Hawa ndiyo wachezaji vitasa wa Simba SC wanaostahili kupongezwa na kupigiwa makofi watakaposhuka uwanja wa ndege

Hawa ndiyo wachezaji vitasa wa Simba SC wanaostahili kupongezwa na kupigiwa makofi watakaposhuka uwanja wa ndege

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Bila kupepesa macho NALIA NGWENA naweka pembeni ushabiki wangu natoa ya rohoni nakuwapa maua wachezaji vitasa waliokipiga kwa kujitoa kwa asilimia moja.

Kwanza nimpongeze Mzamiru Yasin (kiungo punda) huyu ni mchezaji mzawa hakika dimba la Kati Ali haribu sana mipango ya waarabu/wydad kucheza mpira wao wa madoido, nguvu na akili kubwa hakika kiungo punda kafanya kazi yake Kama na kufanikiwa kwa asilimia moja.

Pili, maua yangu nampa beki mzawa namba tatu Mohammed Hussein (Tshabalala) kulikua kuna vita kubwa sana na namba saba wa Wyda Sufiane lakini the captain Mohammed Hussein kafanya kazi yake kisawasawa, hakika akishuka pale airport nitakuwa wa kwanza kupiga makofi mengi ku show respect to him.

Tatu, Shomari Kapombe (show me the way) marking skills yake huyu mwamba hakika ipo juu, huyu ni mzawa hakika mwamba kaitetendea haki namba yake. Achana na kukosa penati kwani penati ni bahati Kama bahati zingine huyu mwamba apewe maua yake kabla hajastaafu.

Nne, maua yangu namwaga kwa Sadio Kanout (The Putin) kazi kazi, nilipoona kaanza nili predict kadi nyekundu kutokana na uchezaji wake lakini mwamba kabisa kutoka Mali MTU kazi, sura kazi Hana muda wakucheka hakika mwamba apewe maua yake.

Tano, maua yangu nayamwaga kwa Kibu Denisi (Drogba wa Bongo) huyu jamaa kutokana na kasi aliyonayo na energy kubwa katika kuwasumbua mabeki hakika mabeki wa wydad hawata msahau huyu mwamba na hii ndiyo sababu ya kocha kumuanzisha Kibu na kumuweka benchi Pape Osumane Sakho, mwamba apewe maua yake.

Sita, Enonga (zee la masifa) Kuna muda alikua anacheza nafasi zote beki kupandisha mashambulizi kumsaidia onyango hapa kwa moyo wangu mkunjufu kabisa namwaga maua yote na makofi hakika he deserves congratulations za kutosha.

Saba na ya mwisho kwa kijana mdogo kabisa kinda Ally Salum naona huyu ni taifa la kesho kwa timu yetu ya taifa kafanya saves muhimu ambapo kasaidia Simba kutokuja na mzigo wa magoli kutokana na uchanga wake wa kimataifa kwa hiki alichokifanya hakika anastahili pongezi.

Kongolee kwa kocha Robertinho na benchi la ufundi kwa kumchezesha Chama Jr na Saidoo ntibazonkiza dakika tisini wakati walikua wamekwisha lowa mipira ilikua haifiki kwa Jean Baleke, mwisho wa siku na kuwa mzururaji uwanjani.
 
Mbona umenisahau Mimi anda twenti?
Screenshot_20230428-230613.jpg
 
Back
Top Bottom