Hatimaye Treni ya Dar-Arusha imeumaliza mwendo. Ilisaidia sana changamoto ya usafiri, itakumbukwa na wengi

Hatimaye Treni ya Dar-Arusha imeumaliza mwendo. Ilisaidia sana changamoto ya usafiri, itakumbukwa na wengi

2019

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2018
Posts
3,130
Reaction score
4,735
Screenshot_20240629_090024.jpg

Kwenye mtandao wa kukata tiketi za treni ya Deluxe kutoka Dar es Salaam hadi Arusha ni rasmi imekufa. Nakumbuka usafiri huu ulisaidia sana changamoto ya usafiri hasa kwa watu wa kipato cha chini na cha kati.

Hata mimi nilipanda baada ya kuona inasifiwa sana na ilikua na vibe la kweli

Nauli kutoka Dar hadi Moshi daraja la 3 ilikua 16500,kila msafiri aliweza kumudu tofauti na mabasi ambayo ni zaidi ya 40,000.

Mradi huu ambao kabla ya kufufuliwa na Magufuli ulikuwa umekufa kwa miaka zaidi ya 30,rais Magufuli akapambana na kuurudisha pamoja na kukarabati vituo vyote vya mkoloni na kujenga vya kisasa.

Nini kimeuwa ruti hizi? Tukisema ni hujuma za wenye mabasi na malori tutakosea? Au ni uzembe wa serikali tutakosea?

Kwanini mpaka sasa shirika la reli liko kimya kutangazia umma kuwa hiyo ruti imekufa?.

USHAURI WANGU KWA SERIKALI
Kwa kweli nikizoom hali ya sasa ya watumishi wengi serikali si makini kwenye usimamizi. Rejea hali ya mabasi ya haraka (mwendokasi) mradi wa Mbagala umekamilika lakini hakuna magari. Iyo hali ya trc hata SGR muda utaongea tu n.k

Serikali kupitia TRC itoe kibali au ibinafsishe hiyo reli iendeshwe na kampuni au taasisi ya binafsi naamini mambo yatakuwa mazuri sana.


View: https://youtu.be/2dUbS5zZkK0?si=ptd_kKrdlvRH8-RZ
 
Utasikia, "....mradi haukuwa na tija, Mwendazake kakurupuka....", kumbe nchi imewashinda.
Matajiri wameishika serikali pabaya sana, kila mradi naamini utakufa, ili wao waneemeke na mema ya nchi huku rais akiwa bize na safari za nje
 
Kampuni za mabasi na malori watafuna nchi wanahisa huko, wasingeweza kuruhusu haya yatokee. Next ni SGR itakata roho mchana kweupe
 
Sasa imekufaje kabla sijaipanda jamani? Naombea liwe ni suala la muda mfupi irudi kufanya kazi nami nipate experience hiyo.
Ukisikia limerudi hata kwa dharura tu, nistue chap, tiketi nitakulipia mimi.
 
Back
Top Bottom