Hawa wanaharakati wa afya wasipodhibitiwa tutatengeneza kizazi goigoi

Hawa wanaharakati wa afya wasipodhibitiwa tutatengeneza kizazi goigoi

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Wakuu haihitaji research yoyote ya kisayansi kujua umuhimu wa kula. Pia haihitaji research kujua kuwa watanzania wengi hawapati chakula cha kutosha achilia mbali balanced diet. Yaani hata ugali maharage wa kushiba ni changamoto. Mimi nimeishi maeneo ya uswahilini Dsm nikaona mwenyewe jinsi watu wanashinda na njaa... kimsingi wanakula hawashibi. Vidonda vya tumbo ni sehemu ya maisha yao. Tatizo la lishe duni ni kubwa mno.

Serikali izuie hawa wataalamu feki wanaoeneza taharuki mitandaoni kwa kutamka karibu kila chakula kina madhara. Ugali, matunda, asali, chapati, wali, viazi, hata nyama choma zimetajwa kuwa hazifai. Wanaharakati wengine wameenda mbali zaidi kuwa kutaka watu wapuuze yote waliyofundishwa shuleni kuhusu vyakula. Wanadai tulidanganywa. Kuna mmoja anasema hakuna haja ya breakfast.

Hawa watu wasipodhibitiwa watazidi kuleta taharuki na wananchi kuwa dhaifu kwa kutokula vizuri. Tutakuwa taifa goigoi. Wizara ya afya itoe tamko kuhusu wenye uhalali wa kuongelea afya na mambo ya vyakula na sio kila mtu ajiamulie kisa ni fitness trainer.
 
Mwili hauchagui chakula gani unakula as long as unabalance kulingana na mahitaji yake ambayo ni matokeo ya life style yako.

Kuna watu wanakaa uswazi huko chipsi wanakula sana tu ila hawanenepi sababu ya life style yao inawaruhusu.

Kuna wamasai wanakula sana nyama mbona hawapati kansa inayosemwa inatokana na kula sana nyama nyekundu but madaktari ndio kutwa kuipigia kelele kuwa nyama nyekundu ni mbaya kwa mwili.

Kuna wazee wanakunywa beer na kuvuta tumbaku hadi wanafika miaka 90 au 100.

Nadhani elimu sahihi ni kuzingatia mahitaji ya mwili,life style yako na mazingira uliyopo ndipo useme hapa utafanya nini sio kusikiliza maneno ya kila mtu utavurugwa tafuta elimu sahihi.
 
Back
Top Bottom