Mkuu
FUHRER
MIE kila siku huwa Nasema mijitu mijinga itaendelea kuteswa Na kuuliwa kila mchao.. Na UOGA Wa Mjinga ni Upumbavu wake.. Embu ona Soga hili la Mfano.... Masharubu kavamia Nyumba yako Usiku Na midude mingine yenye Silaha, wamevunja mlango Na kuingia Ndani Na kuwaamuru mlale chini, Kwa nasibu ukagundua mmoja wapo Wa midude hiyo ni bw masharubu, Na Kwa msaada wa taa ukamuona sawia Yeye Na Sauti yake lakini ukafichama asijue umemgundua, baada ya vichapo, Wizi Na uharibifu Mwingi midude wale wanaondoka. Now Kwa mtete mnajiundaunda Na familia yako kabla ya polisi kuja Kama kawaida nusu saa baadae enewei a-b zao zinaendelea ila sirini unayo Kwamba bw masharubu was the leader.
Mjinga weye ati kesho wajitokeza mediani Na kuanza kubwabwaja.. Ooo aliyeniteka ana sharubu hivi, ana sauti ya hivi Na vile, ni mrefu hivi Na vile .. Huku unashusha wajihi wa bw masharubu nae anakusoma tu Kwenye media ila hujamnanga direct Kwa jina Bali Kwa upumbavu unaongelea wajihi wake, lazima atagundua umeshamfaham Na Kwa mantik hiyo lazima akuwinde akifanyizie Kwa Sababu kumbe umeshamgundua.. Ndivyo wajinga hupwetwa hivyo..
Wewe Kama huna uhakika sema SIJUI---FULL STOP, Na Kama wajua weka mambo HADHARANI.. Sema ni huyu Na Yule pale Na nanihii ndio walio ninanihii.. Ukishawataja nguvu kweisha.. Hawawezi kukudhuru tena Kwa Sababu wakikugusa jamii yote Itajua ni Flan.. Take it from here...