Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

Tetesi: Hatimaye "Chato International Airport" kuzinduliwa rasmi mwezi Aprili

"Eudorite, post: 19093534, member: 266448"]Soma tena. Nimeandika kama kutakuwa na umuhimu wa kufanya hivyo.
Tumekuuliza sana hutaki kujibu.

Tusaidie kuelewa umuhimu wa kujenga Chato ni upi kwa mujibu wa hoja yako?
Tunapinga ujenzi wa uwanja wa chato pasipo kutoa sababu za maana ndiyo sababu kuna ubishani hapa.
Hakuna anayepinga, tunahoji sababu za kiuchumi, kijaamii, kilinzi n.k.

Hakuna anayetueleza ni zipi ukiwemo wewe.
Tutaendelea kuhoji unless utueleze
Sababu za idadi ya watu na za kiuchumi zina walakini kwani watakaotumia uwanja huo su wakazi w chato pekee.
Ndiyo, tueleze kwa jiografia, shughuli za uchumi n.k. ni wakazi wa eneo gani jingine?
Mchumi makini lazima aangalie na shughuli za kiuchumi zilizopo jirani na uwanja huo. Kwa sasa na baadae. Hapo ndipo tunapaswa kujadili
Tueleze basi shughuli gani za kiuchumi ziwe Chato au kuzunguka hapo zinazoelekeza Ujenzi wa Chato airport
 
Maumivu ya kichwa huanza poolepoole,tumeanza na uwanja wa ndege Chato,tutakuja na Ikulu ya Tanzania Chato,tutafuata na kutoa maamuzi na uongozi wote wa nchi tukiwa Chato,mwisho tutahamishia serekali na makao ya nchi Chato.
 
Mbona hamuulizi uwanja wa shinyanga uko ibadakuli km 50 kutoka shinyanga mjini.
Umeleta hoja nzuri sana.
Kama tungetakiwa kujenga kiwanja basi ingekuwa Ibadakuli Inter airport

Williamson diamond -Mwadui imekuwepo kabla ya Uhuru.
Kilichopo ni uwanja mdogo wa kukidihi mahitaji ya eneo na wakazi

Wakazi wa Shinyanga hawahitaji uwanja wa ndege.
Walichohitaji ni MAJI, sote tukubaliane tu jitihada za Lowassa haziwezi kuwekwa pembeni

Kipaumbele hicho kimeinua maisha ya wananchi wa Shinyanga, kwa shughuli, afya na elimu. Mradi unaendelea hadi Dodoma

Huo ndio uwekezaji wa akili.

Leo Shinyanga ingekuwa na uwanja mkubwa, watumiaji pengine wangekuwa 500, kinyume na mamilioni ya watu wanaotumia maji sasa

Kipaumbele cha pili Shinyanga ni miundo mbinu ya usafiri

Tuliunga mkono uwekezaji wa reli ya kati katika kiwango cha SG ni muhimu.

Hakuna aliyelalamika in fact tulishangaa kwanini mradi haujaanza

Mradi wa Reli utasaidia shughuli za kiuchumi nchi nzima.

Utakuwa ni network kuanzia Mtwara hadi Musoma, Tanga hadi Kigoma.

Huu ni uwekezaji wa akili unaoweza kuelezwa kiuchumi, kijiografia, kiusalama na kijamii

Tunahoji, Chato imelenga nini?
 
Kwani

Wabunge wa Upinzani na Community yote ya Wapinzani mbona wamekaa kimya? Yetu macho na masikio. Hivi hapo Chato kila mkazi ana Maji safi ndani, hospital, shule,Na nyumba bora?
Wakiongea wanampa akili ya kufanya acha wakae kimya
 
Hiyo sio kweli.Kama ni kwa kiwango cha International airport hakuna phase inayoweza kutekelezeka na uzinduz kufanyika

Wataalamu wa Civil na structural engineering wanaweza kutusaidia kwa hili.Pia kabla ya kuweka uhakika unachosema rejea ujenzi wa Kiwanja chochote cha ndege unachokijua wewe utueleze phase ya awali kukamilika ilichukua muda gani na vitu gani vilikamilika
Miezi saba ishindwe kukamilika runway,kuweka windsock na eneo la Apron?
Mbona JNIA ile rehabilitation iliyofanywa na Interbeton ilikuwa inafanyika huku operations zinaendelea?
Kufikia April yaani kiezi saba tangu ujenzi kuanza,vitu kama runway,apron na uwekaji wa windsock vitakuwa tayari...

Heri ya Mwaka Mpya mkuu Ngapulila
 
Geita unaijua? wapi utajenga uwanja wakati imezungukwa na milima, halafu watu walivyosongamana utamhamisha nani na umpeleke wapi? Mbona hamuulizi uwanja wa shinyanga uko ibadakuli km 50 kutoka shinyanga mjini.
Hapana. uwanja wa shy ni km 8-10_) kutokana shy mjini
 
Tukundane

Tayari mmeambiwa shughuli za kiuchumi zilizopo karibu na chato na si kwamba wewe na mwenzako hamzifahanu.

Mmeambiwa kuna mbuga za wanyama hapo jirani na mashapo ya madini.

Hapo kuna potential kubwa ya shughuli za utalii uvuvi kilimo na uchimbaji wa madini.

Chato pia imezungukwa na miji inayokua kwa haraka na imetajwa hapa.

Makao makuu ya mkoa wa geita hapafai kujenga uwanja maana ardhi ni adimu na imejaa dhahabu. Huwezi jenga uwanja juu ya dhahabu. Hivyo chato airport itakuwa ni uwanja wa mkoa husika.

Mwisho niwaombe wewe na wenzio kuthibitisha kwamba chato panajengwa uwanja wa KIMATAIFA. Ni juavyo panajengwa uwanja wa kawaida kawa wa Tabora Dodoma au Mpanda. Hili la kusema Chato INTERNATIONA Airport ni upotoshaji na ni makosa.
 
Geita unaijua? wapi utajenga uwanja wakati imezungukwa na milima, halafu watu walivyosongamana utamhamisha nani na umpeleke wapi? Mbona hamuulizi uwanja wa shinyanga uko ibadakuli km 50 kutoka shinyanga mjini.


Kwa hiyo kumbe Geita maana yake ni Geita mjini? Sikumaanisha hivyo. Ninaifahamu Geita kwa upana wake, undani na uhalisia wake nadhani inawezekana kuliko hata wewe. Twende pamoja.
 
Kwa hiyo kumbe Geita maana yake ni Geita mjini? Sikumaanisha hivyo. Ninaifahamu Geita kwa upana wake, undani na uhalisia wake nadhani inawezekana kuliko hata wewe. Twende pamoja.
Kwa unavyoielewa Geita unafikiri huu uwanja ungefaa kujengwa wapi?
 
Kwa unavyoielewa Geita unafikiri huu uwanja ungefaa kujengwa wapi?

Ninatamani sana kujua nia ya kuujengea chato ilikuwa ni nini hasa. Pengine mtazamo wangu unaweza uwe mbali na malengo ya mwenye nao.
 
Ninatamani sana kujua nia ya kuujengea chato ilikuwa ni nini hasa. Pengine mtazamo wangu unaweza uwe mbali na malengo ya mwenye nao.
jamani huu sio Airport kama mnavyotafasiri ni Landing Airstrip tu kama zile za wamissionary wa MAF kule kibondo nassa ilongero au kama viuwanja vya mgodini, lakini misukule ya ufipa ndio imeshupaza shindo
 
I wish I could cry! Kuko wapi kumu enzi Baba wa Taifa Mwl. Nyerere(RIP) kwa Viongozi uchwara wa CCM?
Baba wa Taifa alikaa Ikulu zaidi ya miongo 2! Leo JPM ana mwaka tu tayari anajenga International Airport kwao! This is ridiculous.Baba wa Taifa hakuwahi kufanya ujinga kama huu! Hatuoni Kiwanja CHA NDEGE CHA KIMATAIFA PALE BUTIAMA wala MUSOMA yenyewe!
Je, Magufuli anafikiria nini huko mbele kwa muktadha huu?Je, yawezekana ni dalili ya kuanza kuweka mazingira ya kuitawala Tanzania kwa miaka mingi ijayo kama dikteta?
Mkuu inauma sana. Halileti mantiki hili kabisa. Sijui atakuja na sounds zipi kuhusu hili
 
Sasa ni dhahiri kuwa, kuanzia mwezi Aprili katika mapumziko ya Pasaka, Mkuu wetu atakuwa na uhakika wa kwenda mapumzikoni kwa kutumia uwanja wa ndege mpya wa Chato, yaani Chato Airport.

Kwa sasa uwanja huo unaotegemewa kukamilika mwanzoni mwa mwezi Aprili upo ktk kiwango cha vumbi na unaendelea kufanyiwa matengenezo hadi kiwango cha lami. Tayari ndege ndogo aina ya Beech Craft(King Air) mali ya kampuni binafsi ya TanzanAir imetua kwa mara ya kwanza ktk uwanja wa ndege wa Chato na hivyo kutoa uhakika kuwa sasa Chato inaenda kupokea ndege bila wasiwasi wowote.

Kwa mujibu wa taarifa,uwanja huo una kiwango cha "Aerodrome Reference Code 4D". Hizi "codes" hutolewa na ICAO (International Civil Aviation Organization) kulingana na ubora wa kiwanja kwa kuangalia aina ya ndege zinazoweza kutua, ukubwa wa ndege kwa maana ya uzito na upana wa mabawa.

Codes hizi zipo kuanzia 1A hadi 4F. Hivyo kwa kiwanja kuwa na Code 4D maana yake kimebakiza Code mbili tu kufikia kiwango cha mwisho cha ubora wa viwanja unaotambulika na ICAO.Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere "Code" yake ni 4E, hivyo uwanja wa Chato upo nyuma ya JNIA kwa "code letter" moja lakini upo sawa kwa "Code number" na JNIA kwa sababu vyote vipo kwenye "Code number 4".

Mfululizo wa "Aerodrome Reference Codes" huanza na 1A, 2B, 3C, 4D, 4E, 4F. Hivyo ni hakika sasa Chato Airport kwa kuwa na "Code 4D" inaenda kuwa moja kati ya viwanja vitatu venye kiwango bora Tanzania ikikaa nyuma ya Julius Nyerere na KIA. Uwanja wa Mwanza ni "Code 4D" hadi hapo ukarabati utakapokamilika utakuwa na sifa ya "Code 4E".

Hatuididimizi dhamira ya Mkuu kujenga kiwanja chenye ubora Chato, bali tunahoji kwa uelewa mdogo tu wa kanuni za Uchumi. Kwamba kiwanja hiki huko Chato kinaweza kuwa na matokeo chanya ya kiuchumi kama ambavyo wangeweza kuboresha uwanja wa ndege wa Mwanza?

Tunauhitaji Uwanja wa Mwanza kuliko ule wa Chato kwa sababu za kiuchumi ktk sekta ya Utalii. Tumekuwa tukilalamika sana kwa mbuga yetu ya Serengeti kukosa watalii wa kutosha kisa njia za usafiri kufika huko zilivyokuwa duni kushinda majirani zetu tunaopakana na mbuga ya Maasai Mara.

Uwanja pekee unaohudumia mbuga ya Serengeti kwa njia ya anga ni "Seronera Aistrip" ambapo huwa busy sana na huchukua ndege ndogo zenye abiria wasiozidi 50. Hii ndio moja kati ya "busiest Airstrip" kwa Tanzania.

Ili ufike Serengeti kupitia uwanja wa KIA unahitaji kutembea kilomita 284 kwa gari toka uwanjani, kwa kupitia uwanja wa ndege wa Arusha inakupasa utembee kwa gari umbali wa kama kilomita 226 wakati kwa kupitia Uwanja wa Mwanza,mtalii anatembea kilomita 166 hadi kufika geti la Ndabaka(?).

Kwa mahesabu hayo,kama ujenzi wa Uwanja wa ndege Serengeti ulishindikana,basi Uwanja wa ndege wa Mwanza ndio suluhisho la haraka ktk kuwafikisha watalii kwa urahisi ktk mbuga hiyo.Tukiusahau uwanja huo na kutazama zaidi ule wa Chato, tunaweza kuhoji dhamira hii ya maendeleo ktk kufika uchumi wa kati. Na kuhoji kwetu kusiababishe "hasira" kwa wenye mamlaka, bali ichukuliwe ni kama changamoto za raia kwa serikali yao.

Ukisefu wa usafiri wa uhakika na hasa ule wa njia ya anga, ndio unatukosesha mapato na kupunguza idadi wa Watalii ktk mbuga yetu ya Serengeti na hivyo wengi kuishia Maasai Mara.

Licha ya kuwa Serengeti ina ukubwa mara sita ya Maasai Mara,lakini bado "Vitanda" vya kupokea watalii katika hotel za Serengeti hivizidi 970 wakati wenzetu Maasai Mara ktk mbuga yao, kuna "Vitanda" zaidi ya 4,700. Hakika kupanga ni kuchagua.

Mpaka sasa Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania inamiliki viwanja vya ndege 58(ukijumlisha na Chato itakuwa 59),na wakati Uwanja wa ndege wa KIA ukiwa mikononi mwa Kampuni ya KADCO. TANAPA inamiliki karibu viwanja 26(Vingi vikiwa ni Airstrips),NCAA 2 na viwanja binafsi 93.

Katika hivi vya binafsi,vingi vinamilikiwa na wawekezaji toka nje ambao huvitumia kufanya udanganyifu ktk maliasili zetu.Uwanja wa ndege wa mgodi wa Geita(Mchauru) na Uwanja wa ndege wa Tishwa(HTSW) kule Loliondo unaomilikiwa na mtoto wa mfalme wa UAE ni moja kati ya viwanja vinavyopswa kutazamwa vizuri na serikali hii.

Uwanja huu wa Tishwa Loliondo ndio "unatisha", kwani huku ndege za familia ya mfalme hushuka moja kwa moja na kunyanyuka na mali nyingi. Umejengwa kiasi cha kuweza kutua na kuruka ndege kubwa.

Huu ndio uwanja ulio ktk eneo ambapo ukifika na kuwasha simu unakutana na meseji inasema "Dear Guest,Welcome to the UAE.Enjoy the best network coverage and other unmatched services only with Etisalat.Please use <+> or <00> before the country code for international calls.For directory services call 181,for availability of GPRS,MMS 3G roaming services call Etisalat Travellers help line 8002300 & for inquiries on Tourism,entertainment,shopping,etc call 7000-1-7000(Roaming rates apply).Have a pleasant stay in the UAE"

Labda wengine hatuna utaalamu wa Telecomunication, lkn kweli inawezakana hii kitu iingie tu kwenye simu yako wakati hujafanya "roaming". Haya ndio mambo ya TCRA kututoa tongotongo, sio zile mambo zao za .co.tz

Tunatakiwa tuwekeze ktk usafiri wa anga,lakini tuwekeza kimkakati na kwa faida za uchumi wa pamoja kama Taifa.Tukipewa sababu za kiuchumi zinazoupeleka uwanja wa ndege Chato wenye "Aerodrome Reference Code 4D" hatutakuwa na maswali.Tusipapata majibu yenye faida za kiuchumi,tutaendelea kuhoji hata tukiwa mafichoni.

Tukumbusha umuhimu wa Mwanza ktk kuihudumia Serengeti National Park, tutawakumbusha kuwa mlikuwa na mradi wa kujenge Uwanja wa ndege Serengeti,ila mkapambana na wanaharakati wa Ikolojia. Uwanja wa Serengeti ulipaswa kujengwa kati wa Kiwanja cha Ndege pale Mgumu.

Serengeti International Airport ilikuwa ni Code 4F, ilipaswa kuwa na runway ya mita 3,800 hadi mita 4,200.Mradi huo ulififia,sasa "tumefufukia" Chato na Uwanja wa "Code 4D".Je huku ndio kupanga na kuchagua??

Wakuu ukiyatafakari sana mambo ya nchi hii unaweza kuwa kichaa. Tuishukuru [HASHTAG]#Jamiiforums[/HASHTAG], inatupa wasaa wa kuhoji haya nyuma ya "keyboard". Mambo haya enzi za Waziri wa Maliasili Aboubakari Mgumia yaliondoa maisha ya Ndugu Stan Katabaro. Tunapouanza mwaka mpya, tuzame katika sala na maombi. Ili wale wanaoomba tuwaombee kila siku,tusiwaombee tu wawe na afya njema..Bali walegeze mioyo ktk kuishughulikia mitandao kama mtandao wetu pendwa wa [HASHTAG]#Jamiiforums[/HASHTAG].

Nawatakia Mwaka Mpya mwema. Ninafunga mwaka na "Chato Interantional Airport".... Panapo majaliwa hapo mwakani. Nitakuwa likizo huko kwetu porini.... Ciaoooo!!!!
Hivi, Chato IPO nchi gani?
 
Miezi saba ishindwe kukamilika runway,kuweka windsock na eneo la Apron?
Mbona JNIA ile rehabilitation iliyofanywa na Interbeton ilikuwa inafanyika huku operations zinaendelea?
Kufikia April yaani kiezi saba tangu ujenzi kuanza,vitu kama runway,apron na uwekaji wa windsock vitakuwa tayari...

Heri ya Mwaka Mpya mkuu Ngapulila
Upo makini kujibu.Tusubiri mwezi wa NNE mwakani kuhitibisha huu mjadala
 
Back
Top Bottom