Hatimaye mwanaume mmoja ajitokeza pale Uingereza

bryan2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,323
Reaction score
4,679
Yaa tunaweza kusema mwanaume baada ya leo kumkalisha mtu ambaye amesumbua sana vijana na wazee wa pale Uingereza Msumbufu amewatandika bakora karibia wazee na vijana wote pale kwa malkia tena bakora za moto haswa.

Cystal Palace hatimaye leo ameonyesha kwamba yeye ni mwanaume tena wa shoka baada ya kumzuia mancity kuendeleza wimbi lake la ushindi na kwenda naye Suluhu ya bila kufungana.

Nusura vijana wa kocha mwenye makeke mengi Pep Guardiola waangukie pua baada ya Wanaume hao kukosa mkwaju wa tuta dakika za lala salama.

Sio mbaya makocha wakaanza kuomba ushauri kwa Roy Hodgson.
 
Kweli City kawashika pabaya. "Mwanaume" kwa kuambulia draw?
 
Wewe utakuwa ni mmoja wa wahanga wa gharika la Guardiola.....
Exactly mkubwa ndo maana leo cystal palace wanapata pongezi sio mchezo vijana wamekaza.

Sikuwahi kudhani kuwa mancity inamashabiki Tz au ni kakundi cha Arsenal,Chelsea,liverpool wameungana.
 
Kweli City kawashika pabaya. "Mwanaume" kwa kuambulia draw?
Hebu niambie nan kala drawa zaidi ya ile ya mwanzo?

Angalia na usajili wao na nani alikua home.

Au wamekuchania mkeka nini?joking
 
pongez zangu za dhati kwa crystal palace...nisiwe mchoyo wa fadhila..
 
M cty mbeleko za marefa zinawabeba sana, bado sijaona sababu ya kupeleka mpira mpaka dk ya 98
 
Wanabebwa sana na marefa sijui mashabiki wanaliona au wamepofushwa. Wamewaachia manyoya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…