Tajiri Kichwa
JF-Expert Member
- Apr 2, 2017
- 9,021
- 22,016
Labda nianze kwa kuwatoa wasiwasi wale wanaodhani nitasusa Uzi, Hilo haliwezi kutokea, na sikatazi mtu kutoa maoni yake hata mkinitukana mimi nitayasoma tu na uzuri ni kwamba mimi nikiwa free kama hivi huwa nasoma kila comment, hata aliyecomment nukta huwa napitia comment yake
Iko hivi, nilishindwa kutoa muendelezo jumapili Ile iliyopita kama nilivyoahidi kwasababu jumamosi yake nilisafiri na Mzee nimekuja nae Mwanza, na hadi leo hii tupo huku ila tunategemea kurudi week hii hii kama mambo yataenda sawa kama alivyopanga
Na muda mwingi nipo pamoja na Mzee, muda ambao naacha na Mzee ni ule muda wa kwenda kulala tu, sasa siwezi kuwa na Mzee tumekaa Mahali halafu mimi nipo Busy na simu naandika story, (labda mtasema kwanini nisiandike usiku muda ambao nakuwa peke angu) Huo usiku nao nakuwa nimechoka kwanza natakiwa kuwaza ratiba za siku ya kesho yake, so muda kama huo nautumia kupumzika
Yani ni vile tu hamjui na ndio maana nikiona mtu anatoa maoni yake kwa makasiriko mimi huwa hata sikasiriki wala kumshangaa, kwahiyo nikisema niwaendekeze ili kuwafurahisha naweza kujikuta naharibu sehemu nayopatia ugali kwasababu upande mmoja nita loose focus
Kuandika story (labda kichwa changu ni kizito) huwa inanichukua hata siku nzima, nimemshangaa yule jamaa aliyesema Dakika 20 tu inatosha kuandika episode 1, blaza shida sio kuandika tu kwasababu hii sio story ya kutunga, shida ni kukumbuka matukio, mf mdogo ni zile sehemu Caryn anazotema Yai,
Ivi mnajua kwamba asilimia 90 ya conversations anazofanya Caryn ni za Kingereza, na ili story ivutie inanibidi nipite mule mule lakini ninachokifanya kwa baadhi ya sehemu mimi huwa natafsiri maongezi yake kwasababu nikisema niandike Convo zake kama zilivyo kuna baadhi ya watu hawataelewa, kwanza mm mwenyewe kuna misamiati mingine anayoongea siielewi maana yake, so natumia ujanja wangu kuunganisha maneno
SO nimesema huwa inanichukua siku nzima kwasababu ya kukumbuka matukio na kuyapangilia, na siku zote nikimalizaga kuandika episode huwa naipitia kuisoma zaidi ya mara tano, sometimes naweza nisipost siku hiyo niliyomaliza kuandika nikaja kuipost siku inayofuatia, yote hiyo ni ku make sure hakuna tukio muhimu nililolisahau kwasababu ilishanitokea nimepost episode nikaja kukumbuka Kuna Mahali niliruka
Halafu katika maisha usijilinganishe na mtu mwingine, Mimi kunifananisha na watu wengine wanaoleta story humu ni kunikosea, kwasababu I'm sure tumetofautiana katika kila kitu hadi katika ku priorities mambo
Mimi mwenzenu focus yangu ipo kwenye kazi ambayo inaniweka mjini huku Jamii forum huwa nakuja kuchungulia tu nikiwa free kama hivi, na naamini pia nyie mna kazi zenu zinazowaweka mjini mkishapiga pesa huko mtaani ndio mnakuja kuchungulia humu kama BM kaleta muendelezo
Sasa kama Mimi mwenyewe hii story siipi umuhimu wa hivyo kwanini wewe ujichoshe kwa kuipa kipaumbele namna hiyo, kama ni muhimu sana basi wekeni Dau nikirudi Dar nishushe Episodes back to back kwasababu Mzee kaniambia tukirudi nipumzike siku Saba lakini siwezi kufanya hivyo mimi nina maisha gani ya kupumzika bhana, japokuwa nikipumzika mshahara wangu upo pale pale lakini nikienda job ndio napiga hela zaidi
Narudia tena fanyeni kazi hapa tunakuja kubadilishana mawazo na kuburudishana tu....au inawezekana wenzangu mnapiga pesa huku mmekaa!? kama ndio hivyo wekeni Dau mezani na mimi nipige pesa huku nimekaa kwa kuandika story. Mkifanya hivyo mm nitapumzika hiyo week moja ya Mzee aliyonambia na focus yangu yote nitaihamishia hapa......Deal???
Kwaherini bhana Mzee ni kama anakaribia kutoka lunch time hii
Wale mliokua mnataka episode iyo hapa. Tusubiri inayofata sasa