Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Aaaaaah kumbe mkuu swala la kuamua kuleta humu story ni wewe tu na wala sio ubize wala nini.. Maana hapo unasema ulikuwa na MPANGO wa kuleta hiyo story tarehe 5 March ila kwa kuwa umeguswa na comment ya mwamba unasema utaiwahisha.....Safi. Ila hapa chini nina barua yako ya wazi


With all Due respect, siamini kama wewe ni the most busiest person humu ndani. Naheshimu muda wako unaotumia kuandika hii story ila imekuwa too much.

So inaonekana unakaaga nyuma ya keyboard afu unaenjoy vile watu wanakuw craving na story yako. Mnapata raha gani nyie jamaa kuona watu wanahangaika kuingia na kutoka kwenye nyuzi zenu ili kuona kama kuna updates?

Hata kama haulipwi, kwanini uliamua kuanza kuiandika wakati unajua ni ndefu na hauna muda wa kuandika? Najua watakusaidia kunipopoa kuwa sijalazimishwa kuisoma ila inabidi ujue, the first time mtu yeyote anaamua kupublish story humu ndio first time anapoteza umiliki wa ile story...inakuwa ni mali ya wote.

Afu kuandika sio kazi kama hivyo ambavyo huwa mnajaribu kuexaggerate humu ndani. Hakuna episode hata moja kati ya zote ambazo umeziandika humu ndani ambayo ulitumia zaidi ya dakika 20 kuiandika. HAKUNA!!

Kwahiyo kati ya masaa 24 kwa siku unakosa dakika 20 kuwapa watu wako kitu ambacho kitawasaidia kuua addiction yao ambayo umewapatia?....Let's assume we ni mwanamme na unapenda soka, pamoja na kuwa busy sana lakini hukosi dk 90 za kuangalia games za soka....Unataka kuniambia huangalii mechi na kila kitu chako kimestop kisa ubusy?

Sasa kwanini ukose dk 20 tu basi kwa siku 2 kuandika episode ndefu?....

In long run nashauri Moderators waweke condition mtu yeyote anayeanzisha humu story asiipublish hadi awe ameitimiza yote.

Hii tabia ya watu kuona raha wenzao wakimtag tag kwenye uzi wake ni ya ajabu sana.
Ila watoa story daily nyenyenye ubusy ubusy....NONSENSE!!!

Mimi napongeza watoa story wengine kama Kigakoyo.....Jbourne96.....SinganoJr....pamoja na umughaka....wanajitahidi sana sana sana.

Sio nyie wengine ambao kiepisode chenyewe unatumia siku 15 kuandika na hapo umeliliwa sana.

Kuna mwenzako mwingine aliletaga story yake, baada ya kuona attention ya watu imekuwa kubwa...akaanza kuvimba na kuona raha kubembelezwa....matokeo yake kuna siku akalopoka "leo nilipanga niwape episode 3 ila kwakuwa taifa limepata msiba naomba tuendelee kwanza na maombolezo" [emoji1][emoji1]

Najua utasoma hapa. Vyovyote utakavyochukulia na kutafsiri ni sawa tu as long as naelewa nakwambia ukweli na inabidi ubadilike....

1. Ni either usiendelee nayo na uishie hapa hapa maana sio kwamba ni special kiviiiiile kuliko kunata kiasi hiki.

2. Or uendelee nayo na uwe na consistency kuliko kuwakosea watu hivi. Eti hadi sahizi bado hujamaliza matukio ya November mwkaa jana [emoji3][emoji3][emoji3]

Maswala ya kuleta excuse kuwa ooooh kuandika ni kazi sana kuliko kusoma mara sina muda....HATUKUKULAZIMISHA KUILETA.

Wale watakaokusaidia kunipopoa kuwa sikulazimishwa kuifatilia wajue tu kuwa HII STORY HAINIONGEZEI WALA KUNIPUNGUZIA CHOCHOTE. Ila nipo hapa kuwakilisha watu wanaokereka ndani kwa ndani. Mnawapa addiction kwa sababu za kipuuzi.

NB: Hii barua nimeiandika kwa dk 6 tu....Assume ningeandika kwa dk 20 si ingekuwa ndefu kama episodes 4 za nyie masimuliaji....

Afu eti mtu bila aibu anaanza oooooh tatizo muda wa kuandika nakosa....ULILAZIMISHWA KUILETA? au ulitegemea nini wakati ulijua huna muda?


Acheni kutaka umuhimu/trending isio na faida.

Kuna mwamba anaitwa SINGANOJR.....anasimulia story yake ya jamaa naitwa ROMA. Hadithi ni ndefu hadi sahizi kafika episode ya 320....Episode yake moja ni kama episodes 3 za hii story yako lakini jamaa hazingui....Yeye ni Jumanne anakupa episodes 3....Jumamos anatoa episodes 3....Safi kabisa maana anatimiza wajibu wake. Ndiyo, ni wajibu kwasababu yeye ndio aliianzisha. Hakuna mtu aliyejua wala kumuomba. So anatimiza wajibu wake.

BM acha visinvizio. Acha kutafuta trending na cheap popularity....Acha kujifanya uko busy zaidi ya nini sijui. Acha dharau kwa mashabiki zako. Huwezi kukosa dk 10 kila siku za kuandika hii story kwenye kifaa chako. Then baada ya wiki unaituma episode moja ndefu sana iliyotumia dk 70 kuiandika.


Lakini haya maswala ya kuwaweka watu onhold kwa wiki 4 halafu unakuja na kiepisode kimoja cha maneno 950 ni USHAMBA!!!
Umemchana vizuri kabisa japo hatujui nini kimemsibu unaweza kuta kaugua labda. Pamoja na kia story yake nzuri sema ikikaa sana ina bore coz inapoteza hata kumbukumbu za matukio ya mwisho ili kuunga story inayoendelea. Kama ana busara akusikilize na abadirike.
 
Mimi napongeza watoa story wengine kama Kigakoyo.....Jbourne96.....SinganoJr....pamoja na umughaka....wanajitahidi sana sana sana.
Kunae na huyu mwamba mwingine wakuitwa mireille aisee jamaa ni shenz kabisa,mwamba anazitiririsha kama hana akili vizuri,ukisoma hiyo utampa salute,post alitupia kwa siku 1 tu wewe unasoma wiki nzima na ni tamu blaa😂,
I salute you mwamba
 
Sijawah kuona mpuuzi na mshamba kama ww...mwehu kabisaa...na ulaaniwee...yaan mtu anajitolea tuu...hujui hta anapitia nn...na dole lako gumba tena limekomaa kwa kuandika upuuzi kama huu.....yaan umeandika as if umekatwa kichwa...ww ndio mbinafsi kabisaa....hivi inaingia akilin kwel kwel unaandika utumbo kama huo...kupitia tuu story yake kuna watu ana wainspire kimaisha.....kuachana na burudan anayo itoa...tena shukuru Mungu Hii ni jamii forum...ningekushikisha adabu...ww ni mbinafsi sana..
Wewe ni popoma

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Ilipoishia

Ikabidi tu nimuelewa japokuwa anachokiongea kina make sense ila naona kama ana complicate sana mambo, tukaweka Kila kitu sawa Ilivyofika saa mbili kasoro tukarudi hotelini

Tukapiga msosi tukamaliza tukaelekea vyumbani, chumba changu hakipo mbali na chumba Cha Caryn, nilivyofika tu kwenye room yangu nikaingia bafuni kuoga, natoka bafuni namkuta amekaa kitandani nikajua tu huyu amekosa usingizi anataka tukeshe tukipiga story

BM: "Vip kwema?"

Caryn: "Itabidi tulale wote humu, mimi ugenini siwezagi kulala peke yangu"


MUENDELEZO

Episode 11 SEASON 2

Moyo uka vibrate kidogo ni kama nimesikia kitu ambacho sikutegemea kukisikia ila nikahisi kama nategwa kidizaini flani, mdomo ukawa mzito sijui nimruhusu au nimjibu kitu gani, alivyoona nimekuwa mzito kuongea akaendelea kuongea

Caryn: "Nipo Serious BM, mtu yeyote anayenijua vizuri analijua hili swala hata ukimuuliza Michelle"

BM: "Sawa hamna shida, mimi naweza kulala hata hapa chini kwenye Zuria"

Caryn: "Hapana, tunalala wote kitandani, ila nakuomba ukilala assume kama vile umelala na Mama yako mzazi sipo hapa kwaajili ya kukutega maana Akili za Wanaume nazijua"

BM: "Ivi upo serious kabisa kwamba huwezi kulala chumba Cha peke yako unataka tulale wote humu tena kitanda kimoja?"

Caryn: "Kwani kuna ubaya?...naomba nenda kule room kwangu kanichukulie Handbag yangu kuna sabuni nataka nikaoge"

Nikatoka kuelekea kwa room yake kumchukulia Handbag yake huku kichwani nikijiuliza maswali ya kutosha, kwamba huyu mtu kama ni kweli hawezagi kulala mwenyewe ugenini kwanini wakati tunalipia vyumba aliruhusu nilipie vyumba viwili badala ya kimoja?

Sikupata jibu la hilo swali nikahisi tu kuna kamchezo nachezewa, nilihisi Kimasihara imejileta yani stori ndani ya story kwamba hapa hapa ninaweza kupata Cha kuchangia kwenye Uzi wa Tunda na Masihara yake na Bado nikapata Content ya kunogesha Uzi huu wa kijana wa Buguruni

Kwa muda mfupi kichwa kiliwaza mambo mengi sana hicho ni kichwa Cha juu sasa, kichwa Cha chini nacho kilikuwa kimeshapata Notification kwamba muda wowote kuanzia sasa kunaweza kukanuka so be Attention

Lakini pia nikakumbuka wadau wa hapa hapa Jamii forum kwenye huu Uzi Season 1 kule episode ya mwisho kuna wadau walishauri kwamba nifanye yote lakini nisioneshe urijali kwa Caryn

Nikaona hapa nikiendelea kuwaza nini Cha kufanya sitopata jibu Cha msingi acha niache Universe iamue, nikachukua Handbag nikarudi kule room kwangu ambako nimemuacha Caryn

Caryn akatoa Sabuni akaingia bafuni kuoga, alivyomaliza akatoka akiwa ameshavaa Night dress akanikuta nimekaa kwenye kochi naangalia Tv

Caryn: "Hee! ndio kwanza unaangalia Tv? nikajua nitakukuta upo kitandani"

BM: "Kitandani? kwanini?"

Caryn: "Mizunguko yote Ile hujachoka tu? usie lala mapema, ivi kesho ndio imebaki Document moja eeh?"

BM: "Yeah, nataka ni-fight by saa 4 Asubuhi tuwe tumeondoka"

Caryn: "Kwahiyo kesho tunatoka hapa saa ngapi?"

BM: "Mapema tu kwenye saa 1 ivi, ili saa mbili itukutie maofisini....Sasa Cha kufanya wewe itabidi ukadili na mizigo tuliyoitoa Jana ipakiwe kwenye Boti huku mimi nikiendelea kutoa ambayo imebaki Airport"

Caryn: "Guinness Book itabidi waiandike hii, Mfanyakazi anampangia Boss Majukumu"

BM: "Madam, U Boss uliuacha pale Opposite na Rotana, umevuka Maji huu ni Utawala mwingine mbaya zaidi upo kwenye himaya yangu yani chumba changu"

Mazungumzo yalibase sasa katika mzaha japo nilikuwa namaanisha nilichokiongea, Caryn akavuta shuka mimi nikaganda kwenye Tv kama lisaa lizima

Ukiniuliza kwenye Tv nikikuwa naangalia Program gani najua basi nilikuwa nazuga kuusoma mchezo,

Kikubwa moyoni nilikuwa najiambia kwamba kama vitu vitatokea niache vitokee Automatically nisi force kwasababu huwezi jua inawezekana ni mtego sasa nikijimix nikaleta habari za kupapasana nitakuwa nimelichuma janga

Niseme usiku ulipita salama kabisa, huu usiku sitokuja kuusahau maana haijawahi kutokea katika maisha yangu, Asubuhi yake tuliamka fresh ila mimi ndio nilimuamsha Caryn, nilimuamsha mimi nikiwa nishapiga Maji na yeye akajiandaa tukatoka

Tukajigawa, Caryn alienda Bandarini kuweka kila kitu sawa mimi nikashughulika na Document chap then nikaenda Airport nikautoa mzigo chap kwa haraka sababu haukuwa mzigo mkubwa

Hatimaye tukavuka maji kurudi Dar es salaam, tukafika Bandari ya Dar tuka clear kila kitu tukaupeleka mzigo Ofisini, Kazi yangu ikawa imeishia hapo, nikampatia Storekeeper Parking list ya mizigo ya BATCH hii iliyoingia siku hiyo

Tulivyofikisha mzigo Caryn alienda Ofisini kwake moja kwa moja, muda huo ilikuwa kitu kama saa nane flani mchana nikawa najishauri kwenda kumuomba ruksa, Unajua kipindi kile Cha Utawala wa Bi Mkubwa nilikuwa nikifikisha mzigo tu nilikuwa nasepa zangu, Lakini si kwa huyu Binti ila nilijua kwa leo nitakubaliwa

Kweli nilivyoenda kumuomba akakubali ila yeye alisema atabaki hadi jioni japokuwa amechoka, Mimi nikajikataa nikaingia mtaani,

Siku zikapita wiki zikasonga nakumbuka ilikuwa November tarehe za katikati nikaja kupata nyumba maeneo flani kali sana zile nyumba ni vi Apartments flani hivi vipo sita zote zipo kwenye fence moja na kila nyumba ina vyumba viwili kimoja master halafu choo Cha ku share jiko na sitting room

Ile nyumba nilivyooneshwa tu nikalipia siku hiyo hiyo likabaki swala la kuhama tu, nilikaa kama wiki moja tangu nilipie rent ndio nikahamia kwenye makazi mapya

Kwenye makazi mapya nilihamia na kila Kitu changu kasoro Tv, Muziki na Makochi nilibadilisha, vitu vikakaa Mahali pake kasoro chumba Cha pili kilikosa kitanda maana mwanzo nilikokuwa nakaa ilikuwa One Bedroom nilikohamia ni Two Bedrooms so Budget haikuwa upande wangu kuniwezesha kununua kitanda kingine kwa muda huo

Nikajipa time ila Mpango ni kwamba nikishanunua kitanda nimchukue yule kijana wa mmoja wa Buguruni nikae nae maana nikisema nikae nao wote itakuwa uongo sababu wale wengine ni madogo sana kujihudumia vitu vingi hawawezi na mimi kazi yangu ni ya kusafiri safiri

Weekend ya kwanza nikiwa makao mapya nikapanga kwenda kwa Mzee maana nikitambo sijaenda na sijawahi kukaa muda mrefu kiasi hiki, Unajua tangu Ile safari ya Zanzibar niliyoenda na Caryn sijaenda kwao, ni karibia wiki 3 au mwezi + kama sikosei

Nakumbuka ilikuwa ni jumapili ya tarehe 13 November hii siku pia nakumbuka nilipost muendelezo wa story ambayo ilikuwa Episode ya pili SEASON 2

Basi mimi huyo mdogo mdogo hadi mjengoni kwa Mzee, Wakati naenda niliwasiliana na Mzee akaniambia anatoka mara moja na Bi Mkubwa so niende tu nitawakuta wakina Michelle

Basi nikafika Getini pale nikapita bila kupingwa mlinzi ni yule yule ananijua, Mlango wa nyumba akanifungulia Michelle

Michelle: "Wow! finally, it's been a while"

BM: "Sijakuzoea hivi sister Michelle"

Michelle: "Aje?"

BM: "Si hivyo vizungu mingi, Yai muachie Caryn mjukuu wa Malkia, kwanza yupo?"

Michelle: "Yeah, Boss wako yupo Upstairs "

BM: "U Boss kazini huko, yani Basi tu sina uwezo ila huyu ndugu yako huyu"

Michelle: "Kafanya nini tena jamani, mtu na rafiki yake mshatibuana"

BM: "Urafiki gani wa kukaziana kwenye kila kitu"

Michelle: "Kakufanyaje kwani?"

Nikaanza kumuelezea Michelle....turudi nyuma kidogo ili muelewe vizuri kitu alichonikwaza

Iko hivi mimi huwa naagiza mzigo China Accessories za magari na vitu vingine vya aina mbalimbali vikifika Bongo huwa nafanya Biashara

Baadhi ya vitu vyenyewe ni kama;

Electric toothbrush

Men USB chest bag

Tire Pressure Gauge

Body Renovate

Headlight repair

Car wheel hub reflecting

Crown Car driver license bag

Car air outlet perfume

Creative 3D glass craft metal keychain

Smart Car air compressor

Car Jump starter power bank

Air conditioner vent blinds

Phone holder wall Moun


Sasa mzigo ukatua Bongo, na mzigo wangu mimi ukifika huwa haupimwi kilo, utapimwa kilo ukiwa Bado upo china ndio unataka kupandishwa ndege, ila mizigo mingine inapimwa china na ikifika ofisini inapimwa tena ku confirm Kgs

Mzigo wangu huwa haupimwi mara mbili kwasababu siulipii, yani transport mimi ni Free of charge (hizo ni enzi za Mama Sasa)

Nikachukua mzigo wangu nikapita ofisini kwake ili nimuazime gari yake niukimbize mzigo maskani chapu

BM: "Boss lady nisaidie nafunguo nikimbie nyumbani mara moja, Leo sitakuchelewesha"

(Maana kuna siku nilichukua gari nikamchelewesha kama lisaa akanisusia gari nikaenda nalo nyumbani)

Caryn: "Yani uende nyumbani halafu urudi, sijakuelewa"

BM: "Yeah, naupeleka huu mzigo mara moja then narudi faster"

Caryn: "Aah! utanichelewesha BM, Leo request tu, huo mzigo ni wa nani kwani?"

BM: "Si wa kwangu naupeleka nyumbani, maana nikisema nisubiri jioni nipande nao. Daladala itakuwa uongo halafu mambo ya ku-request mimi sifagilii"

Caryn: "Ooh, so huo mzigo ni wa kwako...umelipiwa?"

BM: "Kulipia nini tena? Mzigo nimekuambia ni wangu"

Caryn: "Sawa sijakataa ni wa kwako, ndio nauliza umelipiwa?"

BM: "Okay haujalipiwa"

Caryn: "Sasa unaondokaje na mzigo wakati haujalipiwa, ebu nione Delivery note uliyoandikiwa"

BM: "Sina Delivery note"

Akanyanyua simu akampigia Storekeeper halafu akaitwa na Accountant, wakaja mule ofisini tukawa watu wa tatu yani mimi, Accountant, Storekeeper pamoja na Caryn akiwa wa nne

Caryn: "Accountant naomba nioneshe malipo ya ule mzigo pale mlangoni iwe ni Cash au Bank transfer, na Storekeeper nioneshe Delivery note ya huo mzigo"

Kwakifupi kwasababu mzigo sijulipia wote wawili Accountant na Storekeeper walikuwa hawana hivyo walivyoambiwa waoneshe

Delivery note ni karatasi ambayo inathibitisha kwamba mzigo ulikifa kwa mwenyewe huku ikionesha kiasi alicholipia pamoja na kilo za mzigo....Ila Accountant akajibu bila kupepesa macho

Accountant: "Ule mzigo haujalipiwa so sina pesa yake"

Caryn: "Kwanini haujalipiwa?

Accountant: "Mizigo ya BM huwa hailipiwi"

Caryn: "Kwanini isilipiwe, give me one and strong single reason kwanini mizigo yake hailipiwi"

Accountant: "Right question to the wrong person, Nadhani hili swali ungemuuliza aliyekuwa incharge wa hii Kampuni au muulize mwenyewe BM"

Caryn: "Okay, tufanye hailipii, wewe kijana naomba nioneshe Delivery note ya kuonesha kwamba BM amepokea mzigo wake"

Storekeeper: "Delivery note sijamuandikia kwasababu mzigo haujafanyiwa malipo"

Caryn: "Na mwenyewe unahisi upo sahihi kabisa kufanya hivyo, akikukana je kwamba hajachukua mzig"

Caryn: "Hawa wawili watakufanya uingie kwenye kosa, kama wanapeana mzigo bila ya kulipia wewe ulitakiwa kuuandikia Delivery note kuthibitisha kwamba mzigo umefika kwa muhusika"

Caryn: "Kaendeleeni na shughuli zenu, ila we naomba uniletee kitabu cha Delivery note"

Storekeeper akaambiwa alete kitabu cha Delivery note Accountant nae akaondoka nikabaki na Caryn, alivyoletewa kile kitabu cha Delivery note akamuambia Storekeeper akaupime ule mzigo wangu kwenye mzani

Kilo zikasoma 29 (29 KGs) Caryn akapiga hesabu ya dollar 12.5 kwa kila kilo, ikaja 833,730 kama hanijui Caryn akaniambia nitoe hiyo pesa ndio mzigo utoke

Nilimuangalia Caryn kama Dakika nzima hivi simmalizi, yeye ndio kwanza yupo busy na laptop

Caryn: "Aisee kama haulipii huu mzigo sema ili urudishwe stoo"

BM: "Urudishwe tu sina pesa sasa hivi ya kulipia mzigo"

Caryn: "Okay but huu mzigo usikae zaidi ya siku Saba huko stoo, ukipitisha ziku Saba za free utachajiwa gharama za stoo vile vile"


Turudi Leo sasa huku kwa Michelle

Michelle: "Unajua sio wewe tu, hata mimi mwenyewe niliagiza nywele akanilipisha, so ndivyo alivyo ni kumzoea tu"

BM: "Sawa sijakataa kulipia lakini usinicharge kama customers wengine, mimi natakiwa kufanyiwa favor, hata wewe pia"

Michelle: "Aahwe! Caryn anifanyie favor mimi? wewe ndio wa kufanyiwa favor, wewe ndiye bwana ake mshakuwa mwili mmoja sasa"

(Mapigo ya moyo yakajilesi nimesikia nilichosikia au ni masikio yangu tu)

BM: "Tushakuwa mwili mmoja? sijakuelewa una maanisha nini? au sijakusikia vizuri?"

Michelle: "Ebu niambie ukweli, wewe na Caryn ni wapenzi? isije ikawa umenihadithia hii story yako ya kulipishwa mzigo ili tu unipange ki saikolojia"

BM: "Aah jamani hatujafikia huko, Ukiachana na urafiki, mimi na Caryn ni mtu na Boss wake"

Michelle: "Ooh! Eti eeh, mtu na Boss wake wanawezaje kulala room moja"

Unajua nilipatwa na mshangao, hii Habari nyeti kama hii nani kavujisha? nilijiuliza lakini nikajua tu huyu atakuwa tu ni Caryn, sasa kama ni yeye kwanini amefanya hivyo akiwa na nia gani haswa?

Wakati naendelea kujiuliza Mzee pamoja na Mama wakawa wamerudi, Mzee akamuulizia Caryn akaambiwa yupo Chumbani kwake na muda wote huo tunapiga Story na Michelle Caryn hakutoka nje

Mzee: "Ebu kaniitie nina mazungumzo na nyie wote watatu"

Michelle akaenda kumuita Caryn, nikabaki na Mzee, nikicheki sura ya Mzee silioni tabasamu kabisa kitu kilichonishangaza zaidi nilimuona anatoa sigara kwenye mfuko wa koti halafu akatoka nje

Unajua tangu nimjue Mzee leo ndio namuona na sigara, nilikuwa sijui kama ni mvutaji, Michelle akarudi akiwa pamoja na Caryn

Michelle: "Huyu Mzee kaenda wapi tena?"

BM: "Kumbe Mzee huwa anavutaga sigara?"

Caryn na Michelle wakaangaliana kama vile kuna kitu wanahisi"

Caryn: "Something went wrong"

Michelle: "Yeah, ukimuona Mzee anaanza kupuliza hayo madude ujue kuna kitu"

Basi kila mtu akawa anahisi jambo lake lakini hakuna ambaye alikuwa anajua ni kitu gani hasa Mzee anataka kukiongea, Mzee akarudi kutoka Smoking zone

Na hii siku ndio nilijua kwamba hii nyumba huwa na smoking zone, Caryn anadai Mwaka unaweza kupita Mzee hajaenda smoking zone

Mzee akarudi akakaa kimya kama Dakika 2 hivi huku akiwa anachezea simu, ni kama alikuwa anajibu jumbe kwenye simu yake

Mzee: "Umefanya vizuri BM kuja leo, maana nilikuwa nafikiria kukutafuta, vipi maendeleo lakini?"

BM: "Mungu mkubwa maendeleo si mabaya"

Mzee: "Vizuri kusikia hivyo"

Mzee: "Unajua BM pamoja na Binti zangu hapa nyie Bado ni vijana wadogo, na katika umri wenu huo mdogo mmepata bahati ya kuongoza Kampuni kubwa mnazofanyia kazi"

Mzee; "Ni ngumu sana kukuta Kampuni ambayo inaendeshwa na kijana inapata maendeleo mazuri kwasababu vijana wana mambo mengi sana, vichwa vyenu vinakuwa havijatulia lakini nilichukua maamuzi magumu nikawapa hiyo dhamana"

Mzee; "Unajua hakuna kitu kibaya kama kuchanganya Mapenzi na kazi...."

Caryn akakohoa, Michelle akajinyoosha kama anataka kukaa vizuri, Mimi sikutikisa hata mguu, niseme tu kwamba KUMEKUCHA


Itaendelea
Yote umeyataka mwenyewe kukaziwA. Saa hizi ungekuwa boss mwenyewe. Kila kitu kingekuwa kwenye maamuzi yako
 
BM hii story yako ni nzuri sana tafadhali rudi ushushe episodes umetupa addiction alafu unatutelekeza
 
1. How I met my wife
2. Story ya Khumbu
3. Penzi la Amida.
4. Peniela
5. Vipepeo weusi.


NB:
1. Namba 4 na 5 ni story za kutunga. 1,2 na 3 ni true stories

2. Huu ni mpangilio tu ambao nimeutoa lakini hizi stories ni hatari sana. Yaani kama umchukue MESSI kwenye Ubora wake na RONALDO kwenye ubora wake....Hapo nani zaidi ni Debate ambayo haina mwisho...Anza tu na mpangilioa niliokupa afu ukimaliza kusoma wewe ndiyo utajua ipi ndiyo kali zaidi kuliko zote maana nimeshindwa kuzi-rank

Kitu pekee nachukuhakikishia....HAUTAJUTIA time yako kama wewe ni Mtu wa kupenda stories!!!
Hiyo Penzi la Amida itupie hapa tuone mkuu
 
Kwangu mimi, with all due respect ningepanga/nazipanga hivi:

1. How I met my wife by Kigakoyo
2. Story ya Khumbu by Konda msafi
3. Penzi la Amida
4. Story ya BM

Huu ndio mpangilio wangu kwa ubora.

Ila ile Peniela kama ingekuwa ni true story....Ingekaa hapo namba moja....Story moja ina ujasusi wa kutisha.
Hii Penzi la Amida sijawahi ipitia. Itupie kichwa hapa tuone ili iwe rahisi kuifuata mkuu
 

James Jason
Asante mkuu. Tupia na hiyo How I met my Wife mkuu
 
"Najua watakusaidia kunipopoa"[emoji23].

Story imejaa events ambazo sio za lazima.

Tunaweza kuelewa stori yako hata pasipo kutuelezea namna gani unafanya shipping ya mizigo na delivering.
 
Labda nianze kwa kuwatoa wasiwasi wale wanaodhani nitasusa Uzi, Hilo haliwezi kutokea, na sikatazi mtu kutoa maoni yake hata mkinitukana mimi nitayasoma tu na uzuri ni kwamba mimi nikiwa free kama hivi huwa nasoma kila comment, hata aliyecomment nukta huwa napitia comment yake

Iko hivi, nilishindwa kutoa muendelezo jumapili Ile iliyopita kama nilivyoahidi kwasababu jumamosi yake nilisafiri na Mzee nimekuja nae Mwanza, na hadi leo hii tupo huku ila tunategemea kurudi week hii hii kama mambo yataenda sawa kama alivyopanga

Na muda mwingi nipo pamoja na Mzee, muda ambao naacha na Mzee ni ule muda wa kwenda kulala tu, sasa siwezi kuwa na Mzee tumekaa Mahali halafu mimi nipo Busy na simu naandika story, (labda mtasema kwanini nisiandike usiku muda ambao nakuwa peke angu) Huo usiku nao nakuwa nimechoka kwanza natakiwa kuwaza ratiba za siku ya kesho yake, so muda kama huo nautumia kupumzika

Yani ni vile tu hamjui na ndio maana nikiona mtu anatoa maoni yake kwa makasiriko mimi huwa hata sikasiriki wala kumshangaa, kwahiyo nikisema niwaendekeze ili kuwafurahisha naweza kujikuta naharibu sehemu nayopatia ugali kwasababu upande mmoja nita loose focus

Kuandika story (labda kichwa changu ni kizito) huwa inanichukua hata siku nzima, nimemshangaa yule jamaa aliyesema Dakika 20 tu inatosha kuandika episode 1, blaza shida sio kuandika tu kwasababu hii sio story ya kutunga, shida ni kukumbuka matukio, mf mdogo ni zile sehemu Caryn anazotema Yai,

Ivi mnajua kwamba asilimia 90 ya conversations anazofanya Caryn ni za Kingereza, na ili story ivutie inanibidi nipite mule mule lakini ninachokifanya kwa baadhi ya sehemu mimi huwa natafsiri maongezi yake kwasababu nikisema niandike Convo zake kama zilivyo kuna baadhi ya watu hawataelewa, kwanza mm mwenyewe kuna misamiati mingine anayoongea siielewi maana yake, so natumia ujanja wangu kuunganisha maneno

SO nimesema huwa inanichukua siku nzima kwasababu ya kukumbuka matukio na kuyapangilia, na siku zote nikimalizaga kuandika episode huwa naipitia kuisoma zaidi ya mara tano, sometimes naweza nisipost siku hiyo niliyomaliza kuandika nikaja kuipost siku inayofuatia, yote hiyo ni ku make sure hakuna tukio muhimu nililolisahau kwasababu ilishanitokea nimepost episode nikaja kukumbuka Kuna Mahali niliruka

Halafu katika maisha usijilinganishe na mtu mwingine, Mimi kunifananisha na watu wengine wanaoleta story humu ni kunikosea, kwasababu I'm sure tumetofautiana katika kila kitu hadi katika ku priorities mambo

Mimi mwenzenu focus yangu ipo kwenye kazi ambayo inaniweka mjini huku Jamii forum huwa nakuja kuchungulia tu nikiwa free kama hivi, na naamini pia nyie mna kazi zenu zinazowaweka mjini mkishapiga pesa huko mtaani ndio mnakuja kuchungulia humu kama BM kaleta muendelezo

Sasa kama Mimi mwenyewe hii story siipi umuhimu wa hivyo kwanini wewe ujichoshe kwa kuipa kipaumbele namna hiyo, kama ni muhimu sana basi wekeni Dau nikirudi Dar nishushe Episodes back to back kwasababu Mzee kaniambia tukirudi nipumzike siku Saba lakini siwezi kufanya hivyo mimi nina maisha gani ya kupumzika bhana, japokuwa nikipumzika mshahara wangu upo pale pale lakini nikienda job ndio napiga hela zaidi

Narudia tena fanyeni kazi hapa tunakuja kubadilishana mawazo na kuburudishana tu....au inawezekana wenzangu mnapiga pesa huku mmekaa!? kama ndio hivyo wekeni Dau mezani na mimi nipige pesa huku nimekaa kwa kuandika story. Mkifanya hivyo mm nitapumzika hiyo week moja ya Mzee aliyonambia na focus yangu yote nitaihamishia hapa......Deal???

Kwaherini bhana Mzee ni kama anakaribia kutoka lunch time hii
 
Labda nianze kwa kuwatoa wasiwasi wale wanaodhani nitasusa Uzi, Hilo haliwezi kutokea, na sikatazi mtu kutoa maoni yake hata mkinitukana mimi nitayasoma tu na uzuri ni kwamba mimi nikiwa free kama hivi huwa nasoma kila comment, hata aliyecomment nukta huwa napitia comment yake

Iko hivi, nilishindwa kutoa muendelezo jumapili Ile iliyopita kama nilivyoahidi kwasababu jumamosi yake nilisafiri na Mzee nimekuja nae Mwanza, na hadi leo hii tupo huku ila tunategemea kurudi week hii hii kama mambo yataenda sawa kama alivyopanga

Na muda mwingi nipo pamoja na Mzee, muda ambao naacha na Mzee ni ule muda wa kwenda kulala tu, sasa siwezi kuwa na Mzee tumekaa Mahali halafu mimi nipo Busy na simu naandika story, (labda mtasema kwanini nisiandike usiku muda ambao nakuwa peke angu) Huo usiku nao nakuwa nimechoka kwanza natakiwa kuwaza ratiba za siku ya kesho yake, so muda kama huo nautumia kupumzika

Yani ni vile tu hamjui na ndio maana nikiona mtu anatoa maoni yake kwa makasiriko mimi huwa hata sikasiriki wala kumshangaa, kwahiyo nikisema niwaendekeze ili kuwafurahisha naweza kujikuta naharibu sehemu nayopatia ugali kwasababu upande mmoja nita loose focus

Kuandika story (labda kichwa changu ni kizito) huwa inanichukua hata siku nzima, nimemshangaa yule jamaa aliyesema Dakika 20 tu inatosha kuandika episode 1, blaza shida sio kuandika tu kwasababu hii sio story ya kutunga, shida ni kukumbuka matukio, mf mdogo ni zile sehemu Caryn anazotema Yai,

Ivi mnajua kwamba asilimia 90 ya conversations anazofanya Caryn ni za Kingereza, na ili story ivutie inanibidi nipite mule mule lakini ninachokifanya kwa baadhi ya sehemu mimi huwa natafsiri maongezi yake kwasababu nikisema niandike Convo zake kama zilivyo kuna baadhi ya watu hawataelewa, kwanza mm mwenyewe kuna misamiati mingine anayoongea siielewi maana yake, so natumia ujanja wangu kuunganisha maneno

SO nimesema huwa inanichukua siku nzima kwasababu ya kukumbuka matukio na kuyapangilia, na siku zote nikimalizaga kuandika episode huwa naipitia kuisoma zaidi ya mara tano, sometimes naweza nisipost siku hiyo niliyomaliza kuandika nikaja kuipost siku inayofuatia, yote hiyo ni ku make sure hakuna tukio muhimu nililolisahau kwasababu ilishanitokea nimepost episode nikaja kukumbuka Kuna Mahali niliruka

Halafu katika maisha usijilinganishe na mtu mwingine, Mimi kunifananisha na watu wengine wanaoleta story humu ni kunikosea, kwasababu I'm sure tumetofautiana katika kila kitu hadi katika ku priorities mambo

Mimi mwenzenu focus yangu ipo kwenye kazi ambayo inaniweka mjini huku Jamii forum huwa nakuja kuchungulia tu nikiwa free kama hivi, na naamini pia nyie mna kazi zenu zinazowaweka mjini mkishapiga pesa huko mtaani ndio mnakuja kuchungulia humu kama BM kaleta muendelezo

Sasa kama Mimi mwenyewe hii story siipi umuhimu wa hivyo kwanini wewe ujichoshe kwa kuipa kipaumbele namna hiyo, kama ni muhimu sana basi wekeni Dau nikirudi Dar nishushe Episodes back to back kwasababu Mzee kaniambia tukirudi nipumzike siku Saba lakini siwezi kufanya hivyo mimi nina maisha gani ya kupumzika bhana, japokuwa nikipumzika mshahara wangu upo pale pale lakini nikienda job ndio napiga hela zaidi

Narudia tena fanyeni kazi hapa tunakuja kubadilishana mawazo na kuburudishana tu....au inawezekana wenzangu mnapiga pesa huku mmekaa!? kama ndio hivyo wekeni Dau mezani na mimi nipige pesa huku nimekaa kwa kuandika story. Mkifanya hivyo mm nitapumzika hiyo week moja ya Mzee aliyonambia na focus yangu yote nitaihamishia hapa......Deal???

Kwaherini bhana Mzee ni kama anakaribia kutoka lunch time hii
Umeeleweka mkuu, we piga kazi.

Hata hivyo wanalalamika ni wachache, watu wengi wanapita kimya kimya.
 
Labda nianze kwa kuwatoa wasiwasi wale wanaodhani nitasusa Uzi, Hilo haliwezi kutokea, na sikatazi mtu kutoa maoni yake hata mkinitukana mimi nitayasoma tu na uzuri ni kwamba mimi nikiwa free kama hivi huwa nasoma kila comment, hata aliyecomment nukta huwa napitia comment yake

Iko hivi, nilishindwa kutoa muendelezo jumapili Ile iliyopita kama nilivyoahidi kwasababu jumamosi yake nilisafiri na Mzee nimekuja nae Mwanza, na hadi leo hii tupo huku ila tunategemea kurudi week hii hii kama mambo yataenda sawa kama alivyopanga

Na muda mwingi nipo pamoja na Mzee, muda ambao naacha na Mzee ni ule muda wa kwenda kulala tu, sasa siwezi kuwa na Mzee tumekaa Mahali halafu mimi nipo Busy na simu naandika story, (labda mtasema kwanini nisiandike usiku muda ambao nakuwa peke angu) Huo usiku nao nakuwa nimechoka kwanza natakiwa kuwaza ratiba za siku ya kesho yake, so muda kama huo nautumia kupumzika

Yani ni vile tu hamjui na ndio maana nikiona mtu anatoa maoni yake kwa makasiriko mimi huwa hata sikasiriki wala kumshangaa, kwahiyo nikisema niwaendekeze ili kuwafurahisha naweza kujikuta naharibu sehemu nayopatia ugali kwasababu upande mmoja nita loose focus

Kuandika story (labda kichwa changu ni kizito) huwa inanichukua hata siku nzima, nimemshangaa yule jamaa aliyesema Dakika 20 tu inatosha kuandika episode 1, blaza shida sio kuandika tu kwasababu hii sio story ya kutunga, shida ni kukumbuka matukio, mf mdogo ni zile sehemu Caryn anazotema Yai,

Ivi mnajua kwamba asilimia 90 ya conversations anazofanya Caryn ni za Kingereza, na ili story ivutie inanibidi nipite mule mule lakini ninachokifanya kwa baadhi ya sehemu mimi huwa natafsiri maongezi yake kwasababu nikisema niandike Convo zake kama zilivyo kuna baadhi ya watu hawataelewa, kwanza mm mwenyewe kuna misamiati mingine anayoongea siielewi maana yake, so natumia ujanja wangu kuunganisha maneno

SO nimesema huwa inanichukua siku nzima kwasababu ya kukumbuka matukio na kuyapangilia, na siku zote nikimalizaga kuandika episode huwa naipitia kuisoma zaidi ya mara tano, sometimes naweza nisipost siku hiyo niliyomaliza kuandika nikaja kuipost siku inayofuatia, yote hiyo ni ku make sure hakuna tukio muhimu nililolisahau kwasababu ilishanitokea nimepost episode nikaja kukumbuka Kuna Mahali niliruka

Halafu katika maisha usijilinganishe na mtu mwingine, Mimi kunifananisha na watu wengine wanaoleta story humu ni kunikosea, kwasababu I'm sure tumetofautiana katika kila kitu hadi katika ku priorities mambo

Mimi mwenzenu focus yangu ipo kwenye kazi ambayo inaniweka mjini huku Jamii forum huwa nakuja kuchungulia tu nikiwa free kama hivi, na naamini pia nyie mna kazi zenu zinazowaweka mjini mkishapiga pesa huko mtaani ndio mnakuja kuchungulia humu kama BM kaleta muendelezo

Sasa kama Mimi mwenyewe hii story siipi umuhimu wa hivyo kwanini wewe ujichoshe kwa kuipa kipaumbele namna hiyo, kama ni muhimu sana basi wekeni Dau nikirudi Dar nishushe Episodes back to back kwasababu Mzee kaniambia tukirudi nipumzike siku Saba lakini siwezi kufanya hivyo mimi nina maisha gani ya kupumzika bhana, japokuwa nikipumzika mshahara wangu upo pale pale lakini nikienda job ndio napiga hela zaidi

Narudia tena fanyeni kazi hapa tunakuja kubadilishana mawazo na kuburudishana tu....au inawezekana wenzangu mnapiga pesa huku mmekaa!? kama ndio hivyo wekeni Dau mezani na mimi nipige pesa huku nimekaa kwa kuandika story. Mkifanya hivyo mm nitapumzika hiyo week moja ya Mzee aliyonambia na focus yangu yote nitaihamishia hapa......Deal???

Kwaherini bhana Mzee ni kama anakaribia kutoka lunch time hii

Kazi kwanza burudani baada ya kz
 
Back
Top Bottom