Haya ndio matokeo ya mwanangu darasa la saba nimefarijika sana

Haya ndio matokeo ya mwanangu darasa la saba nimefarijika sana

Kiswahili - A,
English - A,
Maarifa - B,
Hisabati - A,
Science - A,
Uraia - B,

Average Grade - A

Amemaliza katika shule ya English medium

Mimi baba yake ni kichwa zaidi yake ila matokeo yangu hayakuwa mazuri Kwa sababu ya hali ya maisha magumu ya familia yangu

Ni kama vile nilikuwa najisomesha mwenyewe maana sare za shule na viatu nilivyo nunuliwa na wazazi ni zile nilizovaa siku napelekwa kuanza darasa la kwanza Baada ya hapo nilijinunulia mwenyewe Kila kitu hadi namaliza darasa la saba

Huko secondary na advance ndio kabisa nilikuwa nauza maji Ili kupata naurli ya shule na mahitaji mengine ada zote nimelipa Baada ya kumaliza advance ndio nakachukua vyeti vyangu ada ilikuwa elfu 20 Kwa mwaka lakini bado familia yangu ilishindwa kulipa

Ila bumu la chuo ndio lilinifariji na kunifanya nisome chuo bila ya stress

Ila elimu niliyoipata sio elimu Bora naamini hilo 100% Yani nilikuwa nafaulu tu Kwa sababu Nina akili nyingi

Nikajiapiza watoto wangu sitaki wapitie haya na sitaki wasome kayumba kama Mimi baba yao
Hongera sn kwake,jitahidi kuzidisha dua maana dunia ya sasa hivi imejaa changamoto
 
Kiswahili - A,
English - A,
Maarifa - B,
Hisabati - A,
Science - A,
Uraia - B,

Average Grade - A

Amemaliza katika shule ya English medium

Mimi baba yake ni kichwa zaidi yake ila matokeo yangu hayakuwa mazuri Kwa sababu ya hali ya maisha magumu ya familia yangu

Ni kama vile nilikuwa najisomesha mwenyewe maana sare za shule na viatu nilivyo nunuliwa na wazazi ni zile nilizovaa siku napelekwa kuanza darasa la kwanza Baada ya hapo nilijinunulia mwenyewe Kila kitu hadi namaliza darasa la saba

Huko secondary na advance ndio kabisa nilikuwa nauza maji Ili kupata naurli ya shule na mahitaji mengine ada zote nimelipa Baada ya kumaliza advance ndio nakachukua vyeti vyangu ada ilikuwa elfu 20 Kwa mwaka lakini bado familia yangu ilishindwa kulipa

Ila bumu la chuo ndio lilinifariji na kunifanya nisome chuo bila ya stress

Ila elimu niliyoipata sio elimu Bora naamini hilo 100% Yani nilikuwa nafaulu tu Kwa sababu Nina akili nyingi

Nikajiapiza watoto wangu sitaki wapitie haya na sitaki wasome kayumba kama Mimi baba yao
Na asome hadi awe Profesa; katika jina la Yesu!
 
Wenzio wanaonesha kama hayo lakini ya kidato cha nne. Mwanao bado yuko mbali, si pa kumsifia hapo.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Mimi sijamsifia hata haya matokeo hajui kama Mimi nimeyaona maana sijamwambia chochote aliangalia akiwa na mama yake na mama yake ameniambia yeye mwenyewe alivyoyaona matokeo yake alifurahi sana

Ila pia Mimi kama Mimi nimefarijika na nilishamtafutia shule Moja ya Masister kabla hata matokea hayajatoka
 
Hahaaaa, mi nilimchukua ntoto wa ndugu yangu. Mazingira aliyokuwa anaishi hayakuwa mazuri kwani alikuwa kama "chokoraa" nikasema nimbadikishie mazingira na nimsomeahe English Medium. Akawa anatoka Getini anapanda school bus au siku nyingine nawapeleka kwani shule anayosoma ipo karibia na kazini kwangu.

Toka aanze la kwanzwa yeye ni wa mwisho tu kati ya watoto 12. Hajawahi kutoka mwisho. Mtihani wa La nne akawa wa Mwisho na C yake. Nikaona hapa napoteza pesa yangu. Nikataka nimpeleke st Kayumba ila nikaofia Maneno ya watu na ndugu kwani wanangu walikiwa wanasoma naye. Jamaa hataki kusoma, hafanyi homework hadi nimuulize na ananidanganya. Nikawa naitwa shuleni kujieleza. Kwanini wangu wanafanya ila.yeye hafanyi. Dogo akawa ananigombanisha na walimu
Katika.jaribu nililolipata ni dofo. Jamaa kamaliza la saba wenzie wamepata A&B tu yeye kapata C
Kavuta mkia tena kati ya watu 12. Walimu wamepambana naye sana ila hajasaidika jamaa yangu. Homework nilikuwa nafanya mimi na kama nimesafiri kikazi hafanyi au hamalizi au anajijazia tu hata ukimwambia asome alichoandika hawezi kwani anaogopa kuchapwa shuleni. Hata akiwa na maswali 60, itanidi nikomae usiku mengine tufanye wote asubuni. "Holiday package" ya Darasa la Saba alikuwa na maswali 1800, dingi la mishe ikabidi nikomae nayo kwani mjuba hana huo muda. Shuleni nalaumiwa mzazi kama hajamaliza "leave package" Jamaa kamaliza ila hata umwambie aandike Jina lake anachanganya small and capital letter. Alipomaliza tu, nimempeleka kwa Baba yake. Naye akomae naye. So wapo wanaoscore C huku English Medium Schools.
Huyo ni kilaza pro max.
 
Hongera kwa jitihada...na kwa dogo pia. Lakini kubali tu mtoto amekuzidi akili na iwe fahari kwako sio wivu
 
Mama ana influence kubwa sana kwenye ubongo wa mtoto na intelligence yake na si baba , kwa kiswahili kisicho fasaha ni kwamba mtoto anarithi akili ya mama na si baba .
Mke wangu akili yake ni ya kuungaunga lakini nikicheki akili ya watoto wetu wako vizuri
 
Yangekua ya form four ningekusifu umepambana ila haya ya dalasa la saba ambayo hayana maana yyte
 
Hayo mabanda si kitu kama elimu haina global qualities na mbaya zaidi hayo mabanda yananunulika.tunachotakiwa kujivunia ni quality ya elimu na si quatinty. Kuna haja gani ya kupata la saba A, form four I. 7,form six I. 3 na university GPA ya 4.8 au 5 lakin baada ya yote hayo, mtu anakosa cha kufanya na kuishia kulalamika.
 
Back
Top Bottom