Hawa Voda ni matapeli au?

Hawa Voda ni matapeli au?

Habari wakuu wa JF

Katika harakati za kujiunga nikawa napitia menu yao ya vifurushi, na kulingana na vocha nilionunua ya elfu moja a.k.a buku, nikawa nimependa kifurushi ambacho kwa elfu moja kulingana na menu yao ya vifurushi napewa MB 550, dakika 60 na sms 30.

Baada ya kujiunga kifurushi hicho nikaona niangalie salio sasa ile kucheki salio nakuta nimepewa MB 200, dakika 50 na sms 10 badala ya kupewa MB 550 dakika 60 na sms 30 hivi huu si utapeli kabisa tena kwa mtandao mkubwa kama vodacom

Nilichoamua laini yenu navunja, huwa sipendi ujinga mimi narudi zangu TTCL.
Screenshot tafadhali
 
Naona wameamua tena kunipa vocha ya elfu tano daah asanteni voda kwa wema wenu, wanaendelea kujichanganya tu
Kumbe wapo humu ukiwatolea povu wanakupoza na offer?
 
Back
Top Bottom