Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Kwenye Michezo, ikiwemo soka ndiyo sehemu pekee wanapokutana watu wa Itikadi Tofauti, wanaweza kuwa Chama kimoja cha Siasa lakini wakakutana uwanjani wakiwa Timu tofauti, Na waweza kuwa Mahasimu kisiasa lakini wakawa wanashabikia timu moja. Hii ni kwa sababu Michezo haihusiani na Siasa wala vyama vya kisiasa.
Ili kulinda Mambo haya hatutegemei kabisa kuona Mabango ya Wanasiasa kwenye Tamasha la Simba Day wala lile la Wiki ya Mwananchi, kwa sababu, kufanya hivyo kunaweza kusababisha vurugu kutoka kwa pande tofauti za kisiasa kunakoweza kusababisha Maafa.
Kuna Maeneo mengi mno ya kubandika mabango ya Wanasiasa, zikiwemo ofisi za vyama vyao na kwenye mabango ya kulipia yaliyojaa kila mahali, ama hata kwenye nyumba binafsi ya ambaye amependa kuweka bango la Mwanasiasa amtakaye.
Natoa Wito kwa Mamlaka kuzuia Upuuzi wa Kubeba Mabango yenye picha za wanasiasa kwenye matamasha haya ili kulinda amani.
Kama unampenda mtu kwa sababu ya sura yake basi nenda kanywe naye chai- JK Nyerere
Soma pia: SIMBA DAY 2024: Simba SC vs APR | Mkapa Stadium | 03/08/2024
Ili kulinda Mambo haya hatutegemei kabisa kuona Mabango ya Wanasiasa kwenye Tamasha la Simba Day wala lile la Wiki ya Mwananchi, kwa sababu, kufanya hivyo kunaweza kusababisha vurugu kutoka kwa pande tofauti za kisiasa kunakoweza kusababisha Maafa.
Kuna Maeneo mengi mno ya kubandika mabango ya Wanasiasa, zikiwemo ofisi za vyama vyao na kwenye mabango ya kulipia yaliyojaa kila mahali, ama hata kwenye nyumba binafsi ya ambaye amependa kuweka bango la Mwanasiasa amtakaye.
Natoa Wito kwa Mamlaka kuzuia Upuuzi wa Kubeba Mabango yenye picha za wanasiasa kwenye matamasha haya ili kulinda amani.
Kama unampenda mtu kwa sababu ya sura yake basi nenda kanywe naye chai- JK Nyerere
Soma pia: SIMBA DAY 2024: Simba SC vs APR | Mkapa Stadium | 03/08/2024