Hatimaye Erick Shigongo Atajiunga na chuo mwaka huu

Hatimaye Erick Shigongo Atajiunga na chuo mwaka huu

Huyu jamaa ni kichwa cha hatari.kumbe hajawahi kukusanya course work.hivi angekuwa hata na diploama ingekuwaje.nadhani akimaliza wambakize afundishe Entrepreneurshi a.k.a somo la ujasiria mali.atawakomboa wengi.kwa sababu mimo namuona tayari anastahil Phd
 
Kumbe alikuwa hajasoma .
Kusoma sio kumaliza kila kitu, ila akili za ziada zinasaidia.
Nakumbuka Kuna jaamaa mmoja aliwahi kusema hivi.
"mimi sijasoma, nina nyumba nzuri, maisha mazuri, na chochote ninachokitaka napata."
Nashangaa Yeye kasoma lakini Hana maisha mazuri "alikuwa akimsema mtu.
Amesoma vitu tofauti na vinavyofundishwa mashuleni ndiyo maana hana vyeti
 
Amefuzu kusoma namba kwanza pale lumumba, sasa anataka kwenda chuo kabisa
 
Kumbe alikuwa hajasoma .
Kusoma sio kumaliza kila kitu, ila akili za ziada zinasaidia.
Nakumbuka Kuna jaamaa mmoja aliwahi kusema hivi.
"mimi sijasoma, nina nyumba nzuri, maisha mazuri, na chochote ninachokitaka napata."
Nashangaa Yeye kasoma lakini Hana maisha mazuri "alikuwa akimsema mtu.

Dunia ujanja kupata sio kuwai,...
 
Bill gate mwenyewe aliacha chuo akaenda kupiga dili zake mambo yalivyomnyookea akarudi tena chuo! Vyeti ni heshima tu lakini sio chanzo cha kukufanya ufanikiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
asilimia 100 ya wanaomdhihaki erick shigogo kwenye uzi huu,ni "mapumbafu na malofa" in mkapa's voice.
 
wanaccm kwa unaa utawaweza basi?!!! itakuwa kalipwa ama alitekwa masaa kadhaa akapigwa mikwala na pushap za hapa na pale akatishiwa kufungiwa beshara ya udaku akaona 'BORA YESHEE'......... in mzee Yusuph voice😱😱😱😱😱😱
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] mbele kwa mbele

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Elimu haina mwisho utashi wa kujiendeleza ili kupata maarifa zaidi ni hitaji la muhimu kwa ustawi binafsi wa mtu. na ikumbukwe lipo kinafsi zaidi na hujengwa na msukumo wa mtu husika kufuta ujinga. Sioni sababu ya kumshupalia Shigongo bali ni vema kumpongeza kwa kupambana na hali yake! Elimu hujenga ila kukuza maarifa ni haja yako binafsi wadau.
 
Apewe hongera sana na pia atumike kuhamsisha v9ijana siyo tu katika ujasiliamali, bali pia katika elimu formal. Nakumbuka mwalimu wangu mmoja aliyenifundisha darasa la nne mwaka 1972 akiwa na cheti cha grade C alipata Ph.D mwaka juzi baada ya kujiendeleza kukamua Dip.Ed(Chang'ombe), B.A (OUT), MA(Scotland) baadaye hiyo Ph.D pia huko huko nje ya nchi. Elimu haina mwisho!
 
Mjasiriamali na Mtunzi wa vitabu mashuhuri nchini Tanzania, Erick James Shigongo anatarajia kurudi shule na kusoma elimu ya shahada baada ya kuhangaika muda mrefu kutafuta nafasi hiyo, huku akisukumwa na masimango na matusi ya mitandaoni.

hqdefault-2.jpg

Eric Shigongo

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Erick Shigongo ameandika waraka mrefu akielezea safari yake kitaaluma na furaha aliyonayo, ya kuweza kufikia ndoto yake ya kuwa na elimu ya chuo kikuu, licha ya kuwa na mafanikio makubwa kwenye kazi zake za utunzi na maisha kiujumla.

“Ndoto imetimia, hatimaye naingia Chuo Kikuu, nikiwa mtoto nilitamani sana kusoma hadi chuo kikuu lakini sababu ya umasikini na mazingira magumu hasa shule nilizosoma, sikufaulu mtihani wa darasa la saba, nikarudia darasa la saba katika shule nyingine lakini bado sikufaulu, nilijiona mjinga! Nikajaribu kupitia njia ya ‘vikozi’ vidogo ili hatimaye niingie chuo kikuu lakini sikufanikiwa, nikaachana na ndoto hiyo na kuanza ujasiriamali”, ameandika Erick Shigongo.

Erick Shigongo alendelea kuandika akisema kuwa ndoto yake hiyo imefanikiwa baada ya kujiunga na mfumo wa RPL ambao hufanya watu wenye uzoefu fulani katika jamii bila kuwa na elimu, na kuwapa nafasi ya kusoma elimu ya juu, ndipo alifanikiwa kupata nafasi mwaka huu, baada ya kufeli mwaka jana.

“Nikakusanya vitabu vyangu ambavyo nimekwishaandika na kuvipeleke Tume ya Vyuo Vikuu na kuomba niruhusiwe kufanya mtihani huo, nikaruhusiwa, mwaka jana nikafanya na kufeli, sikukata tamaa, mwaka huu nikafanya tena na kufaulu, hivyo mwezi wa tisa ninaanza mwaka wa kwanza “, ameandika Erick Shigongo.

Chanzo: Bongo5
Mkuu mbona jamaa ana nyota ya kufeli,ccm alifeli,la saba alifeli akarudia akafeli,mahotel yamefeli,mtihani wa kujiunga chuo amefeli sasa huko anakoenda si ndo atafeli zaidi na kujikamua uhai?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom