Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Maalim Seif ni Mtanzania, tena ni Mtanzania mzalendo kwelikweli!
Ni miongoni mwa watu ambao mwalimu Nyerere aliwaheshimu sana kutokana na misimamo thabiti na kipawa chake kikubwa sana cha akili.
Lakini ukiacha kuipenda Tanzania, Maalim anaipenda sana Zanzibar, nchi aliyozaliwa. Wazanzibar wanamheshimu pia.
Sisi huku Tanganyika tuliamua kuendelea kumuita Nyerere "mwalimu", Siyo kwamba hakuna viongozi wengine walikuwa walimu huko zamani, bali ni kutokana na ukweli kuwa Nyerere alikuwa mtawala lakini pia aliendelea kuwa mwalimu wa falsafa za maendeleo na haki.
Na huko Zanzibar mzee wao wampendaye wakaamua kumuita "Maalim", hii ni lahaja tu za Kiswahili lakini mwalimu na maalim ni maneno yenye maana ileile kumaanisha "yule afundishaye"
Maalim Seif amekuwa mvumilivu mno katika masuala ya siasa, kafanyiwa faulo na madhambi chungu nzima katika njia yake ya kisiasa, lakini hajawahi kuhamasisha vurugu, uvunjifu wa amani, umwagaji damu au kuumiza Wazanzibar kwa sababu za kisiasa. Na kitendo hiki cha kuweka mbele maslahi ya wazanzibar ndicho kilichompa heshima sana mbele ya wazanzibar wenyewe.
Tanzania ya Leo ina bahati moja. Ina mtu ambaye ni kipenzi cha Wazanzibar, na pia ni muumini wa Muungano. Natoa rai kwa serikali ya Nchi hii, MTUMIENI HUYU MZEE VIZURI KULINDA MUUNGANO KABLA HAJATANGULIA MBELE YA HAKI!
Hatari ninayoiona ya kudhani kuwa Kuwalazimishia Wazanzibar kiongozi ndiyo njia sahihi ya kulinda muungano, hii ni njia yenye upeo mfupi sana, itafika mahali Wazanzibar watapata Kiongozi mwingine ambaye ni Radical, na huyu anaweza kuwamobilize Wazanzibar waukatae muungano.
Ikifikia hapo, ama itabidi mtumie nguvu kuulinda, mtapelekea umwagaji damu wa kutisha na Dunia itawagomea na itawalazimisha muwaache Wazanzibar wenyewe na nchi yao huku wahusika wa vitendo hivyo wakichukuliwa hatua na mahakama za kimataifa Au itabidi muwaachie tu nchi yao wajitawale!
Sasa sisi tukitumia busara hatupaswi kufika huko, Tumsaidie Maalim na Wazanzibar kwa kuwapa haki yao ya uchaguzi bila kuleta mambo ya Jecha, Kisha maalim atasaidia kuutetea muungano na wazanzibar watamsikiliza.
Uzuri wa mtu kama Maalim ni kuwa hawa ni aina ya viongozi ambao hata wakiwa wameshatangulia mbele ya haki basi vizazi na vizazi huendelea kuwafanya rejea ya utatuzi wa. mambo mbalimbali maana wanakuwa wameacha alama.
Kama Maalimu akiwa raisi wa Zanzibar na akafanikiwa kuweka precedence ya kuuheshimu muungano, basi amini usiamini huu Muungano utakuwa legitimized zaidi vizazi na vizazi vijavyo. Lakini mkimnyima maalim ushindi wake, kisha wazanzibar wakaweka dukuduku moyoni, basi dukuduku hilo litaendelea vizazi na vizazi vya wazanzibar na kuuona muungano kama project ya Ukoloni mamboleo na hivyo kuudharau, kutoupenda na kufanya kila wawezao kuondokana nao na bahati mbaya watakuwa hawana mtu katika historia wa kumfanya rejea ya namna alivyodeal na muungano na akatunza maslahi yao kama nchi!
Hayati Benjamin Mkapa hadi mwishoni mwa uhai wake alijuta sana yaliyotokea pemba kipindi cha utawala wake, na alitamani kuona Muungano wetu unaimarika na pia manung'uniko ya Wazanzibar yanaisha. Na alitamini kuona Wazanzibar wenyewe wanachagua kiongozi wao wenyewe kwa haki bila kuingiliwa.
Tumtumie Maalim kutuwekea precedence nzuri ya kuulinda muungano wetu, nje ya hapo tutegemee radicals wenye ushawishi wasioutaka huo muungano waungwe mkono na Wazanzibar kisha muuone kama huo muungano wenyewe mtafanikiwa kuulinda!
Hatuwezi kuulinda Muungano kwa "kuwateulia" Wazanzibari rais Dodoma kama tulivyofanya kwa huyu mnayemuita "rais mteule"
Maalim Shikamoo!
Ni miongoni mwa watu ambao mwalimu Nyerere aliwaheshimu sana kutokana na misimamo thabiti na kipawa chake kikubwa sana cha akili.
Lakini ukiacha kuipenda Tanzania, Maalim anaipenda sana Zanzibar, nchi aliyozaliwa. Wazanzibar wanamheshimu pia.
Sisi huku Tanganyika tuliamua kuendelea kumuita Nyerere "mwalimu", Siyo kwamba hakuna viongozi wengine walikuwa walimu huko zamani, bali ni kutokana na ukweli kuwa Nyerere alikuwa mtawala lakini pia aliendelea kuwa mwalimu wa falsafa za maendeleo na haki.
Na huko Zanzibar mzee wao wampendaye wakaamua kumuita "Maalim", hii ni lahaja tu za Kiswahili lakini mwalimu na maalim ni maneno yenye maana ileile kumaanisha "yule afundishaye"
Maalim Seif amekuwa mvumilivu mno katika masuala ya siasa, kafanyiwa faulo na madhambi chungu nzima katika njia yake ya kisiasa, lakini hajawahi kuhamasisha vurugu, uvunjifu wa amani, umwagaji damu au kuumiza Wazanzibar kwa sababu za kisiasa. Na kitendo hiki cha kuweka mbele maslahi ya wazanzibar ndicho kilichompa heshima sana mbele ya wazanzibar wenyewe.
Tanzania ya Leo ina bahati moja. Ina mtu ambaye ni kipenzi cha Wazanzibar, na pia ni muumini wa Muungano. Natoa rai kwa serikali ya Nchi hii, MTUMIENI HUYU MZEE VIZURI KULINDA MUUNGANO KABLA HAJATANGULIA MBELE YA HAKI!
Hatari ninayoiona ya kudhani kuwa Kuwalazimishia Wazanzibar kiongozi ndiyo njia sahihi ya kulinda muungano, hii ni njia yenye upeo mfupi sana, itafika mahali Wazanzibar watapata Kiongozi mwingine ambaye ni Radical, na huyu anaweza kuwamobilize Wazanzibar waukatae muungano.
Ikifikia hapo, ama itabidi mtumie nguvu kuulinda, mtapelekea umwagaji damu wa kutisha na Dunia itawagomea na itawalazimisha muwaache Wazanzibar wenyewe na nchi yao huku wahusika wa vitendo hivyo wakichukuliwa hatua na mahakama za kimataifa Au itabidi muwaachie tu nchi yao wajitawale!
Sasa sisi tukitumia busara hatupaswi kufika huko, Tumsaidie Maalim na Wazanzibar kwa kuwapa haki yao ya uchaguzi bila kuleta mambo ya Jecha, Kisha maalim atasaidia kuutetea muungano na wazanzibar watamsikiliza.
Uzuri wa mtu kama Maalim ni kuwa hawa ni aina ya viongozi ambao hata wakiwa wameshatangulia mbele ya haki basi vizazi na vizazi huendelea kuwafanya rejea ya utatuzi wa. mambo mbalimbali maana wanakuwa wameacha alama.
Kama Maalimu akiwa raisi wa Zanzibar na akafanikiwa kuweka precedence ya kuuheshimu muungano, basi amini usiamini huu Muungano utakuwa legitimized zaidi vizazi na vizazi vijavyo. Lakini mkimnyima maalim ushindi wake, kisha wazanzibar wakaweka dukuduku moyoni, basi dukuduku hilo litaendelea vizazi na vizazi vya wazanzibar na kuuona muungano kama project ya Ukoloni mamboleo na hivyo kuudharau, kutoupenda na kufanya kila wawezao kuondokana nao na bahati mbaya watakuwa hawana mtu katika historia wa kumfanya rejea ya namna alivyodeal na muungano na akatunza maslahi yao kama nchi!
Hayati Benjamin Mkapa hadi mwishoni mwa uhai wake alijuta sana yaliyotokea pemba kipindi cha utawala wake, na alitamani kuona Muungano wetu unaimarika na pia manung'uniko ya Wazanzibar yanaisha. Na alitamini kuona Wazanzibar wenyewe wanachagua kiongozi wao wenyewe kwa haki bila kuingiliwa.
Tumtumie Maalim kutuwekea precedence nzuri ya kuulinda muungano wetu, nje ya hapo tutegemee radicals wenye ushawishi wasioutaka huo muungano waungwe mkono na Wazanzibar kisha muuone kama huo muungano wenyewe mtafanikiwa kuulinda!
Hatuwezi kuulinda Muungano kwa "kuwateulia" Wazanzibari rais Dodoma kama tulivyofanya kwa huyu mnayemuita "rais mteule"
Maalim Shikamoo!