figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
Wanachama Yanga wamkabidhi Yusuf Manji aiendeshe Yanga kama klabu binafsi, mikataba ya kumkabidhi nembo kusimamiwa na Baraza la Wadhamini.
Katika mkutano huo unaofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam kipindi hiki, Manji amesema amepeleka ombi la kuikodisha Yanga kwa miaka 10.
“Nitaikodisha kwa asilimia 75 na 25 inabaki kwa wanachama. Nataka kuikodisha timu na nembo, majengo ya klabu yanabaki kuwa mali ya wanachama.
“Katika miaka 10, ikipatikana faida 25 inakwenda kwa wanachama na klabu na 75 kwangu. Kama itakuwa ni hasara basi inakuwa hasara yangu, hakuna hasara upande wa wanachama au klabu,” alisema.
Manji amesema masuala ya timu kuhusu usajili, mishahara, uendeshaji kama safari na gharama nyingine zitakuwa chini yake
Wakati huo huo, Wajumbe watatu wa Kamati Utendaji ya Yanga Ayoub Nyenzi, Hashim Abdallah na Salum Mkemi wavuliwa uanachama wa klabu hiyo.
Katika mkutano huo unaofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam kipindi hiki, Manji amesema amepeleka ombi la kuikodisha Yanga kwa miaka 10.
“Nitaikodisha kwa asilimia 75 na 25 inabaki kwa wanachama. Nataka kuikodisha timu na nembo, majengo ya klabu yanabaki kuwa mali ya wanachama.
“Katika miaka 10, ikipatikana faida 25 inakwenda kwa wanachama na klabu na 75 kwangu. Kama itakuwa ni hasara basi inakuwa hasara yangu, hakuna hasara upande wa wanachama au klabu,” alisema.
Manji amesema masuala ya timu kuhusu usajili, mishahara, uendeshaji kama safari na gharama nyingine zitakuwa chini yake
Wakati huo huo, Wajumbe watatu wa Kamati Utendaji ya Yanga Ayoub Nyenzi, Hashim Abdallah na Salum Mkemi wavuliwa uanachama wa klabu hiyo.