Haya ndiyo niliyoyaona nje na ndani ya uwanja kwenye mchezo wa Yanga vs Azam FC

Haya ndiyo niliyoyaona nje na ndani ya uwanja kwenye mchezo wa Yanga vs Azam FC

(1) Mudathri na Feisal salum walitegeana kuingia uwanjani hii ilishatokea kwa Aziz k na Chama kutopeana mikono.

(2) Vita Kali katikati ya uwanja baina ya viungo wakabaji Aucho, Mudathri na Akaminko, Bajana hakika Moto uliwaka kweli kweli kijana toka Zanzibar Mudathiri alitepeta na kufichwa na kocha aliona Bora amnusuru baada ya kuona kijana kapata kadi ya njano.

Bajana ni Moto hakika ni mwamba kweli kweli Akaminko akiicha lafu zake na kukamia namuona ni moja Kati ya kiungo Bora.

(3) Max Nzengeli, Pakome what a Performance hakika Hawa ni miamba kabisa, wametumwa kazi na kweli wanaifanya kazi.

(4) Gibril sillah huyu ni Moto na Nina mpa man of the match katika upande wa Azam Fc, maana magoli yote yametokea kwake goli la kwanza kafunga yeye pia kaja kusababisha penati likapatikana goli la pili kupitia Prince Dube.

Bacca na Mamunyeto walikua na kazi ya kufanya kupambana na huyu the magician left footer.

(5) Magoli kipa wa pande zote wameonesha uwezo wa Hali ya juu sema bahati haikua kwake kwa Idrisu lakini kafanya saves Kali sana haswa mashine iliyopigwa na Azizi ki.

Ukija kwa Diara mdaka mishale Kuna moja kutoka kwa Silla wameonesha uwezo wa Hali ya juu.

(6) Azizi ki ni motooo hat trick kaondoka na mpira na point tatu muhimu baada ya kufanya come back ya Nguvu.

HAKIKA TUMEONA MPIRA BURUDANI NA SIYO ILI MRADI MPIRA.
Leo kuna pira makande huko kairo
 
Back
Top Bottom