Hatimaye gari la taka lapita kukusanya takataka mitaa ya Singida

Hatimaye gari la taka lapita kukusanya takataka mitaa ya Singida

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Singida taka.jpg
Februari 12, 2025, Mdau wa JamiiForums kupitia Jukwaa la Fichua Uovu alielezea kukerwa na tabia ya mamlaka zinazohusika na uzoaji taka mitaani katika Manispaa ya Singida kuwa na tabia ya uchelewaji wa kuchukua taka katika baadhi ya maeneo hasa Ginery, hatimaye taka zimeanza kuchukuliwa kutoka katika makazi ya watu leo, Februari 12, 2025.

Hali ilivyokuwa awali ~ Singida: Baadhi ya mitaa gari la taka halipiti kwa wakati, wiki ya 3 uchafu umezagaa mitaani

Awali, Mdau alidai Wananchi wanatoa taka nje siku ya kubeba wahusika hawaji kuchukua na kuwa hiyo ilikuwa ni wiki ya tatu hawajafika, taka zimezagaa kwenye mitaa tu.

Alisema hali hiyo inasababisha harufu kali mitaani, uchafuzi wa mazingira na kuhatarisha usalama wa afya za Watu kwa kuwa inaweza kuchangia maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

Leo Wananchi wengi wameonekana wakitoa taka na kuweka kwenye gari la kubeba taka ambalo lilikuwa halijapita takribani mwezi mmoja.

 
Sijui ni nani alileta wazo la kurundika viroba vya taka mitaani eti gari lije likusanye na kwenda kutupa huko nje ya mji! Mji unanuka uvundo kwa gari kuchelewa kwenda kukusanya taka hizo zilizotelekezwa. Bora vile vizimba vingeendelea kuwa sehemu ya kukusanyia taka na magari yakazoe huko kuliko huu mtindo wa kuchafua mitaa kwa viroba vya taka, ni uchafu mtupu
 
Uko tayari kizimba/Kontena/Ghuba liwekwe nje ya geti lako? Wananchi walete taka hapo.
huoni hayo ya sokoni, stendi, waliojenga hawakuona makazi ya watu? Unaambiwa huu utaratibu wa kurundika viroba mitaani tena barabarani si ustaarabu ni uchafu elewa hivyo
 
Singida kuchele.

Nakumbuka mwanzo wa miaka ya 1980s Dar es salaam (Upanga angalau) magari ya Halmashauri ya Jiji yalikuwa yanazunguka kuzoa uchafu mara moja kwa wiki.
 
Hilo tipa halibebi uchafu kwa njia salama linunuliwe gari lililoundwa kwa kazi hiyo , wananchi wanakatwa kodi
 
Back
Top Bottom