MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi.
Toka mwaka jana nilianza kupata mashaka makubwa kuhusu haya matokeo yaliyosheheni division one za saba kiasi cha kutia shaka. Leo nimebahatika kupata sababu mbili za kuyapuuza haya matokeo ya kisiasa;
1. A kwa sasa inaanzia 75% badala ya 81% iliyokuwepo kwa miaka mingi. Kama tayari iko wazi kwamba mitihani imelegezwa hakukuwa na haja ya kutanua goli ili wanafunzi wapate A kirahisi. Wizara ya elimu inatakiwa itoe majibu ya kina kuhusu hili.
2. Hakuna penalty ya Hesabu. Hii sababu namba mbili ndo imefanya kuwepo na One nyingi sana zilizokosa uhalali. Hivi tunaandaa taifa gani lisilojua hesabu huko mbeleni? Hesabu ni sehemu ya maisha ya kila siku ilipaswa iachwe na penalty yake kama ilivyokuwa. Waliofanya huu uamuzi wa kuondoa penalty kwa F ya hesabu ninawalaani. Ni uamuzi wa kushoofisha kabisa taifa. Ni wahujumu.
Ni wito wangu Wizara ya elimu kujirekebisha na kuondoa huu uozo uliopo. Mwisho kabisa naomba kama kuna mtu mwenye list ya shule zote za sekondari zinazomilikiwa na CCM anitumie ili niangalie matokeo yao kwasababu naamini watakuwa wamefanya vizuri sana maana wao ndo wenye ilani ya uchaguzi.
Toka mwaka jana nilianza kupata mashaka makubwa kuhusu haya matokeo yaliyosheheni division one za saba kiasi cha kutia shaka. Leo nimebahatika kupata sababu mbili za kuyapuuza haya matokeo ya kisiasa;
1. A kwa sasa inaanzia 75% badala ya 81% iliyokuwepo kwa miaka mingi. Kama tayari iko wazi kwamba mitihani imelegezwa hakukuwa na haja ya kutanua goli ili wanafunzi wapate A kirahisi. Wizara ya elimu inatakiwa itoe majibu ya kina kuhusu hili.
2. Hakuna penalty ya Hesabu. Hii sababu namba mbili ndo imefanya kuwepo na One nyingi sana zilizokosa uhalali. Hivi tunaandaa taifa gani lisilojua hesabu huko mbeleni? Hesabu ni sehemu ya maisha ya kila siku ilipaswa iachwe na penalty yake kama ilivyokuwa. Waliofanya huu uamuzi wa kuondoa penalty kwa F ya hesabu ninawalaani. Ni uamuzi wa kushoofisha kabisa taifa. Ni wahujumu.
Ni wito wangu Wizara ya elimu kujirekebisha na kuondoa huu uozo uliopo. Mwisho kabisa naomba kama kuna mtu mwenye list ya shule zote za sekondari zinazomilikiwa na CCM anitumie ili niangalie matokeo yao kwasababu naamini watakuwa wamefanya vizuri sana maana wao ndo wenye ilani ya uchaguzi.