Zemanda
JF-Expert Member
- Jan 10, 2021
- 8,323
- 18,051
Natumai nyote muwazima wa afya ya akili na mwili. Leo napenda kuweka sawa matumizi sahihi ya majina haya haya ambayo yamekuwa yakitumika visivyo kuwakilisha rika na jinsia ya kundi husika la watu.
Kama kweli lugha ya malkia yaani English, kuna majina huitwa collective nouns ambayo hutumika kwa kundi bila kubagua tofauti zake. Mfano ukisema children unakuwa umelenga group la watoto bila kusema umri, rangi, jinsia au tofauti zao zingine. Halafu kuna specific nouns ambazo hutumika kulenga specific group ya watu mfano ukisema "one month african baby boys" hapo unakuwa very specific.
Sasa naomba turudi kwenye hoja yangu ambayo imebidi kuiandikia uzi leo baada ya kuona kuna upotofu kama sio mkanganyiko katika matumizi sahihi. Kumekuwa na mkanganyiko wa kimatumizi kwenye jina Kijana. Neno kijana nimeona likitumika kinyume miongoni mwa wana taaluma, viongozi na taasisi kumaanisha mtu wa umri mdogo jambo ambalo ni sahihi kwa upande m'moja ila sio sahihi kwa upande mwingine.
Ni sahihi kwasababu ni kweli kijana ni mtu wa umri mdogo katikati ya mtoto na mtu mzima. Lakini si sahihi kumwita mtu umri mdogo wa jinsia ya kike kijana sababu sio jinsia yake. Mtu wa umri mdogo wa jinsia ya kike huitwa binti.
Sasa leo nikaona niweke kumbukumbu sawa na kurekebisha huu upotofu ambao hata hawa watu wa serikalini na viongozi wengi wamefeli kurekebisha ili kuweka sawa matumizi ya misamiati ya lugha yetu ya taifa.
1. Katika kundi na watu waliopo umri kuanzia miaka 0 hadi 17, jinsia ya kiume huitwa MVULANA na jinsia ya kike huitwa MSICHANA. Hii ni kwa mujibu wa standards za kimataifa ila huwa tofauti kulingana na tamaduni tofauti.
Kwa mfano kwa standards za kimataifa mtu nzima huanzia miaka 18 kwenda juu ila ukija afrika ni tofauti, mtu wa kike akivunja ungo tu kwa maana kuona hedhi yake ya kwanza papo hapo hiyo uchukuliwa kuwa ni ameshaingia utu uzima na si MSICHANA tena bali ni binti. Na mtu wa kiume akishaanza kuonyesha dalili za kupevuka au balehe then huyo huchukuliwa ni mtu mzima na si MVULANA tena bali ni Kijana.
2. Katika kundi la watu kuanzia umri kuanzia miaka 18 hadi 35, jinsia ya kiume huitwa KIJANA na jinsia kike huitwa BINTI. Hii ni kwa mujibu wa standards za kimataifa ila huwa tofauti kulingana na tamaduni tofauti.
Kwa mfano kwa tamaduni za mataifa mengi ukitoa mataifa ya kimagharibi kama US, UK, Canada etc, kwa sisi Africa, Asia, Arabic huwa vijana na mabinti wanaooa na kuolewa katikati ya umri huu huondoka katika kundi hili la vijana na mabinti na kuwa mtu mume mtu mke yaani wanaume na wanawake.
So kwa mfano unaweza kuta mtu amefika miaka 35 hajaolewa wala kuoa huyu hawezi endelea kuitwa kijana au binti bali ataitwa mwanaume au mwanamke basi. Ila kama katika umri huo umemkuta ameoa au kuolewa title yake itakuwa Bwana na bibi. Yaani bwana fulani au bibi fulani.(bibi haimaanishi umezeeka maana watu mtashtuka hapa[emoji23][emoji23])
So ukitazama hadi hapo utaona kuna mtiririko huu ufuatao.
Umri 0 hadi 17 = MVULANA/MSICHANA
Umri 18 hadi 34 = KIJANA/BINTI (kwa wasio ndani ya ndoa)
Umri 35 hadi 55 kuendelea = Bwana /Bibi
Natumai hadi hapa nimeweka rekodi sawa na kuondoa utata wa matumizi ya haya majina. Lakini pia kuna majina mengine ambayo hutumika kama status mfano mume na mke. Hawa ni wanandoa. Ila sio wahuni wawili wanaishi pamoja wajiite mume na mke hao ni kijana na binti mwamflani.
Anyways, nakaribisha maswali kwa ufafanuzi zaidi.
Kama kweli lugha ya malkia yaani English, kuna majina huitwa collective nouns ambayo hutumika kwa kundi bila kubagua tofauti zake. Mfano ukisema children unakuwa umelenga group la watoto bila kusema umri, rangi, jinsia au tofauti zao zingine. Halafu kuna specific nouns ambazo hutumika kulenga specific group ya watu mfano ukisema "one month african baby boys" hapo unakuwa very specific.
Sasa naomba turudi kwenye hoja yangu ambayo imebidi kuiandikia uzi leo baada ya kuona kuna upotofu kama sio mkanganyiko katika matumizi sahihi. Kumekuwa na mkanganyiko wa kimatumizi kwenye jina Kijana. Neno kijana nimeona likitumika kinyume miongoni mwa wana taaluma, viongozi na taasisi kumaanisha mtu wa umri mdogo jambo ambalo ni sahihi kwa upande m'moja ila sio sahihi kwa upande mwingine.
Ni sahihi kwasababu ni kweli kijana ni mtu wa umri mdogo katikati ya mtoto na mtu mzima. Lakini si sahihi kumwita mtu umri mdogo wa jinsia ya kike kijana sababu sio jinsia yake. Mtu wa umri mdogo wa jinsia ya kike huitwa binti.
Sasa leo nikaona niweke kumbukumbu sawa na kurekebisha huu upotofu ambao hata hawa watu wa serikalini na viongozi wengi wamefeli kurekebisha ili kuweka sawa matumizi ya misamiati ya lugha yetu ya taifa.
1. Katika kundi na watu waliopo umri kuanzia miaka 0 hadi 17, jinsia ya kiume huitwa MVULANA na jinsia ya kike huitwa MSICHANA. Hii ni kwa mujibu wa standards za kimataifa ila huwa tofauti kulingana na tamaduni tofauti.
Kwa mfano kwa standards za kimataifa mtu nzima huanzia miaka 18 kwenda juu ila ukija afrika ni tofauti, mtu wa kike akivunja ungo tu kwa maana kuona hedhi yake ya kwanza papo hapo hiyo uchukuliwa kuwa ni ameshaingia utu uzima na si MSICHANA tena bali ni binti. Na mtu wa kiume akishaanza kuonyesha dalili za kupevuka au balehe then huyo huchukuliwa ni mtu mzima na si MVULANA tena bali ni Kijana.
2. Katika kundi la watu kuanzia umri kuanzia miaka 18 hadi 35, jinsia ya kiume huitwa KIJANA na jinsia kike huitwa BINTI. Hii ni kwa mujibu wa standards za kimataifa ila huwa tofauti kulingana na tamaduni tofauti.
Kwa mfano kwa tamaduni za mataifa mengi ukitoa mataifa ya kimagharibi kama US, UK, Canada etc, kwa sisi Africa, Asia, Arabic huwa vijana na mabinti wanaooa na kuolewa katikati ya umri huu huondoka katika kundi hili la vijana na mabinti na kuwa mtu mume mtu mke yaani wanaume na wanawake.
So kwa mfano unaweza kuta mtu amefika miaka 35 hajaolewa wala kuoa huyu hawezi endelea kuitwa kijana au binti bali ataitwa mwanaume au mwanamke basi. Ila kama katika umri huo umemkuta ameoa au kuolewa title yake itakuwa Bwana na bibi. Yaani bwana fulani au bibi fulani.(bibi haimaanishi umezeeka maana watu mtashtuka hapa[emoji23][emoji23])
So ukitazama hadi hapo utaona kuna mtiririko huu ufuatao.
Umri 0 hadi 17 = MVULANA/MSICHANA
Umri 18 hadi 34 = KIJANA/BINTI (kwa wasio ndani ya ndoa)
Umri 35 hadi 55 kuendelea = Bwana /Bibi
Natumai hadi hapa nimeweka rekodi sawa na kuondoa utata wa matumizi ya haya majina. Lakini pia kuna majina mengine ambayo hutumika kama status mfano mume na mke. Hawa ni wanandoa. Ila sio wahuni wawili wanaishi pamoja wajiite mume na mke hao ni kijana na binti mwamflani.
Anyways, nakaribisha maswali kwa ufafanuzi zaidi.