Hawa ndio mapacha wawili wa kuibeba simba msimu huu

Hawa ndio mapacha wawili wa kuibeba simba msimu huu

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
okwi 7.jpg

Bosi Msaidizi wa benchi la ufundi la Simba, Jackson Mayanja, raia wa Uganda, amefunguka kuwa, kombinesheni ya washambuliaji wao, Emmanuel Okwi na Juma Liuzio itaweza kuwa msaada mkubwa ndani ya kikosi hicho baada ya kujaribu kombinesheni za washambuliaji mbalimbali lakini zikafeli.

Kwa mara ya kwanza Okwi na Liuzio walianza pamoja kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ruvu Shooting na kufanikiwa kuifungia timu hiyo mabao matano. Simba walishinda mabao 7-0 huku Okwi akifunga manne na Liuzio moja.
Mayanja amesema kutokana na kiwango cha wachezaji hao, wanaweza kuitumia pacha hiyo ambayo imeonekana kuelewana zaidi ya walivyokuwa wanacheza wachezaji wengine.
“Niwe mkweli kabisa hii pacha ya Okwi na Liuzio leo (juzi Jumamosi) ndiyo imetubeba na kuweza kuibuka na ushindi huu wa mabao saba, wote wamecheza kwa kasi na walikuwa wasumbufu kwa wapinzani wetu.

“Tuliamua kuwaanzisha wachezaji hao kwa sababu tuliona Liuzio ana kasi, nguvu na mwepesi wa kufanya maamuzi na kweli jambo hilo limesaidia kwani wapinzani wetu muda mwingi walikuwa wanamkaba yeye na kumuachia Okwi ambaye alikuwa anafunga kirahisi,” alisema Mayanja

Salehe Jembe
 
Sawa sisi wapenzi wa Simba sc, tunachotaka ni kuzifunga magoli mengi timu zote zitakazo katisha mbele yetu mwaka huu.
Luizio asipozidisha umakini wa Ufungaji atanyang'anywa hiyo namba na Emmanuel Gyan anayekuja mwishoni mwa wiki hii ya mwezi wa nane 2017.
 
mleta uzi hiv umeangalia ni magoli mangapi luzio alikosa, jmaa kwangu sio striker wa kumkabidhi kazi ya kufunga akabisa, mechi ya juzi ilitakiwa na yeye awe na goli nne kama okwi lakini katika target nne sijui tano ambazo ni clean chances kapata moja, wakati okwi ametupia karibu zote... kama ni combination ya namna hiyo basi kama ni tairi za mbele za gari basi upande mmoja unatembelea mguu wa jini (a.k.a spare Tyre ).
 
mleta uzi hiv umeangalia ni magoli mangapi luzio alikosa, jmaa kwangu sio striker wa kumkabidhi kazi ya kufunga akabisa, mechi ya juzi ilitakiwa na yeye awe na goli nne kama okwi lakini katika target nne sijui tano ambazo ni clean chances kapata moja, wakati okwi ametupia karibu zote... kama ni combination ya namna hiyo basi kama ni tairi za mbele za gari basi upande mmoja unatembelea mguu wa jini (a.k.a spare Tyre ).

Tatizo sio magoli aliyokosa, ukimsoma vizuri Mayanja, amempongeza kwa sifa kuu 3

1. Kasi,
2. Nguvu
3. Mwepesi wa kufanya maamuzi

Hali hii ilimfanya awe target ya mabeki wa JKT Ruvu na wao kujikuta wakimwachia nafasi Okwi ambaye alizitumia vzr. Ila ni kweli Luizio anatakiwa aongeze kujiamini ili atumie nafasi vizuri japo yeye sio mfungaji mzuri miaka yote tangu nianze kumfuatilia akiwa Mtibwa
 
Luizao sioni umakini wake amekosa magoli mengi ya wazi Mayanja kasema maneno hayo sababu Simba imeshinda ila hajatengeneza pacha yoyote
 
Luizio jamaa anakosa sana magoli ya wazi
 
Naitaka kombinenga ya Okwi na Gyan,Luizio na Mavugo hamna kitu
Ndio, ila Gyan bado hatujamwona na kumthaminisha katika ligi yetu ya VPL.
Bado, Boko, Mavugo na Luizio kuwanoa ili mmoja wao asimame namba 9. Gyan namba yake ni 10 kwakuwa ana pumzi nzuri ya kuchukua mipira ya kugawa au kufunga mwenyewe.
Okwi anatokea 7 au 11.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom