Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 7,899
- 10,415
HIZI HAPA HATUA TANO ANAZOPITIA GRADUATE WA KITANZANIA ANAPOMALIZA CHUO.
1. Mwaka wa kwanza baada ya kugraduate.Hapa bado kitaa hakijachanganya, anakua na hope kwamba atapata kazi muda wowote. Anatuma maombi sehemu mbali mbali, bado nguo za chuo na suti mbali mbali anazo, bado anang'aa, pengine anatumia muda huo kusalimia ndugu jamaa na kuzunguka mjini.
2.Mwaka wa pili baada ya kugraduate.Mambo ni magumu, nguo zimeisha, nyumbani anaanza kuonekana mzigo, anaanza kuwaza kujitolea, anapiga kazi yoyote inayokuja mbele yake. anatuma applications hamsini kwa siku na haitwi hata moja.
3. Mwaka wa tatu baada ya kugraduate.Hali ni mbaya zaidi, hakuna kinachoenda, matumaini yameisha, anaingia kwenye biashara, anafanya boda, anafanya bajaji etc. hapo lolote linalokaa mbele linafanywa ilimradi mkono uende kinywani.
4. Mwaka nne Baada ya kugraduate.Mawazo ya kuajiriwa yameisha, anafanya kazi zake za kujitegemea, ameanzisha familia, pengine amekua boda mzoefu, au winga mzoefu kariakoo na ameanza kufikiria maisha nje ya box. Akili zimeanza kukaa sawa sasa.
5. Mwaka wa Tano baada ya kugraduate. Mungu anajibu maombi, kama biashara zinaenda, au anapata kazi yake ya kwanza, anaingia kwenye ndoa, pengine anapata na kigari cha kutembelea. the rest inabaki kuwa ni historia.
Huyu ni Mtanzania wa kawaida, asiekua na connections.
1. Mwaka wa kwanza baada ya kugraduate.Hapa bado kitaa hakijachanganya, anakua na hope kwamba atapata kazi muda wowote. Anatuma maombi sehemu mbali mbali, bado nguo za chuo na suti mbali mbali anazo, bado anang'aa, pengine anatumia muda huo kusalimia ndugu jamaa na kuzunguka mjini.
2.Mwaka wa pili baada ya kugraduate.Mambo ni magumu, nguo zimeisha, nyumbani anaanza kuonekana mzigo, anaanza kuwaza kujitolea, anapiga kazi yoyote inayokuja mbele yake. anatuma applications hamsini kwa siku na haitwi hata moja.
3. Mwaka wa tatu baada ya kugraduate.Hali ni mbaya zaidi, hakuna kinachoenda, matumaini yameisha, anaingia kwenye biashara, anafanya boda, anafanya bajaji etc. hapo lolote linalokaa mbele linafanywa ilimradi mkono uende kinywani.
4. Mwaka nne Baada ya kugraduate.Mawazo ya kuajiriwa yameisha, anafanya kazi zake za kujitegemea, ameanzisha familia, pengine amekua boda mzoefu, au winga mzoefu kariakoo na ameanza kufikiria maisha nje ya box. Akili zimeanza kukaa sawa sasa.
5. Mwaka wa Tano baada ya kugraduate. Mungu anajibu maombi, kama biashara zinaenda, au anapata kazi yake ya kwanza, anaingia kwenye ndoa, pengine anapata na kigari cha kutembelea. the rest inabaki kuwa ni historia.
Huyu ni Mtanzania wa kawaida, asiekua na connections.