Hawa walazimishwe kugombea Uspika wa JMT

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Kama tunahitaji Maspika goigoi wa kuburuza wako wengi sana. Lakini kama tunahitaji Spika imara wa kuisimamia serikali kwa kumsaidia Rais kukamilisha kazi basi hawa walazimishwe kuchukuwa fomu kwa nguvu wapende wasipende:

1. Joseph Butiku



2. Kassim Majaliwa



3. Palamagamba Kabudi
(wazungu walilalamika kwamba aondolewe mambo ya nje kwa sababu kila akihutubia wazungu lazima watafute dictionary)



4. Mark Mwandosya



5. David Kafulila




Reserve:
1. Stephen Wassira (mtu na mpwa wake)

2. Bernard Membe



3. January Makamba



4. Fatma Karume



5. Makongoro Nyerere



6. Philip Mangula



7. Dr. Wilbroad Slaa



Taswira zote kwa hisani ya google.
 
Mangula ana mashamba ya nyanya huko kwao, ameyasahau muda mrefu, inabidi akayafufue, hao wengine wote hawafai
 
Yaani kweli unatuonaje sisi Watanzania wenzako.
Kisa nn hadi utuletee hivyo vizeee.

Hivi Mzee Butiku huwa ana kitu gani special ni mzee wa kawaida sana ana bebwa na jina la Mwalimu tu ila hana busara za kawaida tu kama wazee wengine wa kule Nanjilinji.

2.Fatma Karume ni aina ya wanaharakati ila sio viongozi wao kazi yao ni kuonyesha kuliko pinda ili viongozi warekebishe.

3.Prof Mwandosya ana busara nyingi ila umri umemtupa mkono hata Mzee Mangula, Wasira nk.
 
Mwandosya amekwisha amua kuishi bila stress huko kijijini kwake sidhani atakuwa radhi kurudi kwenye siasa za maji taka tena!!
 
isiwe taabu

Sheikh Ponda Isaa Ponda..
Askofu Mwamakula.
Askofu Bagonza.
Sheikh Rashidi Gwajima aka Gwaji boy
Mzee Mpili.
Mzee wa Upako.
Nabii Tito.
 
Natamani sana kumuona Prof.Kabudi akiwa waziri mkuu, toka nimeanza kumfuatilia sijutii kumsikiliza. Ikiwa Prof.Kabudi akawa ndiye nchi itasonga mbele kwa haraka sana. Ni MTU anaweza kujenga na kusimamia misingi

Kwenye uspika tukipata MTU kama Thobias Mwilapwa ,CCM na watanzania mtakuja kunishukuru baadae.

Katika hiyo list natamani Mzee Mangula awe ndie
 
bora wamteue spika wa bunge mwijaku au manara au babu tale au marioo au jokete hawa niliowataja ni wazuri sana watamsaidia sana rais
 
Wassira aliwahi kusema hazeeki akili bali mwili.

Natamani tungewajuwa mmoja baada ya mwingine kwa wasifu wao.
 
Em tutolee hizo list za hovyo.

Hiv kwanin usijitaje wew? Kama umeweza kuona uwezo wa hao watu uliowataja, basi ujue hata wew unao huo uwezo kuweza kushika nguzo na kukalia kiti cha uspika,

Acha uchawa fanya uwezalo nawew jina lako liwemo kati ya wanaoutaka uo uspika.

Kwanza taifa lina watu wengi sana ambao wanaweza shika usukani, na sio kila siku kuwashikilia watu ambao wameshachakaa ktk taifa,

nowadays tunahitaji mbegu mpya za viongoz wapya ambao wanajua shida za wananchi na watakwenda bungeni kubadiri upepo wa siasa za nchi na kuchachua kasi ya maendeleo.
 
Unajua wengine uliowataja wana miaka 100! Usione uso umepigwa scrab!
 
Mkuu, system inakujuwa?? Hata ungekuwa na uwezo kama wa Malaika kama system haikujui usihangaike kuota ndoto hizo mkuu. Hiyo ndiyo kanuni ya dunia hii.

Lkn kama huna uwezo ila system inakujuwa unaletewa uteuzi kitandani kwako.
 
Yaani mleta mada kweli umefulia, hadi akina Kafulila?

Umesahau majuzi tu Kafulila alifulia na kulia?
 
Unajua wengine uliowataja wana miaka 100! Usione uso umepigwa scrab!
Wanasiasa waliishagapitisha zamani msemo kwamba kwenye siasa ubongo haunaga makunyanzi (ubongo hauzeekagi)

Tuliambiwa Mkuchika ni Institutional Memory, yupo tangu enzi za Mwl. Sasa hivi hana wizara maalum lkn ni Waziri Ofisi ya Rais Ikulu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…