Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,515
- 28,506
Miezi michache tu baada ya staa wa Hip Hop Bongo, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kuripotiwa kutoka na msichana anayejulikana kama Chaga Baby, hivi sasa yupo na mrembo raia wa Ethiopia (Mhabeshi) anayejulikana kwa jina la Addi na ameapa kufunga naye ndoa.
Nay na mwanadada huyo ambaye ni msanii wa filamu, kwa sasa wanapoelekea ni pazuri tofauti na wapenzi wengine waliopita, kwani huyu humzungumzia kila wakati.
“Nimesharukaruka vya kutosha, sasa nimetulia na mchumba wangu huyu Addi tuliyekutana uwanja wa ndege huko Afrika Kusini wakati nikiwa narudi Bongo na yeye anarudi kwao, tangu hapo tulianza uhusiano na tunae-ndelea vizuri.
“Sija-wahi kusema kuhusu kuoa, lakini kwa huyu ndiye mke wangu ajaye maana tulipofikia ni pazuri, anawapenda sana watoto wangu, sitaki Wabongo wamzoee maana wataniharibia na maneno yao,” alisema Nay.
Staili ya kukutana kwa wapenzi hao, inafanana na ilivyokuwa kwa Diamond na Zari, ambao pia walikutana ndani ya ndege nchini humo, lakini wenyewe wakiwa na uelekeo mmoja wa Dar es Salaam.
Pamoja na hayo Nay amewachana katika video mastaa kadhaa wa kike wa Bongo Movie na Bongo Fleva kuwa wamezidisha kudandia vitoto wanavyovizidi umri.
Source: Bongo Movie