo na sio matokeo ya tatzo..

Pili hata ww hauko salama sana,
Cha msingi tafuta nguvu kubwa zaid ya kukulinda na balaa la huyo mama,kama ni kuokoka okoka kweli kwa kumaanisha.
Ndo uweze kupambana nae.

Mark 3:27
[27]No man can enter into a strong man's house, and spoil his goods, except he will first bind the strong man; and then he will spoil his house.
Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.

Kama ulozi uwe mlozi kweli kweli.
 
Habari Wana Forum!

Naombeni wataamu wa haya mambo ya Hati za Nyumba wanisaidie kisheria hili limekaaje na je kuna msaada gani unaweza patikana ili haki itendeke!?

Ni hivi.. kwenye Familia Yetu Baba yetu alifariki miaka ya 2003 na akawa ameacha mke kule ndani Vikaao vya ukoo Vikasema kwa kuwa kimeachwa mtu mule ndani tumvumilie mpaka atakapo kuwa hayupo.

Nyumba hii alijenga Baba yangu na Mama yangu ila baadaye wakawa wamegombana na Baba baada ya kichonganishwa na huyu mwanamke aliye kuja kivamia ndani na kuanza ushirikina na hatimaye aka mteka akili mzee na sisi tukawa tumeondoka kwenda kuishi na Mama yetu.

Sasa baadaye Baba akafariki Ndio kule ndani akabaki yule mama.. tulipo dai nyumba yetu Ukoo ulisema tumuache akiwa hayupo kwa kuwa ni mzee watoto wata amua na nyumba yao. basi sisi kweli tukaendelea kupangisha mitaani na mama yetu.. hatimaye leo tumegudua Yule mama kachana ile hati ya Awali ya nyumba iliyokuwa imeandikwa jina la Baba yetu akachana na akaenda kutengeneza nyingine yenye jina lake.

Juzi ndio wamegombana na mwanawe wakike yule mwanawe akaropoka majirani wakasikia ndio sisi tukaambiwa kuwa kumbe hati ilisha badilishwa.

Tulipo mbana mtoto wake aliye mropokea mama yake kweli akasema mbona ilisha badilishwa tangu 2004 baada ya baba kufariki 2003.. Ambapo kwa sasa ina jina la huyu Mama.

Kiukweli tumeshangaa sana alitumianjia gani mpaka akapata yenye jina lake wakati Hajui ata tofali ya nyumba wala hakuwahi jua imehengwaje na walio jenga ni mama yangu na baba yangu tena kwa shida sana miaka hiyo wanafanya miradi ya kusambaza kuku na mayai ya kisasa kwenye mahotel miaka ya 1980 ndio wakaja wakajenga miaka ya 1983 sasa huyu mwana mke alipotuvamia tukaondoka baba akaanza kukaa naye.

Leo hii Hati isha badilishwa na jina kaweka lake.. Je sheria hapo imekaaje ndugu zanguni.. nifanyaje? Maana mwenye kujielewa kidogo aliye baki ni mm wengine huyu mama kawaharibu akili wamekuwa kama machizi.

Msaada wenu tafadhali.

Sent from my SM-N910C using JamiiForums mobile app
Mambo ya $$ tu. In tanzania, kwa mambo mengi sana pesa ndio ina-win. Kwa hio kama haujakaa vizuri kifedha sasa hivi, jipange. Huku ukiendelea kufuatilia kwa uwezo ulio nao ofisi mbalimbali. Ila ujue itakuwa ngumu bila pesa kutatua hilo. Na kama bado huyo mchawi ana pesa vizuri, kila ukimfunga bao, atalirudisha na kukuongezea mabao mengine. Hapo sasa ndio atalayeishiwa na $$$ mapema anasalim amri na ku-surrender. Japo unaweza bahatika bila pesa. Ila ni ngumu.
 
Inavyoonekana mko watoto nyomi mnaogombea mali ya urithi.. Hata mkiachwa wenyewe akaondoka huyo mama bado mtauana.
Kama marehemu kaamua kumgawia mama wa kambo nyumba na nyie mlifukuzwa ina maana marehemu hakuwahitaji kwenye mali zake, so ni bora mpambane na hali zenu mtafute vya kwenu kuliko kugombea mali za urithi.
Nadhani hujaisoma post yangu ukaelewa chanzo cha ugomvi .. mpaka baba anafariki Hati ya nyumba lisha andikwa ni nyumba ya mama yangu na watoto wake ila alipofariki tu yule mwanamke aliyebaki ndani maana alikuwa anaishi ndani akachukua ile hati alali akaichana akaenda tengeneza yenyr jina lake .. ila kimsingi haijui hiyo nyumba imejengwaje maana mama yangu na baba yangu ndio walio ijenga na tuazaliwa hapo na maisha yalikuwa salama mpaka miaka ishirin baadaye alipokuja kuingilia huyu mama ndio maelewano kati ya baba na mama yangu yakaanza kuvurugika mama akaeondoka na sisi mm nikiwa na miaka3 tu. leo hii am 29.
 
Uchawi upo na waganga wapo wazuri wachache waliobaki. Hakika huku jamvini kama una uhakika na mtaalam wa kusaidiwa hii familia tafadhali wasaidie ili wajikomboe. Mkishapata haki yenu mpumzisheni huyo mama maana ataendekea kuwatesa sana. Tit for Tat. Nimesikitika sana.
Kama una mjua mtaalamu nguli kweli kweli njoo inbox unisaidie maana sijawahi kupractice hii.. maana naambiwa waganga wengi ni matapeli.. sasa kama kutakuwa na gwiji wakurudisha hii haki yetu nakuzuia ndugu zangu wasiendelee kuangamizwa nitashukuru sana.
 
Nadhani hujaisoma post yangu ukaelewa chanzo cha ugomvi .. mpaka baba anafariki Hati ya nyumba lisha andikwa ni nyumba ya mama yangu na watoto wake ila alipofariki tu yule mwanamke aliyebaki ndani maana alikuwa anaishi ndani akachukua ile hati alali akaichana akaenda tengeneza yenyr jina lake .. ila kimsingi haijui hiyo nyumba imejengwaje maana mama yangu na baba yangu ndio walio ijenga na tuazaliwa hapo na maisha yalikuwa salama mpaka miaka ishirin baadaye alipokuja kuingilia huyu mama ndio maelewano kati ya baba na mama yangu yakaanza kuvurugika mama akaeondoka na sisi mm nikiwa na miaka3 tu. leo hii am 29.
Basi peleka kesi mahakamani.
 
kulipia ni elfu kumi ..

kapate kwanza uthibitisho wa hizo fununu then ndo uangalie hatua inayofuata,unaweza ukakuta jina wala halijabadilishwa kama ulivyoskia fununu
Asante kaka.. huwa unalipia kiasi Gani? na Je! kama itakuwa kweli ilibadilishwa.. nikakuta jina lake huyu Mama kuna njia gani naweza ifanya kupata haki yetu?
 
achukue na hii itamsaidia
Ni rahisi, nenda halmashauri ya wilaya au manispaa uliyopo uwaone watu wa idara ya ardhi. Omba kufanya upekuzi rasmi(official search) ambayo inagharimu shilingi elfu kumi. Utapata print out ya jina la current owner.

Lakini ili upate suluhisho la kudumi, itisheni kikao cha familia, na mpendekeze msimamizi wa mirathi. Andaa muhtasari alafu nenda mahakamani. Atakayetuliwa na mahakama ndiye atakayekusanya mali zote za marehemu na kuzigawa kwa warithi wa marehemu.

Hivyo, hata kama kuna forgery au fraud, msimamizi wa mirathi ana anauwezo wa kwenda mahakamani kudai ownership ya mali za marehemu.
 
Nenda halmashauri ofisi za ardhi,waambie unataka kufanya kitu kinaitwa "official search" ya nyumba yetu ( uwe na utambulisho wa nyumba kama plot number na block no )...watakutafutia file la nyumba yenu....kupitia hilo file utaona mwenendo wa umiliki wa nyumba yenu..kama kulibadilishwa umiliki utajua
Hili linawezekana lakini lazima awe na hati ya usimamizi wa mirathi.
Ukifika tu halmashauri au wizara ya ardhi swali la kwanza watakuuliza mhusika wa hiyo nyumba yuko wapi?
Ukijibu amefariki mimi ni mtoto wake, hapo ndio watakuomba hiyo hati sasa ya usimamizi.
Ndio maana kwenye comment yangu ya mwanzo nilisema kama hiyo hati ni Original basi itakuwa ameshirikiana na msimamizi wa mirathi waliyemteua otherwise basi itakuwa hati fake.
Cha msingi wakae kikao kama familia pamoja na wanaostahiki kurithi waandae muhtasari wa kikao cha kufungua mirathi halafu wamchague msimamizi,
Baada ya hapo huo muhtasari upelekeni ofisi ya s/mtaa au kata ukagongwe muhuri.
Bila kusahau muwe na cheti cha kifo cha marehemu (certificate of death) mnaambatanisha na muhtasari ambao umegongwa muhuri s/mtaa,kijiji au kata mnapeleka mahakamani.
Ukimaliza kufungua mirathi mtapewa hati ya usimamizi kwa mliyemchagua, yeye sasa ndio atafuatilia huko ardhi. Kwamaana nyingine msimamizi wa mirathi ndie mbadala wa marehemu.
 
Uchawi upo na waganga wapo wazuri wachache waliobaki. Hakika huku jamvini kama una uhakika na mtaalam wa kusaidiwa hii familia tafadhali wasaidie ili wajikomboe. Mkishapata haki yenu mpumzisheni huyo mama maana ataendekea kuwatesa sana. Tit for Tat. Nimesikitika sana.
Dah! Mambo gani sasa! Uchawi!!! Hakuna kitu hicho - ACHANA NA IMANI POTOFU! Nendeni ofisi ya ardhi ya wilaya baada ya kumpata msimamizi mirathi wa huyo kaka mkubwa- msianze kujiwekea vizingiti! Achaneni na uswahili!
 
Dah! Mambo gani sasa! Uchawi!!! Hakuna kitu hicho - ACHANA NA IMANI POTOFU! Nendeni ofisi ya ardhi ya wilaya baada ya kumpata msimamizi mirathi wa huyo kaka mkubwa- msianze kujiwekea vizingiti! Achaneni na uswahili!
Amini usi amini yanayotokea kwenye maisha yetu kama siyo uchawi basi ni Muujiza kutoka sayari inayo ishi kwa sayansi nyingine... kama huamin uchawi niulize mm niliyekuwa napinga sana ila sasa yamenitokea kwenye familia imebidi nielewe kuna uchawi dunian
 
Sisi tumeptia mchakato Huo ila
Tulidai mahakamani Mali(mchango wa mama Yetu katk nyumba Ile )

Zilifanyk tathamin ya mchangoz wa mama Tukapewa (mahak ilitoa umilik wa 40% wa nyumba ambako badae bab mzaz alitulpa Pesa)

NB
kumbuka hyo baba Yupo Hai KwahYo lilifanyik angalia Hai na Bado Yupo hai Sasa uko mbelen sijui itakuwaje

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Habari Wana Forum!

Naombeni wataamu wa haya mambo ya Hati za Nyumba wanisaidie kisheria hili limekaaje na je kuna msaada gani unaweza patikana ili haki itendeke!?

Ni hivi.. kwenye Familia Yetu Baba yetu alifariki miaka ya 2003 na akawa ameacha mke kule ndani Vikaao vya ukoo Vikasema kwa kuwa kimeachwa mtu mule ndani tumvumilie mpaka atakapo kuwa hayupo.

Nyumba hii alijenga Baba yangu na Mama yangu ila baadaye wakawa wamegombana na Baba baada ya kichonganishwa na huyu mwanamke aliye kuja kivamia ndani na kuanza ushirikina na hatimaye aka mteka akili mzee na sisi tukawa tumeondoka kwenda kuishi na Mama yetu.

Sasa baadaye Baba akafariki Ndio kule ndani akabaki yule mama.. tulipo dai nyumba yetu Ukoo ulisema tumuache akiwa hayupo kwa kuwa ni mzee watoto wata amua na nyumba yao. basi sisi kweli tukaendelea kupangisha mitaani na mama yetu.. hatimaye leo tumegudua Yule mama kachana ile hati ya Awali ya nyumba iliyokuwa imeandikwa jina la Baba yetu akachana na akaenda kutengeneza nyingine yenye jina lake.

Juzi ndio wamegombana na mwanawe wakike yule mwanawe akaropoka majirani wakasikia ndio sisi tukaambiwa kuwa kumbe hati ilisha badilishwa.

Tulipo mbana mtoto wake aliye mropokea mama yake kweli akasema mbona ilisha badilishwa tangu 2004 baada ya baba kufariki 2003.. Ambapo kwa sasa ina jina la huyu Mama.

Kiukweli tumeshangaa sana alitumianjia gani mpaka akapata yenye jina lake wakati Hajui ata tofali ya nyumba wala hakuwahi jua imehengwaje na walio jenga ni mama yangu na baba yangu tena kwa shida sana miaka hiyo wanafanya miradi ya kusambaza kuku na mayai ya kisasa kwenye mahotel miaka ya 1980 ndio wakaja wakajenga miaka ya 1983 sasa huyu mwana mke alipotuvamia tukaondoka baba akaanza kukaa naye.

Leo hii Hati isha badilishwa na jina kaweka lake.. Je sheria hapo imekaaje ndugu zanguni.. nifanyaje? Maana mwenye kujielewa kidogo aliye baki ni mm wengine huyu mama kawaharibu akili wamekuwa kama machizi.

Msaada wenu tafadhali.

Sent from my SM-N910C using JamiiForums mobile app

Fanya kazi acha kugombania mali
 
Back
Top Bottom