kubwa jinga jr
JF-Expert Member
- Mar 19, 2017
- 292
- 309
salaam wana bodi
bila kupoteza muda nianze na mada moja kwa moja,ni kipindi kama wiki Mbili hivi kila nikiamka asubuhi nakuta mtu amejisaidia (mavi) mlangoni kwangu,na linakokera zaidi huwa anapakaza kwenye kitasa cha mlango,
mwanzo nilifikiri ni walevi lakini nikajaribu kuuliza kwa majirani nikagundua kituko hiki ni mimi tu nafanyiwa,nikaongea na mke wangu,nikamwambia labda ni hivi vitu vidogo ninavyomiliki ndivyo vinavyotuletea karaha zote hizi yaani hii geregi ya kuziba pancha boda boda,baiskeli na kuchaji simu, ndio naletewa mzigo wa mavi ya mtu mzima, wenye harufu kali ,hata sijui huyu mtu kama anakunywa maji jinsi kinyesi chake kinavyonuka duuh pukeeh wacha niteme mate kidogo
Basi nikashauriana na mama watoto, mimi wacha niweke dago matanga ya nyati kwa usiku ili nimpate anaekunya, lakini siku ya kwanza sikumpata,sikukata tamaa usiku wa jana sasa ndio ikawa tamati ya huyo mkorofi anaekunya mlangoni kwangu,
Nilipokua nimejibanza taratibu kunako usiku wa saa tisa si ndio namuona mwanamke wa makamo mkononi ameshika ndoo na jembe,kwanza nilifikiri ni mtu anakwenda shamba lakini nilipokisia muda ,nikajiuliza shamba gani usiku wote huu hata kama kuchota maji lakini hapana,akaendelea kusogea kuja upande wangu mpaka akanipita karibu yangu,nikamuangalia kwa umakini huyu mama duuuh sikuamini yaani ni mama gire jirani yangu basi akaweka vifaa vyake chini alivyobeba
Nikamuona anaangalia kushoto na kulia akaanza kuizunguka nyumba aliporudi akaenda moja kwa moja mlangoni nikasubiri je anataka kugonga mlango au anataka kufanya nini,ghafla bila kuamini nilichokiona nikamuona ameinua nguo zake akabaki kipande cha chini mtupu na akachuchumaa na kuacha mzigo wa haja wa mavi na kuondoka kwa kasi kufuata vile vitu vyake na kuja ule usawa wangu,kama mshare nikamrukia nikamshika mkono na kumuuliza nini alichofanya... kwa kweli alitaharuki na kuomba msamaha nikamwambia lazima twende kwa mtendaji wa kitongoji,akalalamika sana yeye ana watoto wakubwa wa kike na wakiume pale, anaheshimika kama mzee wa kitongoji na mzee wa baraza la kitongoji sasa utakuwa umenivua nguo,
basi nikamwambia nenda kalale mashauri tutayamaliza kwa mtendaji asubuhi,
lakini mpaka muda huu ninapowaletea hii habari bado sijamueleza mtu na maamuzi sijachukua
Jamani wadau nauliza nimfanyaje huyu mama nichukue hatua gani au nimkaushie
bila kupoteza muda nianze na mada moja kwa moja,ni kipindi kama wiki Mbili hivi kila nikiamka asubuhi nakuta mtu amejisaidia (mavi) mlangoni kwangu,na linakokera zaidi huwa anapakaza kwenye kitasa cha mlango,
mwanzo nilifikiri ni walevi lakini nikajaribu kuuliza kwa majirani nikagundua kituko hiki ni mimi tu nafanyiwa,nikaongea na mke wangu,nikamwambia labda ni hivi vitu vidogo ninavyomiliki ndivyo vinavyotuletea karaha zote hizi yaani hii geregi ya kuziba pancha boda boda,baiskeli na kuchaji simu, ndio naletewa mzigo wa mavi ya mtu mzima, wenye harufu kali ,hata sijui huyu mtu kama anakunywa maji jinsi kinyesi chake kinavyonuka duuh pukeeh wacha niteme mate kidogo
Basi nikashauriana na mama watoto, mimi wacha niweke dago matanga ya nyati kwa usiku ili nimpate anaekunya, lakini siku ya kwanza sikumpata,sikukata tamaa usiku wa jana sasa ndio ikawa tamati ya huyo mkorofi anaekunya mlangoni kwangu,
Nilipokua nimejibanza taratibu kunako usiku wa saa tisa si ndio namuona mwanamke wa makamo mkononi ameshika ndoo na jembe,kwanza nilifikiri ni mtu anakwenda shamba lakini nilipokisia muda ,nikajiuliza shamba gani usiku wote huu hata kama kuchota maji lakini hapana,akaendelea kusogea kuja upande wangu mpaka akanipita karibu yangu,nikamuangalia kwa umakini huyu mama duuuh sikuamini yaani ni mama gire jirani yangu basi akaweka vifaa vyake chini alivyobeba
Nikamuona anaangalia kushoto na kulia akaanza kuizunguka nyumba aliporudi akaenda moja kwa moja mlangoni nikasubiri je anataka kugonga mlango au anataka kufanya nini,ghafla bila kuamini nilichokiona nikamuona ameinua nguo zake akabaki kipande cha chini mtupu na akachuchumaa na kuacha mzigo wa haja wa mavi na kuondoka kwa kasi kufuata vile vitu vyake na kuja ule usawa wangu,kama mshare nikamrukia nikamshika mkono na kumuuliza nini alichofanya... kwa kweli alitaharuki na kuomba msamaha nikamwambia lazima twende kwa mtendaji wa kitongoji,akalalamika sana yeye ana watoto wakubwa wa kike na wakiume pale, anaheshimika kama mzee wa kitongoji na mzee wa baraza la kitongoji sasa utakuwa umenivua nguo,
basi nikamwambia nenda kalale mashauri tutayamaliza kwa mtendaji asubuhi,
lakini mpaka muda huu ninapowaletea hii habari bado sijamueleza mtu na maamuzi sijachukua
Jamani wadau nauliza nimfanyaje huyu mama nichukue hatua gani au nimkaushie