Hawa wanaopanda katika Daladala na Kutuomba Msaada wanatufanya Sisi Abiria hatuna Akili au?

Hawa wanaopanda katika Daladala na Kutuomba Msaada wanatufanya Sisi Abiria hatuna Akili au?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kuna Mmoja kapanda Dala Dala nililopanda Jana Usiku la Buguruni - Mwenge aliniachi Maswali mengi sana.

Kwanza ana Afya nzuri ambayo hata GENTAMYCINE ninayeombwa Msaada sina.

Pili kuna muda akasema kuwa tayari ana Shilingi Milioni Saba na anataka tumchangie Shilingi Mia Tano, Elfu Moja zetu na tulizojaaliwa nazo ili akatibiwe nchini Uingereza.

Tatu na hapa ndipo si tu alinichanganya bali alinikera pia alikuwa anajielezea kwa ufasaha huku akitaja Ugonjwa wake Kisayansi / Kitabibu kabisa na Kujiamini Kwingi mpaka pale macho yangu Makali na yanayotisha yalipogongana nae akaomba Kondakta amshushe Kituo cha mbele huku akiiacha Hela aliyokuwa akipewa na Abiria wa Siti ya Nyuma.

Kwa wale wapanda Bayankata (Daladala) Wenzangu wa hiyo Route ya Buguruni hadi Ubungo River Side huenda huyu Mbaba mtakuwa mnamjua.

Kimwonekano na kwa Afya yake Njema nahisi ni Mhaya au Mnyakyusa na ana POP la Shingoni na ni Hodari wa Kutia Huruma, Kujionyesha anaumwa kweli kweli.

Akiona hakuna anayehangaika nae Kumpa Msaada anaanza Kuwahubirieni huku akiamka Kitini na kutembelea Siti zenu Abiria kwa mwendo wa Mgonjwa Mgonjwa ( wa Kiunyonge na Kiutaratibu ) ila akiona kuna Abiria anataka kumpa Pesa anabadili mwendo na kutembea vizuri na kwa Kasi ya 5G kabisa.

Leo GENTAMYCINE kwa Makusudi napita tena njia hiyo hiyo nikitoka Kushuhudia Marumo Gallants FC wakimfunga Mtu na nikikutana nae simkawizi Namchana makavu kwani kwa nilivyomsoma kwa Saikolojia yangu Kali ya Kuzaliwa nayo, ya Kimaono na ya Kusomea nimegundua kuwa Anatuokota / Anatudanganya tu.

ANGALIZO
Kwa Wewe KISOKOLOKWINYO ( MUWASHWAJI MUWASHWAJI ) na Mpumbavu ( Damn Fool ) unayejijua humpendi GENTAMYCINE na Mada zake / Uwasilishaji wake hapa JamiiForums tafadhali TUSICHOSHANE na acha kabisa Kusoma na hata Kuchangia bali Watafute Members wengine unaowaona ni Bora Kwako na Unawakubali kuliko Mimi.

Nimemaliza
 
Arusha yuko mmoja huwa anaomba hela ya chakula na anakufunulia shati uone operation yake kwa muda mref sana tang enzi hizo nikiwa kachalii had leo anabadilisha bus tu za njia ya Moshi na Babati Wataalam wa stand wanasema huwa ni muhuni tu ila mi sina uhakika

Kwangu binafsi mi naona yule jamaa ni kweli huwa anastahili kupewa msaada ila kwa muda alioomba kwa Sasa alitakiwa hata afanye biashara maana kasaidiwa na abiria wengi sana mwisho watu wameanza kumzoea hawampi msaada mkubwa kama ilivyo zamani
 
Visokolokwinyo vipo vingi sana, haviachi kutokwa povu pindi vionavyo nyuzi zako. Najua dawa yao unayo na huwa unawapa makavu ila hawakomi
 
Arusha yuko mmoja huwa anaomba hela ya chakula na anakufunulia shati uone operation yake kwa muda mref sana tang enzi hizo nikiwa kachalii had leo anabadilisha bus tu za njia ya Moshi na Babati Wataalam wa stand wanasema huwa ni muhuni tu ila mi sina uhakika...
Kuna mmoja nimempa alf 5 😀😀 mchana usiku nakutana nae bar amenisahau kabisa nikasema kenge huyu nilimdai Ile ela
 
Arusha yuko mmoja huwa anaomba hela ya chakula na anakufunulia shati uone operation yake kwa muda mref sana tang enzi hizo nikiwa kachalii had leo anabadilisha bus tu za njia ya Moshi na Babati Wataalam wa stand wanasema huwa ni muhuni tu ila mi sina uhakik...
Wa Jana anakuambia tayari ana Milioni Saba wakati GENTAMYCINE hata Shilingi Elfu 25 tu sina Muamalani au Mfukoni mwangu na anataka kwenda Kutibiwa nchini Uingereza na siyo India ambako tumezoea Masikini Wenzetu huwa wanaenda / wanapelekwa.

Leo kwa Makusudi napita hiyo njia mida ya Saa 1 au Saa 2 Usiku ili nimkute na Nimchane Live ( Mubashara ) wa Kutuokota / Kutudanganya Kwake.

Mgonjwa wa Shingo iliyowekewa POP anaweza Kuongea mambo ya Kidaktari / Kitabibu Kiufasaha kabisa, kuwa na Confidence na akiwa ni Wordsmith ( Mjuzi wa Kuongea Kiingereza ) vizuri vile.

Atakuwa ni Mhaya au Mnyakyusa yule.
 
Ombaomba wa Dar Wana vituko sana

Miaka ya nyuma Nilienda kumcheki mshkaji wangu Buguruni tukiwa tunapita karibu na mataa pale nikaona Mzee mmoja kiwete na kopo lake la kuombea nikampa jero, mwenyeji wangu akawa anacheka kinoma

Kufika mbele namuuliza kulikoni jamaa ananiambia huku anacheka " huyoo Mzee unamsaidia ila kakuzidi maisha, ana nyumba tatu za wapangaji, bajaji 2 na hua ana miziki yake anakodisha"

Dah nikasema kweli mjini akili
 
Kuna mmoja nimempa alf 5 😀😀 mchana usiku nakutana nae bar amenisahau kabisa nikasema kenge huyu nilimdai Ile ela
Mkuu yaani hapa nilipo baada ya Kusoma hii post yako Nimecheka hadi Watu wananishangaa.

JamiiForums raha sana hakyanani.
 
Hapo kwa Wanyakyusa na Wahaya kufanana na huyo ombaomba tapeli [emoji23] paache hivyo hivyo mkuu, usipa-edit! [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hapo kwa Wanyakyusa na Wahaya kufanana na huyo ombaomba tapeli [emoji23] paache hivyo hivyo mkuu, usije uka-edit! [emoji23][emoji23][emoji23]


Acha uchonganishi, unataka mwenzako apigwe za uso halafu uje kumcheka !!🤣🤣
 
Back
Top Bottom