Hawa DP WORLD siyo wawekezaji bali ni mchwa

Hawa DP WORLD siyo wawekezaji bali ni mchwa

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
SERIKALI IJIANDAE KUWATETEA DP WORLD KWA SABABU AJIRA NA MAPATO YA BANDARI YATAKASHUKA MNO!

Hawa DP WORLD siyo wawekezaji bali ni mchwa. Tuna mapigo matatu yanahusiana na huu uwekezaji wa kifisadi yanakuja bila kuchelea.

Pigo la kwanza mapato yatashuka kinyume na matarajio yao. Mapato ya wateja wa bandari ya Dar-es-Salaam yatashuka kutokana na kudorora kwa uchumi wa dunia na hawatasafirisha mizigo mingi.

Pigo la pili baada ya TPA kuporwa ugali itabidi wapunguze ajira kutoka wafanyakazi 3, 450 hadi 600 tu. Serikali iliahidi ajira kutoathirika lakini ukweli zitapungua mno.

Pigo la tatu, mizigo haitaongezeka bali itapungua. Wao wanadai ufanisi utaongeza tashwishwi ya kutumia bandari ya Dar lakini uhalisia sababu kuu ya kupanda matumizi ya bandari ni kasi ya kukua GDP. Na kila kipimo kinaonyesha mapato ndani ya SADCC yatashuka.

Wajiandae kumtetea mwekezaji kwa kushindwa kuongeza mapato na kukaza buti kutukamua kwa kodi kufidia pengo la mwekezaji hewa.

Sisi wengine ni mbavu zetu tu zitakazo kuwa hoi pale matutusa watakapobainika walidhani wanajua kumbe hawajui kitu.

Mfupa ulilolishinda jimbo la Delaware Marekani sisi ndiyo kabisa tusubirie porojo za kwanini mapato na ajira zimetoweka.

Jimbo la Delaware lina mkataba bora kuliko huu wetu wa kitumwa lakini hadi sasa miaka 6 imepita hawajalipwa hata senti moja na DubaiTainer pamoja na mizigo yao kuwa karibu mara tatu ya bandari ya Dar-es-Salaam. Mara wamesingizia kovid na sasa wanajitetea uchumi wa dunia umeyumbishwa na vita vya Ukraine, vikwazo vya uchumi dhidi ya Urusi na Uchina n.k
 
Mpiga ramli kazini. Kwenye sayansi mapato hayawezi shuka. Nyie ndo mnapiga sana hela hapo Bandarini. Wizi kila kukicha hadi serikali inakosa mapato.
 
Mpiga ramli kazini. Kwenye sayansi mapato hayawezi shuka. Nyie ndo mnapiga sana hela hapo Bandarini. Wizi kila kukicha hadi serikali inakosa mapato.
Sayansi ipi? Mapato hayana uhusiano na ufanisi tu bali ukubwa wa pato la taifa ambalo litashuka. Wateja wote wa bandari uchumi kughairi na hivyo kutoagiza au kusafirisha mizigo mingi. Na TPA kwa kupunguziwa shughuli idadi ya wafanyakazi nayo itabidi ipungue na mwekezaji hatawahitaji kwa sababu anatumia mitambo.

Hivi wajua sayansi ni nini?
 
Sayansi ipi? Mapato hayana uhusiano na ufanisi tu bali ukubwa wa pato la taifa ambalo litashuka. Na TPA kwa kupunguziwa shughuli idadi ya wafanyakazi nayo itabidi ipungue na mwekezaji hatawahitaji kwa sababu anatumia mitambo.

Hivi wajua sayansi ni nini?
Hujui tu! Pale TPA kuna mapato mengi sana yanaishia mikononi mwa watu walioweka mizizi pale. Mapato tuliyopaswa kuyapata kutokana na uwekezaji tunaoufanya kama taifa ni makubwa sana almost mara 3 hadi 4 ya tunayoyapata sasa.

Kilichoenda kufanyika ni kuweka mfumo mpya ili kuzuia huo upoteaji wa mapato hayo na Serikali kuhakikisha inapata mapato yake vizuri.

Kamwe haitotokea mapato kushuka. Niamini
 
Sasa nakuambia hivi kuna shehena zinatongezeka kwa promo ya hao jamaa baadhi ya wateja wao wataanza kuleta mizigo.

Pia serikali itakaliwa koo katika ufuatilia wa utendaji kazi na hao jamaa wakiwa wanafanya kazi presha itakuwa juu sana ,bado watakuwa wankosolewa kwa siasa za hapa na pale ...kwa maana hiyo lazima watakuwa wafanisi ,mtakuja kusikia mfanyakazi fulani mweusi kanyanyaswa ili mradi tu wanasiasa kuleta taharuki.
 
Sasa nakuambia hivi kuna shehena zinatongezeka kwa promo ya hao jamaa baadhi ya wateja wao wataanza kuleta mizigo.

Pia serikali itakaliwa koo katika ufuatilia wa utendaji kazi na hao jamaa wakiwa wanafanya kazi presha itakuwa juu sana ,bado watakuwa wankosolewa kwa siasa za hapa na pale ...kwa maana hiyo lazima watakuwa wafanisi ,mtakuja kusikia mfanyakazi fulani mweusi kanyanyaswa ili mradi tu wanasiasa kuleta taharuki.
Uchumi wa dunia unashuka na uwezo wa wateja wa bandari ya Dar-es-Salaam kuagiza mizigo utapungua mno tatizo ambalo limeikumba bandari ya Wilmington ya Delaware na mapato kupungua.


Kwenye hilo huwezi kuchakachua kama walivyozoea.
 
Acha
SERIKALI IJIANDAE KUWATETEA DP WORLD KWA SABABU AJIRA NA MAPATO YA BANDARI YATAKASHUKA MNO!

Hawa DP WORLD siyo wawekezaji bali ni mchwa. Tuna mapigo matatu yanahusiana na huu uwekezaji wa kifisadi yanakuja bila kuchelea.

Pigo la kwanza mapato yatashuka kinyume na matarajio yao. Mapato ya wateja wa bandari ya Dar-es-Salaam yatashuka kutokana na kudorora kwa uchumi wa dunia na hawatasafirisha mizigo mingi.

Pigo la pili baada ya TPA kuporwa ugali itabidi wapunguze ajira kutoka wafanyakazi 3, 450 hadi 600 tu. Serikali iliahidi ajira kutoathirika lakini ukweli zitapungua mno.

Pigo la tatu, mizigo haitaongezeka bali itapungua. Wao wanadai ufanisi utaongeza tashwishwi ya kutumia bandari ya Dar lakini uhalisia sababu kuu ya kupanda matumizi ya bandari ni kasi ya kukua GDP. Na kila kipimo kinaonyesha mapato ndani ya SADCC yatashuka.

Wajiandae kumtetea mwekezaji kwa kushindwa kuongeza mapato na kukaza buti kutukamua kwa kodi kufidia pengo la mwekezaji hewa.

Sisi wengine ni mbavu zetu tu zitakazo kuwa hoi pale matutusa watakapobainika walidhani wanajua kumbe hawajui kitu.

Mfupa ulilolishinda jimbo la Delaware Marekani sisi ndiyo kabisa tusubirie porojo za kwanini mapato na ajira zimetoweka.

Jimbo la Delaware lina mkataba bora kuliko huu wetu wa kitumwa lakini hadi sasa miaka 6 imepita hawajalipwa hata senti moja na DubaiTainer pamoja na mizigo yao kuwa karibu mara tatu ya bandari ya Dar-es-Salaam. Mara wamesingizia kovid na sasa wanajitetea uchumi wa dunia umeyumbishwa na vita vya Ukraine, vikwazo vya uchumi dhidi ya Urusi na Uchina n.k
Ach ujinga
 
SERIKALI IJIANDAE KUWATETEA DP WORLD KWA SABABU AJIRA NA MAPATO YA BANDARI YATAKASHUKA MNO!

Hawa DP WORLD siyo wawekezaji bali ni mchwa. Tuna mapigo matatu yanahusiana na huu uwekezaji wa kifisadi yanakuja bila kuchelea.

Pigo la kwanza mapato yatashuka kinyume na matarajio yao. Mapato ya wateja wa bandari ya Dar-es-Salaam yatashuka kutokana na kudorora kwa uchumi wa dunia na hawatasafirisha mizigo mingi.

Pigo la pili baada ya TPA kuporwa ugali itabidi wapunguze ajira kutoka wafanyakazi 3, 450 hadi 600 tu. Serikali iliahidi ajira kutoathirika lakini ukweli zitapungua mno.

Pigo la tatu, mizigo haitaongezeka bali itapungua. Wao wanadai ufanisi utaongeza tashwishwi ya kutumia bandari ya Dar lakini uhalisia sababu kuu ya kupanda matumizi ya bandari ni kasi ya kukua GDP. Na kila kipimo kinaonyesha mapato ndani ya SADCC yatashuka.

Wajiandae kumtetea mwekezaji kwa kushindwa kuongeza mapato na kukaza buti kutukamua kwa kodi kufidia pengo la mwekezaji hewa.

Sisi wengine ni mbavu zetu tu zitakazo kuwa hoi pale matutusa watakapobainika walidhani wanajua kumbe hawajui kitu.

Mfupa ulilolishinda jimbo la Delaware Marekani sisi ndiyo kabisa tusubirie porojo za kwanini mapato na ajira zimetoweka.

Jimbo la Delaware lina mkataba bora kuliko huu wetu wa kitumwa lakini hadi sasa miaka 6 imepita hawajalipwa hata senti moja na DubaiTainer pamoja na mizigo yao kuwa karibu mara tatu ya bandari ya Dar-es-Salaam. Mara wamesingizia kovid na sasa wanajitetea uchumi wa dunia umeyumbishwa na vita vya Ukraine, vikwazo vya uchumi dhidi ya Urusi na Uchina n.k
Hoja yako ni ipi hasa?
 
Uchumi wa dunia unashuka na uwezo wa wateja wa bandari ya Dar-es-Salaam kuagiza mizigo utapungua mno tatizo ambalo limeikumba bandari ya Wilmington ya Delaware na mapato kupungua.


Kwenye hilo huwezi kuchakachua kama walivyozoea.
Katika kukubailiana na hilo ndo utajua utendanji kazi wao katika kuendana na economic trend ,tuwaache tuone.

Mapema sana kuwapinga.
 
Bandari zetu ni urithi wetu ,kataa madalali ,kataa wahuni ,kataa wezi wa rasilimali.
 
Hujui tu! Pale TPA kuna mapato mengi sana yanaishia mikononi mwa watu walioweka mizizi pale. Mapato tuliyopaswa kuyapata kutokana na uwekezaji tunaoufanya kama taifa ni makubwa sana almost mara 3 hadi 4 ya tunayoyapata sasa.

Kilichoenda kufanyika ni kuweka mfumo mpya ili kuzuia huo upoteaji wa mapato hayo na Serikali kuhakikisha inapata mapato yake vizuri.

Kamwe haitotokea mapato kushuka. Niamini
Hao wezi wa Bandarini Taasisi zetu zote pamoja na Rais mwenyewe wameshindwa kuwadhibiti wanahitaji mamluki kwa gharama kubwa ya fedha,udhalilishaji na mgawanyiko mkubwar kiasi hiki?
 
Hao wezi wa Bandarini Taasisi zetu zote pamoja na Rais mwenyewe wameshindwa kuwadhibiti wanahitaji mamluki kwa gharama kubwa ya fedha,udhalilishaji na mgawanyiko mkubwar kiasi hiki?
Gharama kubwa kivipi?udhalilishaji kivipi?
 
Back
Top Bottom