bigmind
JF-Expert Member
- Oct 28, 2015
- 12,457
- 12,689
Muda sasa takribani mwaka na miezi nasumbuana na huyu kicheche. Kicheche huyu bwana ni kama alikuwa anatumwa, amekula viranga na kuku wangu sana, huwa anafumua nyavu za banda na kutinga ndani usiku, anasomba vifaranga kimyakimya nikiamka mama kuku hana viranga.
Mara chache sana huwa inatokea mama kuku akistuka nitaamshwa na mayowe makubwa natoka nduki bandani mara mlango ukilia tu, huyo anasepa.
Sasa jana shetani wake kazidiwa ujanja na Mungu wangu akamtuma mapema sana, kabla ya saa mbili maana amezoea huwa anazamia mida ya wachawi usiku wa manane, jana nikiwa nipo nje napunga upepo natega nikaone taarifa ya habari nikasikia kelele za mama kuku, nikatoka nduki hadi bandani abadani USO KWA USO na huyo mbaya wangu kicheche, nilichofanya nikazima taa na kuwasha hivyo hali ile ili mchanganya sana KICHECHE akapotea njia yake aliyochonga kwa pesa ya makinikia.
Mungu saidia nikakimbilia upande alipo chonga njia, ile anataka apande nilimpa buti la haja, akatoa mlio kama simba, kidogo nijikojolee kujikaza kiume nikamuita mshikaji wangu njoo huku vita ni vita mura takenya mura waituuh..(hapa najua ni akina mwita na bhoke wameelewa).
Kicheche kanichimba biti, na Mungu saidia nikapata kipande cha ubao nikaenda naye SAKO KWA BAKO anakala rugu ya kichwa mara chini ila sema ukweli hii vita ilikuwa kubwa mno..! Mungu saidia nikawa nimeshinda vita na kicheche mwenyewe huyu hapa chini[emoji116][emoji116][emoji116]
Wataalam mnaojua vicheche njooni mtwambie huyu kicheche wa namna gani, na anawezaje kuishi mjini kabisa dsm, katikati ya mji maana sikai maeneo ya mashambani.
Nasubiri vita iendelee maana naamini atakuwa na familia niombeni nishinde vita hii.
ASANTENI .
Mara chache sana huwa inatokea mama kuku akistuka nitaamshwa na mayowe makubwa natoka nduki bandani mara mlango ukilia tu, huyo anasepa.
Sasa jana shetani wake kazidiwa ujanja na Mungu wangu akamtuma mapema sana, kabla ya saa mbili maana amezoea huwa anazamia mida ya wachawi usiku wa manane, jana nikiwa nipo nje napunga upepo natega nikaone taarifa ya habari nikasikia kelele za mama kuku, nikatoka nduki hadi bandani abadani USO KWA USO na huyo mbaya wangu kicheche, nilichofanya nikazima taa na kuwasha hivyo hali ile ili mchanganya sana KICHECHE akapotea njia yake aliyochonga kwa pesa ya makinikia.
Mungu saidia nikakimbilia upande alipo chonga njia, ile anataka apande nilimpa buti la haja, akatoa mlio kama simba, kidogo nijikojolee kujikaza kiume nikamuita mshikaji wangu njoo huku vita ni vita mura takenya mura waituuh..(hapa najua ni akina mwita na bhoke wameelewa).
Kicheche kanichimba biti, na Mungu saidia nikapata kipande cha ubao nikaenda naye SAKO KWA BAKO anakala rugu ya kichwa mara chini ila sema ukweli hii vita ilikuwa kubwa mno..! Mungu saidia nikawa nimeshinda vita na kicheche mwenyewe huyu hapa chini[emoji116][emoji116][emoji116]
Wataalam mnaojua vicheche njooni mtwambie huyu kicheche wa namna gani, na anawezaje kuishi mjini kabisa dsm, katikati ya mji maana sikai maeneo ya mashambani.
Nasubiri vita iendelee maana naamini atakuwa na familia niombeni nishinde vita hii.
ASANTENI .