Haya madaraja mapya kwa mitihani ya kidato cha nne: Kuboresha kiwango cha elimu inchi

kipenga

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
219
Reaction score
55
MADARAJA MAPYA KWA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE:
Serikali kwa kupitia wizara ya elimu imefanya mabadiliko kwenye madaraja ya alama za mitihani ya kidato cha nne. Hapo awali, madaraja yalikuwa ni kama ifuatavyo:

A = 81%-100%-
B = 61%-80%-
C = 41%-60%-
D = 21%-40%-
F = 0%-20%-

Mabadiliko mapya yamefanywa na sasa madaraja MAPYA ni kama ifuatavyo:

A = 80%-100%-
B = 65%-79%-
C = 50%-64%-
D = 35%-49%-
F = 0%-34%-

Taarifa imetolewa mapema ili wanafunzi kwa kidato cha nne waanze kujiandaa vyema na mitihani ijayo.

Nini Maoni yoke. . .
 
Duh itayofata sasa ni wachache kufaulu na wengi kufeli
 
Nadhani madalaja haya yalianza kutumika kabla hawajayatoa kwa umma.

Ndio maana vijana wengi wa mwaka jana hawakuweza kufanya vizuri.
 
Nadhani madalaja haya yalianza kutumika kabla hawajayatoa kwa umma.

Ndio maana vijana wengi wa mwaka jana hawakuweza kufanya vizuri.

masikini tanzania
Masikini taifa la kesho!
 
safi sana . Angalau wenye 80% nao watapata grade A badala ya grade B ya zamani. Haikuwa haki! Grades zingine pia ziko safi.
 
Reactions: SMU
safi sana . Angalau wenye 80% nao watapata grade A badala ya grade B ya zamani. Haikuwa haki! Grades zingine pia ziko safi.

Mkuu, hapo umekosea, jaribu kutetea majority ambao kiwango chao cha uelewa ni mdogo.

Hapo kwenye hizo grade za F na D
 
baadala ya kuanza kuboresha mazingira ya kufundishia ikiwemo kuwaongezea waalim mishahara, wanaongeza madaraja.....MASKINI WATANZNIA SISI!!!!
 
Mkuu, hapo umekosea, jaribu kutetea majority ambao kiwango chao cha uelewa ni mdogo.

Hapo kwenye hizo grade za F na D
Sijakosea boss. Kwa maoni yangu lengo la hizi grades ni kuwafanya wanafunzi wajitume-wasomena kwa bidii. sekondari siyo sehemu ya kukuzia vijana bali kusoma na kuelimika
 
baadala ya kuanza kuboresha mazingira ya kufundishia ikiwemo kuwaongezea waalim mishahara, wanaongeza madaraja.....MASKINI WATANZNIA SISI!!!!

Mkuu kwa hili tupo pamoja.
 
Sijakosea boss. Kwa maoni yangu lengo la hizi grades ni kuwafanya wanafunzi wajitume-wasomena kwa bidii. sekondari siyo sehemu ya kukuzia vijana bali kusoma na kuelimika

Unadhani kushuka kwa kufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne kunatokana na wao kutojituma pekee!?

Nakupandishwa kwa grade inamaana ya kutakuwa na kupanda kwa ufaulu wa wanafunzi hao?
 
Ni kweli elimu itaboreka, lakini sipendekezi hizi grade mpya zitumike kabisa. Itasababisha kuzalisha Great Failure, hakika idadi ya zeros itaongezeka.
Serikali iboreshe miundombinu ya kufundishia na kujifunzia kwanza.
 
Unadhani kushuka kwa kufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne kunatokana na wao kutojituma pekee!?

Nakupandishwa kwa grade inamaana ya kutakuwa na kupanda kwa ufaulu wa wanafunzi hao?
HUWEZI KUPANGA GRADES ZA UFAULU WA WANAFUNZI KWA VIGEZO VYA MIGOMO YA WALIMU, UKOSEFU AU UPUNGUFU WA WAALIMU, VIFAA VYA KUFUNDISHIA, i.e MATATIZO YANAYOISIBU wizara YA ELIMU ETC . GRADES ZINATAKIWA ZI-REFLECT UELEWA WA WANAFUNZI KATIKA NGAZI HUSIKA- IRRESPECTIVES OF THE PREVAILING PROBLEMS FACING THE EDUCATION SYSTEM. KWAMBA GRADES ZIPANGUZWE/ZISHUSHWE KWA SABABU KUNA MATATIZO KWENYE WIZARA YA ELIMU IS RIDICULOUS
 
Sasa inabidi wajee na solution ya kujaza nafasi za wanafunzi wapya wa kidato cha 5 maana idadi inaonesha wazi kuwa ni wachache sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…