Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Majungu tu, kwani chato wanakaa nyani? Kwani lazima ndege zote wapande watalii? Hacheni ubwe.ge kwani chato ipo sudan?
Hacheni-Acheni
sasa kama msamiati mdogo kama huo huwezi kuuandika ipasavyo tusiwashangae kweli?
 
na Bomba Dear lazima ziwe na route za huko....sasa ole wake atakayekaidi
 
Hii tabia yakuvutia mambo mazuri nyumbani kwa mtawala ipo siku yataligawa taifa, tutaanza kuchaguana kimakabila na kikanda kwa maana mkikosa mtu maendeleo hayaji.
Enewei huku Tanga tunasubiri upanuzi wa Bandari Itabidi tufanye jambo Shemweta nae aingie nyumba kubwa.
 
hahaha. Chato utakuwa mkoa muda si mrefu patachangamka kupita ARUSHA.
 
Aisee kumbe rafu zilianza kitambo sana.
Kaka mtenda akitendewa huwa inauma sana- WAKASKAZINI wameumiza sana wa kanda zingine. hebu fikiri inakuwaje mradi wa kilimo cha mpunga uweke Lower Moshi kule ambapo hata wali hawajui kuupika badala ya Msoga wanakokula wali kila siku- Sababu WAKASKAZINI ndio walikuwa makatibu wakuu wa wizara, hazina nk nk- KUTESA kwa zamu
 
Kaka hapo umezidisha chumvi; kwa taarifa yako hakuna ndege kutoka hivyo viwanja vidogo vidogo inaruhusiwa kuruka nje ya anga ya Tanzania BILA KUPITIA viwanja vikubwa
 
kuna barabara inajengwa pale kutokea Chato mpaka Serengeti mwendo wa nusu saa tu
 
kuna barabara inajengwa pale kutokea Chato mpaka Serengeti mwendo wa nusu saa tu
Wait lets be realistic chato mpaka serengeti?? mkuu kupitia wapi maana hata kama ni kupiyia ziwani haiwezekani iyo nusu saa
 
Mkuu hongera. Toka uzungumze stories za mbuzi kula almasi na mikiki mikiki yake. Nakuambia ukweli hata wale makomando wa Uhuru niliona wanadanganya kuwa ni makomando zaidi yako. [HASHTAG]#jamii[/HASHTAG] forum# happy new year
 
Mkuu hongera. Toka uzungumze stories za mbuzi kula almasi na mikiki mikiki yake. Nakuambia ukweli hata wale makomando wa Uhuru niliona wanadanganya kuwa ni makomando zaidi yako. [HASHTAG]#jamii[/HASHTAG] forum# happy new year
 
OTE="Brigedia Chan-ocha, post: 19084321, member: 213307"]Mkuu Barafu baada ya kuleta ile habari ya kwanza ya Uwanja wa NDEGE WA CHATO niliona nifuatilie sababu za Ujenzi wa huo Uwanja na umuhimu wake...

Findings....

Nimeelezwa kuwa, Rais Magufuli amejenga Uwanja huo CHATO ili aweze kuziteka nchi za RWANDA, BURUNDI, na UGANDA, Kwamba, Ndege za kutoka mataifa hayo zitatua CHATO INT. AIRPORT, halafu abiria watapanda Gari zao kutoka CHATO hadi MWANZA ambapo watapanda tena NDEGE kwenda wanapopataka ndani au nje ya nchi, (SIJUI NI AKILI GANI ILIYOTUMIKA HAPA) nimeelezwa kwamba, Rais Magufuli anataka kujenga DARAJA La BUSISI ili kurahisisha usafiri huo wa wageni kuja Mwanza kutoka CHATO INT. AIR.

Nimeelezwa kuwa, Mpango wa Magufuli ni Kuutenganisha mkoa wa GEITA Na CHATO hapo baadae, hivyo anaandaa mazingira ya kushawishi ugawaji wa MIKOA Hiyo, na makao makuu ya mkoa wa CHATO yatakuwa eneo moja linaitwa RUSUNGU hivi kama sijakosea jina, nakubali nirekebishwe maana nimesahau jina lake kwa usahihi.

Nimeelezwa kwamba, Eti CHATO kuna Mbuga ya WANYAMA binafsi ya RAIS Magufuli ila sijawa na uhakika na hili...

Kwa kifupi, hata kama Chato walikuwa na uhitaji wa uwanja wa ndege siyo sasahivi jamani, wewe fikiria, Plan zipo kwenye vitabu miaka mingi juu ya ujenzi wa viwanja kama MWANZA, MUSOMA Nk. lakini hadi sasa hakuna kilichofanyika kwenye viwanja hivyo, ila hiki cha chato ndo kiwe Urgent?[/QUOTE]
Kwanini kisinge jengwa Bukoba!!??
 
Geita unaijua? wapi utajenga uwanja wakati imezungukwa na milima, halafu watu walivyosongamana utamhamisha nani na umpeleke wapi? Mbona hamuulizi uwanja wa shinyanga uko ibadakuli km 50 kutoka shinyanga mjini.
 
Kwahiyo rasilimali fedha sio tatizo hivyo tujenge tu viwanja vya ndege kila mahali au unamaanisha nini?
Soma tena. Nimeandika kama kutakuwa na umuhimu wa kufanya hivyo.

Tunapinga ujenzi wa uwanja wa chato pasipo kutoa sababu za maana ndiyo sababu kuna ubishani hapa.

Sababu za idadi ya watu na za kiuchumi zina walakini kwani watakaotumia uwanja huo su wakazi w chato pekee.

Mchumi makini lazima aangalie na shughuli za kiuchumi zilizopo jirani na uwanja huo. Kwa sasa na baadae. Hapo ndipo tunapaswa kujadili.
 
Kipindi hiki mtatokwa sana ma Mapovu yako mengi yanakuja Chato kwetu.
Mnalipa kodi lakini? Au ndio ubabe kuwa kodi walipe watanzania wengine nyie mtumie kibabe kwa vile mko madarakani. Refer to Newton's Third Law of Motion
 
Kuna kaharufu kaubinafsi hapa,watanzania tusipokuwa macho kwa mara ya kwanza tunakwenda kumuzalisha Mugabe wa Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…