Haya majina huwa yanatumika visivyo sana

Haya majina huwa yanatumika visivyo sana

Zemanda

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2021
Posts
8,323
Reaction score
18,051
Natumai nyote muwazima wa afya ya akili na mwili. Leo napenda kuweka sawa matumizi sahihi ya majina haya haya ambayo yamekuwa yakitumika visivyo kuwakilisha rika na jinsia ya kundi husika la watu.

Kama kweli lugha ya malkia yaani English, kuna majina huitwa collective nouns ambayo hutumika kwa kundi bila kubagua tofauti zake. Mfano ukisema children unakuwa umelenga group la watoto bila kusema umri, rangi, jinsia au tofauti zao zingine. Halafu kuna specific nouns ambazo hutumika kulenga specific group ya watu mfano ukisema "one month african baby boys" hapo unakuwa very specific.

Sasa naomba turudi kwenye hoja yangu ambayo imebidi kuiandikia uzi leo baada ya kuona kuna upotofu kama sio mkanganyiko katika matumizi sahihi. Kumekuwa na mkanganyiko wa kimatumizi kwenye jina Kijana. Neno kijana nimeona likitumika kinyume miongoni mwa wana taaluma, viongozi na taasisi kumaanisha mtu wa umri mdogo jambo ambalo ni sahihi kwa upande m'moja ila sio sahihi kwa upande mwingine.

Ni sahihi kwasababu ni kweli kijana ni mtu wa umri mdogo katikati ya mtoto na mtu mzima. Lakini si sahihi kumwita mtu umri mdogo wa jinsia ya kike kijana sababu sio jinsia yake. Mtu wa umri mdogo wa jinsia ya kike huitwa binti.

Sasa leo nikaona niweke kumbukumbu sawa na kurekebisha huu upotofu ambao hata hawa watu wa serikalini na viongozi wengi wamefeli kurekebisha ili kuweka sawa matumizi ya misamiati ya lugha yetu ya taifa.

1. Katika kundi na watu waliopo umri kuanzia miaka 0 hadi 17, jinsia ya kiume huitwa MVULANA na jinsia ya kike huitwa MSICHANA. Hii ni kwa mujibu wa standards za kimataifa ila huwa tofauti kulingana na tamaduni tofauti.

Kwa mfano kwa standards za kimataifa mtu nzima huanzia miaka 18 kwenda juu ila ukija afrika ni tofauti, mtu wa kike akivunja ungo tu kwa maana kuona hedhi yake ya kwanza papo hapo hiyo uchukuliwa kuwa ni ameshaingia utu uzima na si MSICHANA tena bali ni binti. Na mtu wa kiume akishaanza kuonyesha dalili za kupevuka au balehe then huyo huchukuliwa ni mtu mzima na si MVULANA tena bali ni Kijana.

2. Katika kundi la watu kuanzia umri kuanzia miaka 18 hadi 35, jinsia ya kiume huitwa KIJANA na jinsia kike huitwa BINTI. Hii ni kwa mujibu wa standards za kimataifa ila huwa tofauti kulingana na tamaduni tofauti.

Kwa mfano kwa tamaduni za mataifa mengi ukitoa mataifa ya kimagharibi kama US, UK, Canada etc, kwa sisi Africa, Asia, Arabic huwa vijana na mabinti wanaooa na kuolewa katikati ya umri huu huondoka katika kundi hili la vijana na mabinti na kuwa mtu mume mtu mke yaani wanaume na wanawake.

So kwa mfano unaweza kuta mtu amefika miaka 35 hajaolewa wala kuoa huyu hawezi endelea kuitwa kijana au binti bali ataitwa mwanaume au mwanamke basi. Ila kama katika umri huo umemkuta ameoa au kuolewa title yake itakuwa Bwana na bibi. Yaani bwana fulani au bibi fulani.(bibi haimaanishi umezeeka maana watu mtashtuka hapa[emoji23][emoji23])


So ukitazama hadi hapo utaona kuna mtiririko huu ufuatao.

Umri 0 hadi 17 = MVULANA/MSICHANA
Umri 18 hadi 34 = KIJANA/BINTI (kwa wasio ndani ya ndoa)
Umri 35 hadi 55 kuendelea = Bwana /Bibi

Natumai hadi hapa nimeweka rekodi sawa na kuondoa utata wa matumizi ya haya majina. Lakini pia kuna majina mengine ambayo hutumika kama status mfano mume na mke. Hawa ni wanandoa. Ila sio wahuni wawili wanaishi pamoja wajiite mume na mke hao ni kijana na binti mwamflani.

Anyways, nakaribisha maswali kwa ufafanuzi zaidi.
 
Neno kijana linatumika kwa jinsi zote mbili, wavulana na wasichana.

Lakini neno binti hutumika kwa jinsi moja tu ya kike ambapo inaweza kutumika katika mukhtadha mitatu:-

1. Msichana au mwanamke mdogo.

2. Kutumiwa kwa "mtoto wa fulani"

Mfan. Ukisema binti Burhani = mtoto wa Burhani.

3. Kutumia kwa heshima na upendo kumwita msichana au mwanamke aghalabu ambaye bado hajaolewa lakini ukiwa umemzidi umri.
 
Neno kijana linatumika kwa jinsi zote mbili, wavulana na wasichana.

Lakini neno binti hutumika kwa jinsi moja tu ya kike ambapo inaweza kutumika katika mukhtadha mitatu:-

1. Msichana au mwanamke mdogo.

2. Kutumiwa kwa "mtoto wa fulani"

Mfan. Ukisema binti Burhani = mtoto wa Burhani.

3. Kutumia kwa heshima na upendo kumwita msichana au mwanamke aghalabu ambaye bado hajaolewa lakini ukiwa umemzidi umri.
Ndio maana nikaleta huu uzi ili ujifunze na kuwaelimisha wengine. Mimi pia nilikuwa nakosea kama wewe na wengine. Na hizi lawama ziwaendee balaza la kiswahili wataalamu wake wamekaa kimya na hawatoi marekebisho ya lugha ili maneno yatumike kiusahihi.

Neno kijana nenda hata kwenye bible hakuna sehemu utaona kijana limetumika kwa mwanamke. Ila limetumika kuelezea maisha ya mtu wa kiume wa umri mdogo. Ila kijana. Humaanisha mtu mwanaume wa umri mdogo.

Nikuulize tu swali simpo hapa ambalo utafeli. Kinyume cha binti ni nini?!

Msichana nimeshaweka pale tafsiri yake, kinyume cha msichana ni mvulana.

Katika kiswahili huwezi ita mwanamke mdogo ukaita hilo ni jina. Hilo sio jina. Umeunda sentence. Hiyo ni sifa, kwahiyo mwanamke mdogo kwa minajiri ipi, mdogo kwa cheo, umri, umbile, au kivipi?!

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Ndio maana nikaleta huu uzi ili ujifunze na kuwaelimisha wengine. Mimi pia nilikuwa nakosea kama wewe na wengine. Na hizi lawama ziwaendee balaza la kiswahili wataalamu wake wamekaa kimya na hawatoi marekebisho ya lugha ili maneno yatumike kiusahihi.

Neno kijana nenda hata kwenye bible hakuna sehemu utaona kijana limetumika kwa mwanamke. Ila limetumika kuelezea maisha ya mtu wa kiume wa umri mdogo. Ila kijana. Humaanisha mtu mwanaume wa umri mdogo.

Nikuulize tu swali simpo hapa ambalo utafeli. Kinyume cha binti ni nini?!

Msichana nimeshaweka pale tafsiri yake, kinyume cha msichana ni mvulana.

Katika kiswahili huwezi ita mwanamke mdogo ukaita hilo ni jina. Hilo sio jina. Umeunda sentence. Hiyo ni sifa, kwahiyo mwanamke mdogo kwa minajiri ipi, mdogo kwa cheo, umri, umbile, au kivipi?!

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Kinyume cha binti kwa namna moja inaweza kuwa BIN (IBN) kwa ile maana moja ya binti kwamba ni 'mtoto wa kike wa... '


Mfano

Hamida binti Burhani

Jamaal bin Jason
 
Kinyume cha binti kwa namna moja inaweza kuwa BIN (IBN) kwa ile maana moja ya binti kwamba ni 'mtoto wa kike wa... '


Mfano

Hamida binti Burhani

Jamaal bin Jason
Na ndio maana nikaanzisha huu uzi tuweze kujiuliza jina collective la kuwaita Vijana na mabinti tunawaitaje? Ila sio kusema Vijana ni collective name ya wanawake na wanaume wa rika fulani.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Na ndio maana nikaanzisha huu uzi tuweze kujiuliza jina collective la kuwaita Vijana na mabinti tunawaitaje? Ila sio kusema Vijana ni collective name ya wanawake na wanaume wa rika fulani.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Vijana tayari imejumuisha walulana na wasichana.
 
Wewe umesoma nilichokiandika hapo. Yaani ni kama umeuliza kwan Baiskeli haiwezi kuwa bodaboda?!

Vitu viwili tofauti.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Kijana maana yake ni nini na binti maana yake ni nini?

Unaelewa kwamba kijana haiishii kwenye jinsia ya kiume, kijana ni hali ya mtu aliye katika umri fulani, ndiyo maana hata umoja wa vijana wa CCM, CHADEMA etc una vijana wa kiume na kike?

Unajua kwamba kuna vijana wa kiume na kike?

Unaelewa kwamba kuna binti ambao ni vijana na hivyo vijana si wa kiume tu?
 
Vijana tayari imejumuisha walulana na wasichana.
Dah ila wewe ni mzito kuelewa hebu nenda kasome tena kule nimeweka hadi age range kabisa. Wewe tena unakuja kuvuruga mada. Hivi umesoma nilichoakiandika kweli?

Huo utata ndio nimeuzungumzia kule juu.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Dah ila wewe ni mzito kuelewa hebu nenda kasome tena kule nimeweka hadi age range kabisa. Wewe tena unakuja kuvuruga mada. Hivi umesoma nilichoakiandika kweli?

Huo utata ndio nimeuzungumzia kule juu.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Ushahidi wa maelezo yako unayosema umeweka umejifunzia wapi? Au umeyatoa wapi?

Neno KIJANA ni kwa jinsi zote mbili, jinsi ya kike na jinsi ya kiume.

Binti nimeeleza maana yake na mukhtadha mitatu ambayo neno hilo linaweza kutumika.

Ugumu wangu kuelewa uko wapi?
 
Kijana maana yake ni nini na binti maana yake ni nini?

Unaelewa kwamba kijana haiishii kwenye jinsia ya kiume, kijana ni hali ya mtu aliye katika umri fulani, ndiyo maana hata umoja wa vijana wa CCM, CHADEMA etc una vijana wa kiume na kike?

Unajua kwamba kuna vijana wa kiume na kike?

Unaelewa kwamba kuna binti ambao ni vijana na hivyo vijana si wa kiume tu?
Dah, ama kweli elimu yetu inahitaji kufumuliwa na kurekebishwa ili tusiwe na wahitimu ambao hawana uwezo wa kuchambua mambo na kuyarekebisha.

Wewe unaonekana hata darasani ulikuwa unameza tu definitions na haukuwa na uwezo wa kutengeneza definition yako kamili.

Nime elezea vizuri kabisa kule juu labda kama hauelewi na hauna uwezo wa kusoma kiswahili vema.

Nimesema vema kule juu kuwa Unaposema Kijana unakuwa unamuongelea mwanaume wa rika la umri ambao nimeelekeza pale juu.

Kimsingi, jamii inatabia ya kutumia maneno kwa mapokeo. Ukienda hata kwenye vitabu vinamwita mwanadamu MAN. kwasababu kihistoria mwanadamu aliyeumbwa ni Mwanaume na mwanamke alitengenezwa kama ubavu wa huyo mwanaume so mwanamke huwa hachukuliwi kama mwanadamu kamili kimaagano.

Sasa ukija katika rekodi za mapokeo ni kuwa wanaume wa umri mdogo yaani vijana ndio wamekuwa wakitumika katika platforms mbali mbali za kisiasa, kiuchumi, kisayansi na mengineyo. Miaka hii mabinti nao wameanza kuingia ila wanakuta documents zote zinatumia neno vijana kumaanisha washiriki wa umri chini ya watu wazima.

Sasa imekuwa adopted hivyo hivyo ila mimi nataka tupate kupeana elimu kuwa documents zinabidi kusoma vijana na mabinti kama vile zinavyosema wanaume na wanawake.

Ndio maana hata ukienda katika medani ya mashujaa utaona siku hizi kuna neno Sheroes limeongezwa kwa maana ya mashujaa wakike ambapo zamani lilitumika neno Heroes sasa wanawake wanaona hili neno kwao haliwatambulishi vema.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom