Hawa vijana wanaovimba mtandaoni kwa maburungutu ya milioni 40 ni washamba wa pesa, Ili uvimbe kama don walau uringishie milioni 200

Au atoe ajira kwa watu mia mbili...
 
Umenikumbusha kuna siku nilizishika hizi ilinibidi nipige picha kabla ya kuzigeuza madafu
 
Sawa mkuu, nikizishika sitafanya hivyo maana najua nilipotoka.
 
Wewe kumbe hujui wanaume wa Dar kwenye swala la pesa ndio malimbukeni nambari 1 ,

Nilienda Njombe huko yani kijana unaambiwa ana ghorofa na anamiliki semi 5 yani ukimuona yuko poa sana halafu hata huwezi jua kuwa anapesa hiyo yote ni kama fala hivi
 
Aisee...
 
Wewe kumbe hujui wanaume wa Dar kwenye swala la pesa ndio malimbukeni nambari 1 ,

Nilienda Njombe huko yani kijana unaambiwa ana ghorofa na anamiliki semi 5 yani ukimuona yuko poa sana halafu hata huwezi jua kuwa anapesa hiyo yote ni kama fala hivi

Kule wanaogopa uchawi. Ukivimba sana wazee hawachelewi kukuchukua msukule
 
Ukivimbia milioni 250 pia wapo watakokwambia hiyo sio ya kuvimbia. Watasema uwe na angalau milioni 700. Ukiwa na hiyo pia kuna watu watakuona hautoshi kuvimba eti tafuta angalau bilioni 2. Kimsingi hata ukiamua kuvimba na 35,000 (elfu thelathini na tano) ni uamuzi wako.

Ni kama tu swala la magari. Unamvimbia asiye na gari kwa kuwa una Raum yako. Mtu mwenye Dualis anaiita baby walker. Halafu anakuja mtu mwenye Discovery anawaona wote hamna magari. Kwamba mna vyombo vya usafiri. Nae wanakuja wenye magari ya pesa nyingi zaidi wanamvimbia. Hata uwe na mafanikio kiasi gani kuna wengi waliokuzidi. Hata uwe masikini wa kiwango gani kuna masikini zaidi yako.

Kwa hiyo nadhani tuache watu wafanye wanayoyapenda kwenye social media. Akaunti yake, bando lake, simu ni yake na pesa ni zake. Akivimba kama hupendezwi scroll down endelea na content nyingine zinazokuvutia.
 
Dar es salaam mji wa kijinga sana , mtu unakuta una coaster 10 na hakuna anayekujua mtaani [emoji3][emoji3]
Jombaa, Thamani ya Coaster 10 mpya kwa kila moja labda weka Tshs. 80M yaani jumla Tshs. 800M ndio thamani ya nyumba za kuishi mitaa mingi ya watu wenye mifuko mipana kama vile Laiboni, Oyster Bay hapo sijaweka hata thamani ya ardhi. Unafikiri ukiishi maeneo kama haya kuna mtu hata anaweza kukufahamu?
 
hizo pesa nafikiri ni za demo, siyo halisi.

zinatengenezwa kwa ajili ya kuigizia, mfano kama zile za kwenye movie au miziki ya Kimarekani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…