Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Hatma ya maisha yangu ipo mikononi mwa kijana wa Buguruni

Nilijua hi story kwenye huu uzi itaishia season one kumbe imeendelea hata hatushtuani
 
Sijakuelewa, una maanisha nn?
Mm ni mgen humu. Nimekuwa nikisoma story hii.

Inafundisha. Via BM hustling zako
Inaburudisha via watoto wa mzee.

Nili court maneno ya mzee haya..
Screenshot_20230309-222413.jpg

Tatizo unakuwa busy inavyotakiwanila unasahau umetuonjesha kiongoz.

Naelewa sana

Moja eneo ambalo nimelochukia ni kula au kujali familiar ya njem i remember that line.

MB muda mbaya.
BM bahati Mbaya.
MB bando bei mbaya
 
Mm ni mgen humu. Nimekuwa nikisoma story hii.

Inafundisha. Via BM hustling zako
Inaburudisha via watoto wa mzee.

Nili court maneno ya mzee haya..
View attachment 2553534
Tatizo unakuwa busy inavyotakiwanila unasahau umetuonjesha kiongoz.

Naelewa sana

Moja eneo ambalo nimelochukia ni kula au kujali familiar ya njem i remember that line.

MB muda mbaya.
BM bahati Mbaya.
MB bando bei mbaya
[emoji1545][emoji1545][emoji1545]

Muendelezo mchana huu, haifiki hata jioni naifanyia review then nipost
 
Ilipoishia

Baada ya Accountant kumaliza kazi yake Caryn aliniita na kunipa maagizo flani

Caryn: "Una mawasiliano ya Mr Michelle?"

BM: "Hapana"

Caryn: "Basi nitamuambia Secretary ampigie ili aje kuanza kazi tarehe 1 December"

Nikashusha pumzi kwanza, nikajua hapa sasa nimemalizana na Michelle ila kuna kitu nikamuuliza Caryn maana nilijua àmempotezea jamaa

BM: "Pamoja na kwamba nilikuwa nakushauri huyu jamaa umpe kazi Lakini sikuwahi kuwaza kama utakubali"

Càryn: "Wewe tulia mimi najua nini nafanya, kama ana akili timamu ataikataa hii kazi"

BM: "Kwanini akatae sasa?"

Caryn: "Wewe alikunyima kazi kwasababu tu aliona picha yangu, hiyo ina maana ya kwamba Mimi na yeye hatuko sawa, kama mimi ndio ningekuwa ni yeye ningejiweka katika taadhari sana kwa mtu ambaye anaonesha kunijari au kunipenda na wakati najua hatukuwa sawa, Mimi huwa naamini kuwa mtu mbaya akipanga kufanya ubaya hutanguliza wema kwanza"


Muendelezo

(Episode 17, SEASON 2)

Tarehe 1, December, siku ya Alhamisi Opportunist aliitikia wito jamaa alifika ofisini mapema tu, Wakati nipo ofisini kwa Caryn secretary alikuja kumpa taarifa kwamba Opportunist tayari ameshafika.

Sasa mimi nikataka niondoke kusudi nimpishe Caryn na mgeni wake ila Caryn akanizuia

Caryn: "Unaenda wapi wewe kaa hapo, huyu naongea nae na wewe ukiwepo"

BM: "Sio heshima bhana Caryn, vitu vingine vinahitaji privacy"

Caryn: "Nina maana yangu kutaka wewe ubaki hapa"

Ikabidi nifuatishe order, halafu kitu kingine nilichokisoma kwa Caryn ni kwamba nikionesha kama nipo upande wa bwana ake Michelle ana kwazika sana, basi jamaa akaitwa akatinga ofisini na confidence zote akatusalimia halafu jamaa akakaa kwenye kiti

Caryn: "I didn't ask you to sit"

Opportunist ikabidi asimame, na muda huo Caryn amechange kabisa sio yule niliyekuwa naongea nae Dakika 2 zilizopita

Caryn: "Anyways, you may sit"

Nilivyomcheki Opportunist usoni nikamsoma kama kamaindi vile, kwasababu alikuwa ameshakaa kwenye kiti halafu Caryn akamuamsha eti kisa hajamruhusu kukaa na jamaa hicho kitendo kimemuudhi facial expression yake tu ilidhihirisha, Sasa kama ndio atakuwa mtu wa kumaindi vitu vidogo kama hivi sidhani kama atatoboa

Wakaanza maongezi yao mimi nipo pembeni nawasikiliza

Caryn: "Mr ****, I believe you dropped your CV with us few weeks ago, well the vacant job is not what you applied for but it's something based on the fact that you have an interesting"

Caryn: "Here is your work description work hours schedules and payments so if you agree kindly sign and resume immediately"

Jamaa aka sign, baada ya Caryn kumalizana na Jamaa Secretary akaambiwa awape taarifa staff wote kwamba baada ya lunch time kuna kikao

Basi, baada ya lunch time kweli kikao kikaanza na lengo la kikao ni watu kupangiwa majukumu yao upya hasa kwa Opportunist pamoja na Utambulisho wake kama new staff

Kwa kifupi jamaa alipewa kazi ya ku deliver mizigo kwa wateja hapa Dar kwa wateja ambao wanataka huduma hiyo na kupakia mizigo kwenye mabasi kwa wale wateja wa mikoani

Kwa haraka haraka kazi aliyopewa jamaa unaweza kuona ni ya kiseng* lakini ni moja kati ya Kazi ambayo mtu akiifanya basi atakutana na tip za kutosha, nasema hivyo kwasababu Mimi ndio nilikoanzia huko na nilikuwa napata vi tip sana japo si kwa wateja wote kama mnavyojua watu hawafanani,

Ila pia ina changamoto yake hii kazi, hasa kwenye hii mizigo inayoenda mikoani, ukijikoroga ukapoteza mzigo wa watu ujue Ofisi ndio inalipa na Ofisi hailipi hivi hivi tu itakukata kwenye mshahara wako.

Sasa Caryn alivyomaliza kumtambulisha mfanyakazi mpya na kumpangia majukumu, akaanza kumsomea kila mtu mashtaka yake coz pale ofisini kuna kisanduku Cha maoni au complaints kwa wafanyakazi

Caryn: "I have some grievances here in my desk....

Caryn: "Accountant you have treated as lot of your colleague here with disrespect, I get complaints all the time but I overlook them because of friendship between your Mom and Dad, I'm giving you a second chance to redeem yourself, I want to see if you can change for the better or if you remain this person that you are"

Accountant: "So correcting people's mistakes at work is that act interpreted as Disrespect?

Caryn: "But you don't correct people by being rude to them you speak to them nicely and with love no matter who they are"

Caryn: "Nadhani tumeelewana Accountant, na BM naomba kama hauko Zanzibar nikuone Ofisi, Habari za kupotea na kuonekana siku za safari hiyo tabia ife tafadhali yani unafanya kazi kama vile we ni Agent na wakati umeajiriwa"

Hatimaye na mimi sikuachwa salama nikachanwa mbele ya kadamnasi

Caryn: "Last but not least, naomba tufanyeni kazi kwa bidii, Watanzania tuna utamaduni wakupoteza sana muda, tunajifanya na kujionesha tunapenda sana kufanya kazi lakini kiuhalisia hatufanyi kazi kama tunavyoonekana. Mimi sitalipa mtu kwa kuonekana anafanya kazi, nitakulipa kwa matokeo ya Kazi uliyoifanya"

Tukafunga kikao, masaa yakaenda hatimaye na muda wa kufunga Ofisi ukafika tukafunga, Usiku wa siku hiyo Wakati nipo kwangu nataka kulala Mzee akanipigia simu akanambia kwamba Asubuhi ya jumamosi ya kesho kutwa nijitahidi tuonane,

Ilivyofika Jumamosi mapema tu nilikuwa nyumbani kwa Mzee, kumbuka jumamosi ni siku ya kazi pia japo ni nusu siku lakini sikwenda ofisini nimekuja kwa Mzee moja kwa moja (Kosa hilo, a very Big one)

Nilivyofika kwa Mzee nikamkuta nikamsubiria sitting room alivyomaliza kujitayarisha tukaanza safari wakati tunaondoka nyumbani sikujua tunaenda wapi hadi tulipofika tulipokuwa tunaenda, sema hapa naomba nisiingie deep sana Incase Uzi huu ukaja kusomwa na family member

Tukatoka kule tukarudi mjini tukaenda hoteli flani ipo maeneo ya Mikocheni, hii hotel ndio kwa mara ya kwanza naenda na Mzee lakini nilishaenda na Caryn mara kadhaa

Tukatafuta Mahali tukaketi akaja muhudumu akatusikiliza Mzee akanambia niagize chochote nikaagiza then yule muhudumu akaambiwa na Mzee amuite Manager

Manager alivyokuja ndio nikajua sasa kuhusu Ile hotel, kumbe Ile hotel ni ya Mzee bhana na tunakujaga na Caryn hata hakuwahi kuniambia, Manager alivyoondoka ikabidi nimuulize Mzee

BM: "Mzee kumbe hapa ni kwako?"

Mzee: "Ndio lakini nimepanunua juzi juzi tu hapa, kama miezi 7 iliyopita"

BM: "Ooh! ndio maana hata wahudumu hawakujui sababu naona wanakuhudumia kama mteja wa kawaida tu"

Mzee: "Na Mimi ndio nataka iwe hivyo, ukiwa unamiliki sehemu kama hii Kuna faida kubwa kama wafanyakazi watakuwa hawakujui sababu ni rahisi kuona madudu yanayofanyika"

BM: "Sasa Mzee huyu manager hawawezi kuwaambia wafanyakazi ili mradi wawe makini pindi wewe unapokuwepo hapa"

Mzee: "Kwenye mkataba wake kuna kipengele kinambana kufanya hivyo"

Mzee: "Hata wewe Mungu akikubaliki na Mali za kutosha usipende kuwa front kila sehemu hata kama Mali zako ndio zitakupa umaarufu"

Basi tulivyomaliza kula tukaondoka tukaenda masaki kule kwenye Appointments zake ambapo nilishawahi kwenda na Caryn pia, Mzee akakagua kagua pale then akampigia simu Caryn nikamsikia anamuomba namba za msimamizi wa zile Apartments

Mzee: "Nina Mwaka sijaja huku, naona Binti aliamua kubadilisha rangi za kuta"

BM: "Yeah, management mpya iliyowekwa inajaribu kufanya vitu tofauti"

Mzee: "Na sijui mtu mwenyewe anafanyanana aje, asije akawa adui yangu ndio anasimamia Mali zangu"

BM: "Mzee Kwani wewe una maadui?"

Kabla ya kunijibu Mzee akacheka kwanza

Mzee: "Unajua kwenye ridhiki adui hakosekani, tena hasa ukiwa na ukwasi wa kutosha sio binadamu wote watakuangalia kwa jicho zuri, kumiliki utajiri inakubidi uwe na roho ngumu sana, sikutishi lakini ndio uhalisia kama roho yako ni nyepesi na huruma huruma nyingi hutoboi"

Saa hiyo tunashuka ngazi huku tunaongea, tumetoka rooftop kuangalia matank ya Maji

BM: "Mzee mbona wewe una huruma bhana na umetoboa"

Mzee: "Kwa bahati mbaya umenijua uzeeni, Mimi Wakati najitafuta hii huruma unayoniona nayo sikuwa nayo kabisa"

Mzee: "Hata spirit ya kutafuta pesa sio kama Ile niliyokuwa nayo zamani, nimekuja kupunguza speed baada ya kujua kwamba tunapambania vitu tusivyozikwa navyo na tunazikwa na vitu tusivyo vipambania, lakini hii kauli isikufanye ubweteke na maisha ikupe tu angalizo katika njia unazochagua katika kutafuta hayo maisha"


Sasa wakati tunaendelea kuzunguka zunguka kwenye compound ya zile apartments manager akatokea nikawaacha na Mzee wanaongea, mm nikatoka nje ya fence kabisa tulikopaki Gari (Jeep Wrangler) Mzee alivyomalizana kule ndani akatoka tukasepa tukarudi nyumbani

Kikawaida kama ukitoka na Mzee mkianzia safari nyumbani kwake mkimaliza Mizunguko yenu huwa anataka mrudi wote nyumbani halafu ndio uondoke, hawezi mkatoka wote nyumbani halafu akakuachia juu kwa juu, hapa ndio huwa simuelewagi

Sasa wakati tumefunguliwa Geti ndani Parking tukakuta gari ya Michelle Audi, Mzee akaniambia

Mzee: "Ivi ulianza kile nilichokuagiza?"

BM: "Yeah" (ilibidi nimdanganye)

Mzee: "Jitahidi, watoto wa kike hawa sio wa kuwaamini sana hasa huyu Michelle"

BM: "Sawa Mzee nimekuelewa"

Tukaingia ndani, Tukakuta sitting room ipo tupu hakuna mtu, Mzee akamuita Michelle alikuwa chumbani kwake then akamuagiza Michelle aniletee kinywaji halafu yeye akaenda chumbani kwake

Nikamwambia Michelle aniletee juice, akaleta juice

Michelle: "Usipende kunywa kunywa majuice haya sio mazuri hasa kwa mwanaume yana masukari mengi"

BM: "Sasa kama sio nzuri mbona mnaendelea kuzitengeneza?"

Michelle: "Huu ni ushauri tu kama uliopo kwenye pakti la sigara, shauri yako utashindwa kunanii"

BM: "Kufanyaje?"

Michelle: "Umenielewa....umetoka wapi na Mzee?"

BM: "Town tu misele misele ya hapa na pale"

Michelle: "Ooh, naona mmempatia mtu wangu kazi ila katika nafasi zote ndio mmeamua kumpa Ile?"

BM: "Ile si kazi mbaya kama unavyofikiria, Iko na pesa kama akijua ku deal na wateja, huko Mimi ndipo nilipoanzia"

Michelle: "So kwasababu wewe ulianzia huko chini basi unataka watu wote waanzie ulipoanzia wewe sio"

BM: "Hapana sina maana hiyo, ila kama nafasi nyingine ingekuwepo angepatiwa ni vile tu hakukuwa na nafasi na Ile ndio iliyokuwepo"

Wakati tunaendelea maongezi Caryn akafika, mida hiyo ni ya jioni, amefika hata hajasalimia

Caryn: "BM Kwanini hujaja kazini Leo?"

BM: "Aah nilikuwa na Mzee leo ndio tumerudi tu muda sio mrefu"

Caryn: "You can't be serious, nikajua unaumwa kumbe ulikuwa katika mishe zako!"

BM: "Nimekuambia nilikuwa na Mzee"

Caryn: "Hata kama ulikuwa na Rais, ulinipa taarifa?"

BM: "Sasa hata hivyo kulikuwa na ulazima gani wa Mimi kuja? maana najua hakuna kazi inayohitaji uwepo wangu pale"

Caryn: "Unajua wewe nilishakusoma kitambo sana, linapokuja swala la kazi unachukulia poa sana, hata juzi kwenye kikao nilikusema makusudi mbele ya watu kuhusiana na hii issue nikijua utachange.....sasa usije kabisa ofisini mpaka nitakapo kupigia simu"

Halafu huyoo akaelekea chumbani kwake

Michelle: "Ashavurugwa huyo huko alipotoka"

BM: "Aah atajua mwenyewe bhana, anamtisha nani sasa"

Michelle: "Mwenzako alichokiongea kamaanisha, we kwani bado hujamjua Caryn?

BM: "Aah uzuri nilikuwa na Mzee na Mzee mwenyewe anajua"

Michelle: "Sasa ukitaka usiharibu zaidi kwenye hii issue usiende kushtaki kwa Mzee kwasababu Dad hawezi kuingilia maamuzi ya Caryn namjua yule Mzee, na Caryn akijua tu umemshtaki atakukazia zaidi ili ku prove kwamba ana power"

BM: "Dah! nishakosa mood ya kuendelea kukaa hapa, kama vipi tutoke basi unisogeze sogeze na gari yako"

Michelle: "BM nimechoka, unajua nilianza kulala wewe na Mzee ndio mmeniamsha"

BM: "Twende bhana hata ukashangae shangae mlimani City"

Michelle: "Sasa mlimani City nikashangae Nini ambacho sijawahi kukiona? wewe sema tu unataka kwenda mlimani"

Akakubali akaenda kujiandaa Sasa alivyenda kumuaga Mzee nadhani Caryn alimsikia, Michelle akaja ameongozana na Caryn

Caryn: "Count me in guys kwenye hiyo Outing yenu, sijisikii kula chakula Cha nyumbani leo"

Michelle: "But sisi hatuendi kula"

Caryn: "Mnaenda Kufanya nini?"

Michelle: "Original request BM alitaka nimsindikize, kwenda mlimani ni idea tu ya kwenda ku buy buy time"

Caryn: "Ni sawa, wewe msindikize unayemsindikiza na wakati mki buy-time mm nakula"

Michelle: "Okay, let's go"

Tutatoka na (Audi) gari ya Michelle na Dereva alikuwa ni yeye mwenyewe Mimi nimekaa kushoto kwake mbele Caryn kakaa Back left yani nyuma yangu

Tukafika mlimani City tukaenda hadi kuku kuku wote tukajikuta tumeagiza chakula

Caryn: "Si mlisema hamli nyie?"

Michelle: "So ulitaka tukuangalie ukila, tumeamua tu kukusupport isingeleta picha nzuri kwenye mezani ya watatu mtu mmoja tu ndio anakula....au unasemaje BM"

BM: "Yeah, true"

Michelle: "BM"

BM: "Yes"

Michelle: "I feel like you want to say something but you're scared"

Hii sasa michoro, Michelle kaamua kunichoresha

BM: "Something to say? to who?"

Michelle: "Maybe to Caryn

Simu yangu ikaita katikati ya maongezi kucheki alikuwa ni Annie nikaenda kuongea pembeni kule parking kabisa, baada ya Dakika kama 4 nikarudi nikakuta mhudumu kaanza kuleta Cutlery kiashiria Cha kwamba msosi unakaribia kuja

Michelle: "So Madam, you hired my man yes I appreciate for that, but you put him into a cheaper position! really!?"

Caryn: "Unatakiwa Appreciate pia kwa hiyo kwa nafasi ambayo ameipata kwasababu nimefanya kama favor tu, nilikuwa na uwezo wa kumuweka mtu mwingine bila kuulizwa na yeyote"

Michelle: "Sawa, lakini kumbuka hata hizo favors unazoziongelea hata mimi nimekufanyia sana tu mdogo angu"

Caryn: "Niache nile tafadhali"

Msosi ukaja tukaufinya, tulivyomaliza kula tukaachana pale pale mlimani City, hiyo siku ilikuwa Jumamosi Jumatatu yake nikaingia job nilichelewa kama Dakika 20 ivi nikapita ofisini kwa Caryn kusaini ile kwanza hakutegemea

Caryn: "We vipi! kwani juzi hukunielewa?"

BM: "Nilikuelewa, Ina maana hadi Leo umemaindi?"

Caryn: "Narudia tena usije kazini hadi nitakapokupigia simu, kama mimi na wewe tunaheshimiana utanisikiliza ninachokiongea"

Nikaona mambo yasiwe mengi nikaondoka, ila nikawa nimemaindi yani kumbe Caryn ndio ana mambo ya kiduanzi hivi!

Nikarudi nyumbani, kesho yake Jumanne nikaenda kule manzese kwa kijana wa Buguruni anapojifunzia ufundi furniture nilikuwa nimewapa kazi ya kunitengenezea kitanda lakini nilitaka Kijana wa Buguruni ndio akitengeneze mwenyewe chini ya uangalizi wa mwalimu wake ili kumpima kama amekwiva?

Basi nilivyofika manzese nikakuta Bed ndio inapigwa polish, na kufanyiwa finishing hiyo siku niliimalizia pale manzese jioni mida ya saa 11 jioni nikarudi zangu home, kwa kifupi kijana amekwiva maana kitanda amekitoa fresh.

Sasa katika siku ambayo nilikuwa nategemea simu ya Caryn ni leo lakini simu haijaita kwasababu ndio siku ambayo huwa naenda Zanzibar, Yani nisipoenda Jumatatu basi nitaenda Jumanne halafu usiku wa Jumanne nageuza na mizigo Asubuhi ya Jumatano inanikutia Bandarini

Kwahiyo kama hadi sasa hivi simu haijaita hiyo ina maanisha kwamba kuna mtu mwingine ndio ameenda kufuata mizigo sio! atakuwa ni nani? hapo ndio sijui

Jumatano Asubuhi nikiwa nawaza niende wapi, Nikapata wazo la kumcheki Michelle, nikampigia simu akanambia yupo job nikamuibukia,

Uzuri wa Michelle ha complicate mambo office hours unaweza ukapiga nae story fresh tu lakini sio kwa Caryn

BM: "Nikajua utakuwa umeenda site"

Michelle: "Hapana leo sio siku ya kwenda site, vipi ww hujaenda kazini kwani?"

BM: "Mdogo wako si ndio kashaamua, me nikajua Ile siku anazingua tu kumbe alikuwa serious"

Michelle: "Ooh dah nilisahau, lakini nilikuambia kwamba Mwenzako yupo serious...lakini nyie watu huwa mnanishangaza sana"

BM: "Kwanini?"

Michelle: "Anyways acha nisifikirie vitu ambavyo pengine hata havipo, ila ngoja me nitaongea nae japokuwa najua kwasasa ww unammudu Caryn ila Hujataka tu kuongea nae vizuri"

BM: "Achana nae bhana, vipi Shemeji yangu hajambo?"

Michelle: "Hajambo, mzima kabisa wa afya"

BM: "Ooh nice, ila muambie asichelewe kuleta Mahali kwasababu watu wanaokutaka ni wengi"

Michelle: "Nilienae ananifaa kwakweli, labda aamue kuniacha yeye"

BM: "Ivi mshkaji anakupenda kama wewe unavyompenda?

Michelle: "BM Ebu niache, naona umeishiwa na story"

Nilivyoona hayupo interested kuendelea kumuongelea jamaa wake nikachange topic tukaendelea na story baada ya muda kidogo akapokea simu kwamba kuna mgeni anamsubiri ikabidi nimuache maana mgeni mwenyewe alikuwa ni wa kiofisi zaidi

Ikafika weekend siku ya Jumapili nimemaliza kufanya usafi

(Kuna mtu aliniambia eti jumapili sio siku ya kufanya usafi, nitafute Hela)

Sasa nimetulia zangu sina hili Wala lile simu ikaita kucheki ni Accountant anapiga

Accountant: [emoji338]"Vip Boss unaumwa na hausemi!"

BM: "We nani kwakuambia kama mimi naumwa"

Accountant: "Si kaniambia Boss wako sijui Demu wako, mnapendana wenyewe hadi mkiumwa mafua tu mnapeana off"

BM: "Sijaelewa madhumuni ya hii simu yako, umenipigia kunijulia hali au kuninanga?"

Accountant: "A na B yote majibu, halafu nikuulize huyu mtu wenu mmemtoa wapi?"

BM: "Mtu gani?"

Accountant: "Si huyu Mfanyakazi wenu mpya"

BM: "Nani? Opportunist au?" (Nilimtaja kwa Jina lake halisi)

Accountant: "Mm sitaki kujua anaitwa nani, ila mwambie aache mazoea na mimi"

BM: "Haya kafanyaje tena?"

Accountant: "We nishakuambia muambie aache mazoea na mimi"[emoji3513]

Moja kwa moja nikawa nishaelewa kwamba Opportunist atakuwa alijaribu kuchapa verse na kwa bahati mbaya verse zikadunda kwa Accountant,

Ila sikushangaa sana ni kawaida yetu sisi wanaume ila jambo lililonishangaza ni hili la Caryn kuwaambia watu kuwa naumwa akati kanipiga stop kwenda kazini

Nikampigia Michelle kumpeleleza maana aliniambia ataongea na ndugu yake kuhusu mimi

BM: [emoji338]"Mambo"

Michelle: "Poa, nambie BM"

BM: "Vip uliongea na hako ka Boss lady?"

Michelle: "Yeah, niliongea nae lakini kaniambia mambo yenu nisiyaingilie mtamalizana wenyewe"

BM: "Ooh"

Michelle: "Kwani wewe hukuongea nae tena?"

BM: "Sikumtafuta mimi tangu nilipotoka ofisini Ile siku"

Michelle: "Tatizo wewe sijui unamuogopa, au unavimba? unamvimbia Boss? shauri yako, mtafute ametoka hapa muda sio mrefu"

BM: "Sawa"[emoji3513]

Nilivyokata simu ya Michelle nikampandia hewani Caryn

BM: [emoji338]"Hello...Mambo"

Caryn: "Poa"

BM: "Vipi uko wapi"

Caryn: "Niko town, sema una shida gani"

BM: "Nimekumiss, nilikuwa nataka nikuone"

Caryn: "Niko busy kidgo kwasasa nitakutafuta mwenyewe"[emoji3513]

Imefika majira kama ya saa Tisa alasiri kweli Caryn akanipigia simu akanambia anakuja mjengoni Uzuri nilikuwa mtaani tu maeneo karibu na nyumbani,

Nikarudi home fasta nikafanya usafi kwa mara nyingine tena, nikabadilisha hadi mapazia yale aliyoyasema kwamba ni ya kichaga

Nika make sure kila kitu kipo sawa, after one hour ivi nikamsikia mtu anabisha hodi, kufungua mlango kumbe ni Caryn

BM: "Kwani haukuja na Gari?"

Caryn: "Nimekuja nalo nimelipaki nje hapo"

BM: "Kwanini sasa?"

Caryn: "Acha tu likae huko si kuna usalama pia au?"

BM: "Yeah, usalama upo"

Caryn: "Nisaidie na Maji please"

Nikaenda jikoni kumchukulia Maji nikamletea alivyomaliza kunywa kama kawaida yake akaanza na swali

Caryn: "BM Ivi una side hustle nyingine unafanya au unategemea tu kazi moja kukuingizia pesa"

BM: "Kwasasa nina kazi moja tu, vipi kwani?"

Caryn: "Hiyo kazi moja ni ipi sasa?"

BM: "Si ya pale ofisini"

Caryn: "Sasa mbona huichukulii serious, kama ndio kazi pekee unayoitegemea?"

BM: "Sijajua Sasa ww kwa upande wako ili mtu awe serious na kazi unataka aweje"

Caryn: "Halafu ivi unajua kama una dharau? sijui kwasababu tumezoeana sana, I don't know ila unadharau aise"

BM: "Dah! labda ni kweli siwezi jua"

Caryn: "Ndio ujue sasa, labda nikuulize kama wewe ndio ungekuwa katika nafasi yangu halafu mtu anajiamulia kutokuja kazi na hatoi hata taarifa, wewe kama wewe ungechukua uamuzi gani juu ya huyo mtu"

BM: "Kiukweli sijajua ningechukua hatua gani kwa kitu ambacho ni Assumption hadi hiyo circumstance ini face ndio ningejua nini Cha kufanya"

Caryn: "Ooh nice, jibu zuri sana...Mimi maamuzi niliyoyachukua nilikusimamisha kazi, unajua ni kwanini nilikusimamisha kazi?"

BM: "Hapana, sifahamu"

Caryn: "Pengine ulikuwa na mentality ya kwamba bila ya wewe mambo hayataenda pale ofisini, so niliamua kukusimamisha makusudi ili kukuonesha kwamba bila ya uwepo wako mambo yanaweza kwenda tena vizuri tu"

Caryn: "We unadhani kwanini nilitaka kwenda na wewe Zanzibar? Kama ulikuwa hujui mimi nilienda kule kwa ajili ya kutengeneza Back up, kila ninachokifanya mimi lazima niwe na Backup plan"

Dah! sikuwaza hili Jambo, Aisee kumbe Ile trip ya Zenji niliyoenda na Caryn kumbe mwenzangu alienda kutengeneza network yake, so kwenye Ile trip alijuana na maagent na maafisa wa TRA, hadi ZBS kote huko mawasiliano anayo, Yani Dah niliishiwa nguvu nyie nikakosa hata cha kuongea

Caryn: "Halafu mm najua kama unaiibia Kampuni ila nilijifanya mjinga nikatulia, kona zote unazopita mimi nazijua, kama utabisha mimi ushahidi ninao"


Itaendelea
 
Back
Top Bottom