Hatua ya kwanza ya mafanikio ni kuondoka nyumbani

Hatua ya kwanza ya mafanikio ni kuondoka nyumbani

mwanazuoni mgeni

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2016
Posts
1,944
Reaction score
1,726
Hi wana Jf,
Nimejaribu kuchunguza hasa hizo nchi zetu za Africa hususani (East Africa) limekuwa ni jambo la kawaida kukuta kijana ana miaka takribani 30 na bado anaishi kwa wazazi wake bila aibu anasubiri ugali wa shikamoo.
Hili jambo ukiliangalia kwa mapana utagundua linasababishwa na vitu Vingi..

Mfano mfumo wetu wa elimu nao unachangia kwa sababu elimu mtu anayopata mpaka chuo kikuu haimjengi muhusika katika kuwa na mawazo ya kujiajiri . Tatizo linakuja pale mtu kamaliza chuo alafu kakosa kazi ..utashangaa mtu anakaa nyumbani mpaka anaoa/kuolewa akiwa nyumbani.

Lakini upande wa pili hata kama mtu hajasoma pia bado utakuta anaishi nyumbani kwa wazazi akiwa na umri mkubwa..mi nadhani pia sisi wa Africa uvivu unatupeleka pabaya.

Tumezoea kukaa vijiweni muda mwingi tukijadili mambo yasiyo na msingi na tumekuwa watu wa kutojali muda kabisa... Wala hatuna ratiba ..

Yangu ni hayo tuu kama kuna mwingine mwenye mawazo tofauti na mimi anaweza akaongeza au kunipinga kwa hoja lakini...
Nawasilisha
 
Wabongo tuna akili finyu na kudhani kukimbia kwenu ndio kwenda kutafuta maendeleo, hebu tuangalie jamii za Waasia na waarabu wengi hupenda kuishi katika familia kubwa, unamkuta babu, mtoto na wajukuu wanakaa kwenye mansion moja na bado wametuzidi mara hamsini kwenye maendeleo.
 
Hi wana jf
Nimejaribu kuchunguza hasa hizo nchi zetu za Africa hususani (east Africa) limekuwa ni jambo LA kawaida kukuta kijana ana miaka takribani 30 na bado anaishi kwa wazazi wake .. Bila aibu anasubiri ugali wa shikamoo.. Hili jambo ukiliangalia kwa mapana utagundua linasababishwa na vitu Vingi..

Mfano mfumo wetu ww elimu nao unachangia kwa sababu elimu MTU anayopata mpaka chuo kikuu haimjengi muhusika katika kuwa na mawazo ya kujiajiri .tatizo linakuja pale MTU kamaliza chuo alafu kakosa kazi ..utashangaa MTU anakaa nyumbani mpaka anaoa/kuolewa akiwa nyumbani..

Lakini upande wa pili hata kama MTU hajasoma pia bado utakuta anaishi nyumbani kwa wazazi akiwa na umri mkubwa..me nadhani pia sisi wa Africa uvivu unatupeleka pabaya... Tumezoea kukaa vijiweni muda mwingi .tukijadili mambo yasiyo na msingi... Na tumekuwa watu wa kutojali muda kabisa.... Wala hatuna ratiba ..

Yangu ni hayo tuu kama kuna mwingine mwenye mawazo tofauti na Mimi anaweza akaongeza au kunipinga kwa hoja lakini...
Nawasilisha
 
Wabongo tuna akili finyu na kudhani kukimbia kwenu ndio kwenda kutafuta maendeleo, hebu tuangalie jamii za Waasia na waarabu wengi hupenda kuishi katika familia kubwa, unamkuta babu, mtoto na wajukuu wanakaa kwenye mansion moja na bado wametuzidi mara hamsini kwenye maendeleo.
Akili za mwendokasi mbaya, mtu anasemea kwa African setting wewe unatuletea waasia
 
kibongo bongo ni heri kutoka home ukaenda kujitafutia maisha hasa pale unapoona hali ya home hairuhusu na wewe ni mkubwa.
kwa wasio wabongo wakiona home mambo safi hakuna kuondoka ni kubanana hapohapo kurithi utajiri na mtoto akitaka kusepa wazazi wanamkataza wanamtengenezea mazingira ya kuwa mrithi wao...
shida ya huku kwetu unakuta familia ina watoto 8 au zaidi, mtoto wa kwanza kamaliza chuo kikuu mdogo wake wa mwisho hata chekechea hajaanza, so kuendelea kukaa home ni kubana tu nafasi kwanza unajishtukia mwenyewe.
 
Wabongo tuna akili finyu na kudhani kukimbia kwenu ndio kwenda kutafuta maendeleo, hebu tuangalie jamii za Waasia na waarabu wengi hupenda kuishi katika familia kubwa, unamkuta babu, mtoto na wajukuu wanakaa kwenye mansion moja na bado wametuzidi mara hamsini kwenye maendeleo.
Mkuu umeongelea watu wa Asia na Mimi nine base kwa jamii za Africa ambazo nyingi ni masikini na pia zina utamaduni tofauti..... Sasa kuna faida gan kukaa familia yenye watoto kumi afu bado familia ni ya hali ya chini
 
Back
Top Bottom