Hatua gani za kufuata ili kupata uhamisho Serikalini?

Hatua gani za kufuata ili kupata uhamisho Serikalini?

KING KIGODA

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2018
Posts
3,893
Reaction score
3,145
Habari,

Ni taratibu zipi nifuate ili kupewa uhamisho wa muda kutoka halmashauri moja kwenda nyingine au kwenda mashirika ya umma?
 
Ukienda kwa mwaajiri wako utapata msaada wote unao uhitaji. Na kama unataka kuhamia mashirika ya umma, basi chagua moja!

Kuandika barua ya kuacha kazi, au kuomba likizo ya bila malipo ya miaka mitatu.
 
Habari,

Ni taratibu zipi nifuate ili kupewa uhamisho wa muda kutoka halmashauri moja kwenda nyingine au kwenda mashirika ya umma?
""Uhamisho wa muda"" kwamba unaenda Halmashaur/Taasisi nyingine ya Serikali...Halafu utarudi tena ulipotoka baadae??????? Ndo unavyomaanisha?

Swali; kwa nini usiahamie tu huko unapopataka moja kwa moja?
 
Ukienda kwa mwaajiri wako utapata msaada wote unao uhitaji. Na kama unataka kuhamia mashirika ya umma, basi chagua moja!

Kuandika barua ya kuacha kazi, au kuomba likizo ya bila malipo ya miaka mitatu.
Mashirika ya umma...anaweza kuhamia kwa taratibu za kawaida za uhamisho.

Hiyo ya kuandika barua ya kuacha kazi haipo hiyo, na asifikirie hata kusoma hiyo sentensi yako.
 
Mashirika ya umma...anaweza kuhamia kwa taratibu za kawaida za uhamisho.

Hiyo ya kuandika barua ya kuacha kazi haipo hiyo, na asifikirie hata kusoma hiyo sentensi yako.
All in all, bado ushauri wangu mwingine utamsaidia wa kwenda kwa Mwajiri wake kujieleza kwa maneno au kwa kuandika hiyo barua ya uhamisho.

Maana hawezi kuhama bila ruhusa ya Mwajiri wake.
 
All in all, bado ushauri wangu mwingine utamsaidia wa kwenda kwa Mwajiri wake kujieleza kwa maneno au kwa kuandika hiyo barua ya uhamisho.

Maana hawezi kuhama bila ruhusa ya Mwajiri wake.
Sawa mkuu...but mtoa mada aje aelezee huo ""Uhamisho wa muda"" halafu tuanzie hapo[emoji23]
 
Habari,

Ni taratibu zipi nifuate ili kupewa uhamisho wa muda kutoka halmashauri moja kwenda nyingine au kwenda mashirika ya umma?
FUATA HATUA ZIFUATAZO

1. Andika barua ya KUOMBA NAFASI (SIYO YA UHAMISHO) katika Shirika la Umma unalotaka kuhamia ipitie kwa Mwajiri wako wa sasa.
2. Ukijibiwa kuwa nafasi ipo.
3. Andika barua ya KUOMBA UHAMISHO kwa Katibu Mkuu UTUMISHI kupitia kwa Mwajiri wako wa sasa ukiambatanisha na barua uliyopewa na Mkuu wa Shirika unalotaka kuhamia (Ile barua uliyojibiwa nafasi ipo).
4. Posti halafu subiria majibu au unaipeleka kwa Mkono unaenda KU-PUSH Wizarani UTUMISHI maana ukisubiri barua ikufikie utakaa sana hata mwaka na zaidi au inaweza kuja Mwajiri aka-MuTE nayo.

NB: Kuna baadhi ya Wakuu wa Taasisi kutokana na UHITAJI wao (Maana JPM alizuia ajira kwa muda mrefu) wakipata barua yako ya ya kuomba nafasi iliyopitishwa na Mwajiri wako wa sasa KUOMBA NAFASI wanamaliza wenyewe na UTUMISHI. ila ni wachache sana

Kila la heri mkuu kwa kutaka kukimbia TGS.
 
Sawa mkuu...but mtoa mada aje aelezee huo ""Uhamisho wa muda"" halafu tuanzie hapo[emoji23]
SECONDMENT mbona simpo tu akisashapokelewa anaweza kuhamia mojakwa moja kama mwajiri mpya atampenda au kumrudisha kwa mwajiri wa zamani baada ya mwaka mmoja
 
""Uhamisho wa muda"" kwamba unaenda Halmashaur/Taasisi nyingine ya Serikali...Halafu utarudi tena ulipotoka baadae??????? Ndo unavyomaanisha?

Swali; kwa nini usiahamie tu huko unapopataka moja kwa moja?
Uhamisho wa moja kwa moja ni lazima uchukue muda mrefu kukamilika na mimi nina matatizo ya kifamilia yanayo nilazimu kuwa home kwa haraka na kwa muda wa miezi miwili hadi mitatu hivi.
 
FUATA HATUA ZIFUATAZO

1. Andika barua ya KUOMBA NAFASI (SIYO YA UHAMISHO) katika Shirika la Umma unalotaka kuhamia ipitie kwa Mwajiri wako wa sasa.
2. Ukijibiwa kuwa nafasi ipo.
3. Andika barua ya KUOMBA UHAMISHO kwa Katibu Mkuu UTUMISHI kupitia kwa Mwajiri wako wa sasa ukiambatanisha na barua uliyopewa na Mkuu wa Shirika unalotaka kuhamia (Ile barua uliyojibiwa nafasi ipo).
4. Posti halafu subiria majibu au unaipeleka kwa Mkono unaenda KU-PUSH Wizarani UTUMISHI maana ukisubiri barua ikufikie utakaa sana hata mwaka na zaidi au inaweza kuja Mwajiri aka-MuTE nayo.

NB: Kuna baadhi ya Wakuu wa Taasisi kutokana na UHITAJI wao (Maana JPM alizuia ajira kwa muda mrefu) wakipata barua yako ya ya kuomba nafasi iliyopitishwa na Mwajiri wako wa sasa KUOMBA NAFASI wanamaliza wenyewe na UTUMISHI. ila ni wachache sana

Kila la heri mkuu kwa kutaka kukimbia TGS.
Sawa.Asante.
 
Back
Top Bottom