SoC01 Hatua za msingi na wajibu katika jamii na Serikali yake ili kujenga taifa endelevu

SoC01 Hatua za msingi na wajibu katika jamii na Serikali yake ili kujenga taifa endelevu

Stories of Change - 2021 Competition

ImanHB

Member
Joined
Mar 14, 2019
Posts
10
Reaction score
17
Sadoth H. Balilonda
( Mjasiliamali )
sadothhenry250@gmail.com
+255756536474/+255676436474



Makala hii inatoa muamko ambao unalenga kuchochea mabadiliko katika nyanja mbalimbali za uchumi kupitia biashara, kilimo, sayansi na teknolojia, afya, maendeleo ya jamii na uajibikaji kwa ujumla. Lengo ni kujenga taswira nzuri ya maendeleo ya uchumi wa taifa
  • Tunapozungunzia uchumi tunazungumzia jumla ya shughuli zile zote za kibinadamu zinazomuingizia mtu kipato kinachotosheleza mahitaji yake. Kuna shughuli kadha wa kadha ambazo kila mtu ni kipao mbele chake kujimudu kimaisha hasa katika uzalishaji. Hii ni kwa ngazi ya chini {jamii}, kwa upande wa serikali, uchumi unatafasilika kwa upana zaidi {kitaifa}. Kuna shughuli mbalimbali za uchumi nazo huegemea katika idara za serikali ambazo ndio watendaji wakuu kuhakikisha shughuli hizo zinanufaisha jamii na kuliingizia taifa kipato sahihi.

Shughuli na vyanzo vya uchumi ambavyo idara husika zikisimamia vyema
zitaleta tija katika Taifa.


  • MIUNDOMBINU BORA
Hakika katika kuboresha miundombinu, serikali yetu imejitahidi sana hasa idara ya usafirishaji pande zote majini, ardhi na anga. Lakini ni vyema ikaangazia pia na upande wa nishati nikimaanisha nishati ya umeme hasa vijijini na maeneo ya makazi na viwanda vidogovidogo, ingawa wanapata huduma ya umeme wa REA lakini bado wanakumbwa na tatizo la umeme kukatikakatika mara kwa mara kitendo ambacho kinasababisha kuzorota na kukwamisha wazalishaji wadogowadogo ambao kodi zao hizo ndogondogo zinashiriki katika mchango mkubwa kuinua uchumi wa nchi. Iwapo miradi mikubwa ya kufua umeme JNHPP inayotarajiwa kukamilika february 2022 ipo katika mkakati, basi iwekewe nguvu kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

  • KILIMO​
Pato la taifa hutegemea zaidi kilimo, hivyo inaonyesha ni jinsi gani kilimo kina mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa. Kwakuwa zaidi ya asilimia 80 ya ardhi hapa nchini inatawaliwa na wakulima wadogowadogo wakitegemea jembe la mkono, plau na trekta kwa baadhi yao, serikali kupitia wizara ya kilimo itenge bajeti ya fedha ambazo zitamuwezesha mkulima kutatua changamoto za pembejeo, mbegu bora, mbolea na hata pia wapatiwe mafunzo ya elimu ya kilimo bora. Siyo hilo tu lakini pia ni wazi kuwa nchi hii inakumbwa na migogoro ya ardhi, hii ni kwa sababu sehemu kubwa ya ardhi haijapimwa na kuendelezwa, hivyo hupelekea watu kufanya shughuli zao tofauti na matumizi ya eneo husika kama kuchoma misitu, kuweka makazi hifadhi za wanyama na kuchunga mifugo maeneo yasiostahili.

  • AFYA​
Afya bora kwa jamii ni jambo la kupewa kipaombele, si kwa kuitegemea serikali tu kama ilivyo ada, ijenge vituo vya afya vyenye dawa za kutosha na watoa huduma wa kukidhi mahitaji ya wagonjwa. Pia ni jukumu la jamii kwa kila mtu kuchukua hatua stahiki juu ya changamoto zinazoweza kuathiri afya zetu ikiwemo kuzingatia usafi wa mazingira yanayotuzunguka na kuhakikisha vitendea kazi na vyakula tunavyotumia viko salama kwa afya zetu. Na kwa upande mwingine tunapaswa kuchukua tahadhali dhidi ya milipuko ya magonjwa yanayojitokeza, hasa kwa wakati huu mgumu tunaopitia wa janga la Corona, ni wazi tunahitajika kuchukua tahadhali zaidi kwa kutekeleza maagizo yanayotolewa na wizara za afya kujikinga na gonjwa hili.

  • SAYANSI NA TEKNOLOJIA​
Tume ya taifa ya sayansi na teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na taasisi zingine pamoja na vyuo vya sayansi na ufundi stadi ndani na nje ya nchi, ni wakati sahihi wa kukaa pamoja kujadili, kutatua na kutathminni ni nini kifanyike ili kukuza na kuendeleza ujuzi wetu wa ndani.

Tanzania tunaweza, wapo vijana wengi katika jamii zetu wanao ujuzi, vipaji na ndoto za kufika mbali kimaendeleo kulingana na vipawa tofautitofauti walivyojaaliwa na Mwenyezi Mungu na wengine ni wazee sasa wamezeeka navyo, nani wa kuwashika mkono? Haya ni malighafi, idara, tume na taasisi za elimu chonde tunaomba zifanye maboresho katika mitaala yake ya elimu. Kuwepo na vitengo vya elimu maaalumu ya kuinua vipaji kwa kila mtanzania mwenye ujuzi wake na hata wale angali bado wana umri mdogo.

  • UWAJIBIKAJI NA MAENDELEO YA JAMII​
AJIRA; Vijana ndio nguvukazi ya taifa. Tumegawanyika katika makundi tofauti kwa ngazi mbalimbali za elimu. Naweza kusema ya kwamba tumekuwa tukijijengea dhana, malengo, fikra na mitazamo hasi katika swala la ajira hasa kwa wahitimu. Kuajiriwa ni jambo la kheri katika hatua za mafanikio, lakini kulingana na sababu nyingi ikiwemo utekelezaji wa miradi ya kimikakati kuwa wa hali ya chini, uhaba wa viwanda na makampuni mengi kuzingatia sifa za ufaulu kwa waombaji, ukweli wengi wetu huishia manung'uniko. Kizazi cha sasa wasomi ni wengi nafasi za ajira ni chache ukweli hazijawahi kukidhi idadi ya wahitimu katika muhula husika.
Ukosefu wa ajira mtaani.jpg

Ukosefu wa ajira mtaani ; Chanzo IPP Media

Hivyo basi nini cha kufanya?...Tuamke, tuwajibike na kuondoa dhana ya kusubiri kuajiriwa iwe una degree au haujabahatika kupata elimu, badala yake kutumia fursa na vipawa tulivyonavyo kujenga mifumo sahihi ya kujiajiri. Angalia faida za kujiajiri link hapo chini
Faida za kujiajiri

LABDA NIKUSHUHUDIE: "Mimi mwenyewe Mungu ni muweza nilibahatika kupata elimu ya kidato cha nne mwaka 2015. Nilipomaliza nikafanikiwa kupata ufaulu wa kujiunga na chuo cha uuguzi Geita, nikatuma maombi ya kujiunga yakapokelewa. Lakini kwa bahati mbaya gharama za masomo zikawa kubwa kulingana na corse niliyochukua hivyo sikuweza kuimudu kutokana matatizo ya kifedha. Hivyo basi nilikuwa na rafiki yangu nilieishi nae kama ndugu yeye alikuwa anajishughulisha na uuzaji wa miche ya matunda, ndipo na mimi nikaona bora nijiegeshe kwake nikiwa namsaidia saidia kuchanganya udongo, mbolea na kupakia kwenye vimfuko. Baada ya miezi 3 nikawa na uzoefu, Mungu amjaalie zaidi alinipa kaeneo pembezoni na kunishauri nianze kupanda miche yangu mwenyewe. Kwa juhudi namshukuru Mungu bustan yangu ilipanuka na kupata wateja. Lakini akili yangu haikukomea hapo, nilipopata akiba ya kutosha mwaka 2017 mwezi 5 nilimuajiri mtu wa kusimamia bustan, nikajiunga na kalakana ya uchomeleaji hapohapo mtaani. Baada ya mwaka mmoja na nusu kujua ufundi, mwaka juzi 2019 mwezi wa pili wishoni kwa fedha ninazoingiza kwenye bustani nikafungua kalakana yangu mwenyewe. Na amini usiamini mpaka sasa namiliki kalakana mbili ya welding (uchomeleaji) na ya Alminium pamoja na bustani kubwa."
Mimi ni nani na wewe ni nani ushindwe. Elimu yako ulionayo kamwe haiwezi kuamua kiwango cha mafanikio yako ya baadae, bali ni juhudi zako tu ndizo zitakazoamua. THUBUTU UNAWEZA!!!
 
Upvote 3
Kama tuko pamoja kwenye mjadala huu naomba ushirikiano wenu katika kuiendeleza kampeni ya maendeleo ya taifa letu
Pia usisahau kuacha kura yako juu ya andiko hili kama umeguswa Mungu akubaariki.
 
Kama tuko pamoja kwenye mjadala huu naomba ushirikiano wenu katika kuiendeleza kampeni ya maendeleo ya taifa letu
Pia usisahau kuacha kura yako juu ya andiko hili kama umeguswa Mungu akubaariki.
Nimependa sanaa hatua ya mafanikio uliofikia kwa kujituma
Ni vyema na sisi tukajifunza kwako
 
Nimependa sanaa hatua ya mafanikio uliofikia kwa kujituma
Ni vyema na sisi tukajifunza kwako
Thanks, Hata serikali inatakiwa ilione hili itusaidie kutupatia elimu ya ujasiliamali katika na pia ifundishwe shuleni kama masomo mengingine kwa ngazi zote za elimu. Sio mpaka mtu afuzu kidato cha nne au cha sita akiwa na vigezo ndo akajiunge na chuo cha biashara, tutashindwa kabisa
 
Thanks, Hata serikali inatakiwa ilione hili itusaidie kutupatia elimu ya ujasiliamali katika na pia ifundishwe shuleni kama masomo mengingine kwa ngazi zote za elimu. Sio mpaka mtu afuzu kidato cha nne au cha sita akiwa na vigezo ndo akajiunge na chuo cha biashara, tutashindwa kabisa
Ibadilii mfumo wa elimu
 
Ukweli imenigusa maana hat me ni muanga wa ajira nimemalza certificate ya ualimu 2018 mpk leo hii niko nyumbn nafac zinatoka nafany aplication lakn sibahatiki
 
Ukweli imenigusa maana hat me ni muanga wa ajira nimemalza certificate ya ualimu 2018 mpk leo hii niko nyumbn nafac zinatoka nafany aplication lakn sibahatiki
Pole sana jitahidi kutafuta suruhisho ikiwezekana funngua hata biashara.Na km tatizo ni mtaji wa fedha, biashara haihitaji mtaji mkubwa wa fedha, ila inahitaji juhudi kubwa na nidhamu. Huo ndio mtaji wa biashara. Ukijituma na kuwa na nidhamu ya fedha unaweza kuukuza mtaji wa elf 15 kuwa milion 15.
 
Ni waazo zuri ni km ulikuwa kweny akili yang nilishawah kufikiria hvy
Ila sasa napata changamoto kujua ni kaz gani au biashar nawez fanya maan sjawahi na uzoefuu
 
Na sina uzoefu wa biashara yoyote
Thubutu unaweza. Kuna shughuli nyingi zakibiashara ambazo unaweza kkujikwamua kimaisha
shughuli hizo ni kama;
  • Utengenezaji wa sabuni za maji na miche
  • Kuanzisha kitalu cha miti na miche ya matunda
  • Kuanzisha bustani za mbogamboga
  • Ufugaji wa kuku
  • Ufugaji wa samaki
  • Ushonaji wa nguo (cherehani)
Na nyingne nyingi. shughuli hizi hazihitaji mtaji mkubwa ila ni uthubutu juhudi na nidhamu ya muda na fedha
Mafunzo yake si ya ghalama sana pia unaweza kupata mafunzo hayo hata kupitia njia za mtandaoni
 
Usingoje mpaka mtu mwingine aje kuitumikisha elimu yako, ni vyema ukaitumikishe mwenyewe kwanza ndo ikusaidie
 
Mafanikio ni jitihada na bidii zako mwenyewe
 
Back
Top Bottom