Haya ndio huwa yanafanyika hata wakati wa uchaguzi ili kupoteza watu kwenye jambo husika, tujifunze kuhakiki taarifa

Haya ndio huwa yanafanyika hata wakati wa uchaguzi ili kupoteza watu kwenye jambo husika, tujifunze kuhakiki taarifa

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Naimani mlikutana na mabango haya yanayoelezea vingozi wa CHADEMA kufanya mkutano na waandishi wa habari, moja likiwa sahihi na mawili yakiwa ya uongo kuwapoteza watu na kuwagawanya wasifuatilie nini kinataka kusemwa na mtu sahihi.

Mbinu ni hizi hizi hata kipindi cha uchaguzi, utakuta matokeo hayajatoka lakini kuna watu washatoa matokeo yao, unakuna mgombea kasema hiki lakini inatengezwa bango ikionesha account yenye mpaka kitiki juu kuwa yeye ndio kasema maneno fulani na post inasambazwa kama njugu.

Tuwe makini hasa katika kipindi hiki ambako kila mtu anachafua mtu na kusafisha pa kwake, taarifa potofu ni nyingi, tujifunze kufanya uhakiki, na ukishindwa kabisa peleka JamiiCheck wafanyie mafekeche na kuhakikisha una taarifa sahihi wakati wote.

heche.jpg
lissuu.jpg
GVg1WpEXQAAJQaP.jpeg
 
Simbayanga mmeletewa wafadhili 😄
Mnaambiwa mtaletewa zaidi mafestivo pia

Ova
 
Back
Top Bottom