Hawa Polisi wetu vipi? Mtakamata kabila zima?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
I'm sorry.. nadhani tuna tatizo kubwa zaidi kuliko tunavyofikiria..


Sawa..

Masanga was being held because he was the one who brought James Mabakuli (22) to Daraja's family to work as a houseboy.
wanamshirikia kwa kosa la kumrecommmend mtu kupata ajira? Wanamtuhumu kuhusika au kula njama? Lakini kumrecommend mtu? Gademu.. nani aliyemrecommend Mramba kuwa Waziri wa Fedha?


Masanga has also worked at the Daraja's residence before he left. He runs a video library shop at Kimara B.
Kuna mtu mwingine yoyote ambaye amewahi kufanya kazi kwa Daraja na anatafutwa?


The two are from the same tribe according to police.
So.. f....ing what!? mtaamua kuwasaka watu wote wenye kabila moja nao? au wote ni watu wa dini moja?


The houseboy was the only other person who was in the house with the deceased.
how on earth do you know that? Unless you know for a fact that there was no one else there!
 
Nafikiri Polisi inabidi wamuweke kolokoloni Jakaya Kikwete kwa sababu yeye ndiye alimpa kazi EL ya uwaziri mkuu akatuletea Richmond na Dowans. Na ndiye huyu huyu alimpa uwaziri Mramba pamoja na Chenge. Khe khe kheeeeeeeeee.
 
MKJJ natofautiana na wewe kidogo kuhusu kutokamatwa kwa waliomrecommend Mramba. Tofauti kwa Mramba ni kuwa yeye hajakimbia ila houseboy amekimbia.
 
Laiti polisi wetu wangekuwa wanatazama csi kama mimi...
 
Laiti polisi wetu wangekuwa wanatazama csi kama mimi...


Ha ha! What conclusions have you drawn so far using your CSI-acquired investigative skills?

Mimi napendekeza kwa wenzangu hapa JF, hasa kwa ambao wako nje ya nchi na mnatarajia kurudi nyumbani/ mna nyumba Tanzania, muwekeze katika kununua CCTV ndogo za nyumbani, wakati unaweka haumwambii mtu (hasa watoto wadogo kwa sababu huwa wanaelewana na wafanyakazi wa ndani na watasema), ikibidi kusema sema ni kifaa cha kugundua moshi kama moto ukiwaka.

CCTV pia zinapatikana Tanzania, hasa Dar, Arusha na Mwanza ila bei ni ghali kidogo ukilinganisha na bei unayoweza kununulia Magharibi/ Mashariki ya Kati, Mbali

Hii inasaidia sana hasa pale unapokua kazini muda mrefu na mfanyakazi anaweza fanya lolote ndani ya nyumba.
 
Sasa kama kamatakamata ndio dizaini hii basi wamkamate na mme wake maana ndie mtu wa mwisho kumwacha kwa sababu ya safari na wa kwanza kugundua mke wake ameuawa.
KWANZA NAZITANGULIZA SALAMU ZANGU ZA POLE KWA FAMILIA YA WAFIWA.
 
MKJJ natofautiana na wewe kidogo kuhusu kutokamatwa kwa waliomrecommend Mramba. Tofauti kwa Mramba ni kuwa yeye hajakimbia ila houseboy amekimbia.

So unasema kumkamat huyo bwana ni haki?

Laiti polisi wetu wangekuwa wanatazama csi kama mimi...

Common sense tu, ethics, police techniques, CSI watasema hawana yale makompyuta na zile maabara!

wanachofanya ni uvivu wa kufikiri na kushindwa kazi

Ukishindwa kazi, ili uonekane unafanya ndio unaanza hizo kamata kamata

Hatuna wapelelezi, hatuna ujuzi, hatuna lolote...

Very same case ukisema yaje mashirika toka nje, utaona watakavyo-idadavua

Tusisingizie teknolojia au maendeleo, Investigation/intelligence use more brains than tools!


Kwa hiyo kuanzia leo, watu tunaokuwa referee kwenye CV za watu, na tunaoomba udhamini from other people mchezo huo ufe!
 

kama walivurunda katika lile swala la jerry muro,je unategemea nini kwenye murder case na "mtuhumiwa" hajapatikana??uwezo wao mdogo hao polisi mi naamini kama una lawyers wazuri you'll get away with murder case even if they catch you ready handed with a smoking gun
 
Polisi wetu wasirudie makosa. Namshukuru Mbu kwa kutukumbusha kuhusu mwalimu aliyeuawa Arusha 2002, na mara moja Polisi wakaamua ni kijana wake wa kazi ndiye aliyeua. Hadi leo hawajampata huyo kijana, na inaelekea hawajaangalia uwezekano kwamba naye aliuawa na kufichwa ili kuwapumbaza Polisi.

Ni kosa, kwa sasa, kusema Mabakuri ndiye muuaji. Hatuwezi hata kusema ni mtuhumiwa, maana hakuna ushahidi hata kidogo. Hakuna ushahidi kwamba siku ya tukio waliokuweko nyumbani ni yeye na marehemu tu.

Kwa sasa Mabakuri anakuwa ni mshukiwa (person of interest). Wako washukiwa wengine vile vile.
 
Ndivyo hali ilivyo nyumbani. Akiguswa mkubwa basi atapatikana mtu wa kubebeshwa lawama hata kama hamna ushahidi wa maana wa kumhusisha. Kwa wenzetu huyu kijana angeitwa Person of Interest. Kwetu tayari ameisha hukumiwa, yeye pamoja na wote waliowahi kuwa na uhusiano nae. Wakati wakifanya hivyo wanasahau maelfu ya watu wanaouawa bila juhudi yeyote ya maana kufanywa kutafuta m/wahusika.

Amandla......
 
unajua inatisha sana; kwa sababu inaonekana hakuna mtu kwenye hii serikali ya magenius wetu anayefikiria kuwa yawezekana huyo kijana ni victim of foul play vile vile. Wakati huo huo huyo anayeshikiliwa inawezekana anapewa "enhanced interrogations techniques" ili kumfanya aseme Mabakuri anatoka wapi, na anaishi wapi na kama alikuwa na mawasiliano naye siku ya tukio.

Tayari tunajua the crime area was contaminated by Daraja and his driver and probably police kwani walipofika tu waliambiwa "mtumishi wa nyumbani hayupo".. and the story was carried verbatim..
 
Naona watu wanaichukua hii ishu na kui-blow out of context. Tuwaamini polisi at once wajameni. Wamesomea haya mambo. ebo!
 
MKJJ natofautiana na wewe kidogo kuhusu kutokamatwa kwa waliomrecommend Mramba. Tofauti kwa Mramba ni kuwa yeye hajakimbia ila houseboy amekimbia.

What about 'marehemu" Dr. Balali? manake naye alikuwa au ni 'fugitive'
 
hapo hapotu mie nakelekwa hivi why wakubwa wanakuwa hivo ila sisi kuku tu unakula mvua hama kweli umasikini wetu sasa unaelekea kubaya haya namuachia manani ndiye ajuae lakini hasa huyu mkuu anafanya nini au ndio kila kukicha root kwake haa hanahabari
aah amesahau msemo wa usimtoke kibanzi while ktk eye lako kuna nanihii
conquest:vijana tubadilike ubishoo wakupenda pesa watu hupewa na hurejesha ushoga.
 
Naona watu wanaichukua hii ishu na kui-blow out of context. Tuwaamini polisi at once wajameni. Wamesomea haya mambo. ebo!

yeah.. ndio maana miye napendekeza waseme kabila la huyo mtuhumiwa na aliyemrecommend ili watu wa kabila hilo wanaoishi maeneo hayo ya Kimara wawekwe kwenye kambi ya aina fulani..
 
Naona watu wanaichukua hii ishu na kui-blow out of context. Tuwaamini polisi at once wajameni. Wamesomea haya mambo. ebo!

Historia mzee, Historia: Tukiangalia historia mzee inatufanya tuchelee kuvumilia. Ya Mauaji ya Mzee Kombe Kule Arusha then Zombe etl . Give us a break. For your Info approval rate ya polisi natumaini hiko below zero.
 
nyie subirini tu.. mtasikia kuna mwili umeokotwa huko halafu polisi ndio waanze kutafuta "wauaji".. si unaona kama alivyokumbushia Shadow kwenye kesi ya Zombe.. magenius wetu wameenda hadi mahakamani .. mwisho wa siku wanaambiwa kamtafuteni aliyebonyeza "trigger"..

Kwenye suala la Mbatia ni hivyo hivyo..

Kwenye suala la Wangwe ni hivyo hivyo..

Tunawapa utaalamu wote humu ambao hauitaji wawekezaji badala yake wanatuona "wanajifanya wanajua sana!"..
 
Historia mzee, Historia: Tukiangalia historia mzee inatufanya tuchelee kuvumilia. Ya Mauaji ya Mzee Kombe Kule Arusha then Zombe etl . Give us a break. For your Info approval rate ya polisi natumaini hiko below zero.
Historia kwamba?

Tukio likitokea kazi ya polisi ni kuangalia viashiria na vidhibiti, motives etc etc. Na wana procedures zao, sasa labda mniambie kumdetain mtu ili kupta maelezo kuhusu tukio kunakiuka kitu gani au sheria gani, nitaanza kuwachukulia serious.
 
mkuu mie naenda cuba kujifunza ujeda then nije kuwatoa roho na wao waone maana sasa naona kama tutakuwa hat kushika kibastola ni wao tu basi tutakuwa tunakufa kama kuku kwa kweli mkuu inatia uchungu hebu tubadilike watz
Conquest
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…