Haya ni maajabu ya tume ya ajira!!!!tutafika????????????? ???

msani

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2011
Posts
1,801
Reaction score
1,191
wakuu,heshima mbele!!!
nimekuta tangazo la kuwaita watu kwenye interview kwa mwezi wa tano(may) ila kilichonisikitisha ni haya masharti ya kwenda kwenye interview:::

Wasailiwa wanashauriwa kuzingatia yafuatayo:
1. Kuja na vyeti Halisi (original certificates) za kuanzia kidato cha nne, sita,
Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na
sifa za mwombaji.
2. “Transcript”, Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”,
hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS
SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
3. Kila msailiwa aje na picha moja (Passport size).
4. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi.
5. Kila msailiwa azingatie tarehe na eneo alilopangiwa
6. Kila msailiwa aje na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate)
7. Wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa
maombi yao hayakufanikiwa na wasisite kuomba mara nafasi za kazi
zitakapotangazwa tena.

swali langu:
je kati ya academic results na leaving certificate kipi ni halali kutumia!!!!!!
 
ahaa na nyie vijana sasa mnatuchosha. kwa nini hamshauriki? utata hapo uko wapi? sasa wewe unang'ang'ania uende na leaving/ academic results, za nini?
 
ahaa na nyie vijana sasa mnatuchosha. kwa nini hamshauriki? utata hapo uko wapi? sasa wewe unang'ang'ania uende na leaving/ academic results, za nini?
mkuu taratibu,hivi ni vyuo vingapi wanatoa wanatoa papo hapo unapomaliza chuo,au wanatoa transcript,pia cheti hakioneshi matokeo bali transcript ya chuo!!!
 
wee kaa kimya kuna watu wanavyo wataajiriwa na ukipata na wewe chja kwako utafute kazi
 
mkuu una level gani ya elimu? samahan kwa swali hilo, ila litasaidia namna yakukupatia majibu.
 
kazi zipi tena hizo walizotoa majina?au weka ni gazeti gani mkuu tuangalie kama tuko kwenye ufalme
 
mkuu una level gani ya elimu? samahan kwa swali hilo, ila litasaidia namna yakukupatia majibu.
mkuu mie sijasoma bana ila nimesikitika kuona kuwa kuwa watu wanashindwa kuajiriwa kwa kuwa hawana vyeti huku wakiwa na transcript halali za chuo lkn pia haohao utumishi wanaajiri walimu bila hata transcript na mtu anaonesha transcript anaporipoti kwenye kituo cha kazi!!!!!je sera ni ipi inayofanya kazi kwa walimu na kwa watu wa kada zingine!!!??
 
sasa cha ajabu ktk hilo tangazo lao ni nini?mbona linaeleweka,wewe kama huna hivyo vinavyotakiwa,wapo ambao wanavyo!
 
zumbemkuu pole,mdogo wangu amemaliza tia mpaka sasa vyeti havijatoka mpaka mwaka uishe kila anapopeleka trascript anaambiwa alete cheti.ni mfumo mbovu huu sa sijui ni serkali au chuo
 
Mshafanya JF kuwa facebook. Kuna malalamiko ya kitoto jamani mods mko wapi?? Mnatuchosha macho na akili nyie watoto mliomaliza vyuo!!

:yawn:
 


Kama hauna si ukae kimya, mbona hapo hakuna kitu cha kushangazi. Au ulikosa kitu cha kuongelea??????????
Ushauri wangu, nenda mpaka na madaftari uliyotumia chekechea mpaka ulipoishia kielimu. Kuhusu kuzaliwa hapo sina ushauri.
 
Mshafanya JF kuwa facebook. Kuna malalamiko ya kitoto jamani mods mko wapi?? Mnatuchosha macho na akili nyie watoto mliomaliza vyuo!!

:yawn:

kwani umelazimishwa kusoma na kucomment? Shida ipo kwenye transcripts, kwani kwenye tangazo la ajira hawazikatai...ila likija suala la usahili hawazitaki...huu ni wendawazimu, wawe na msimamo mmoja basi.
 
Haha UDOM hawajatoa Transcript wala Vyeti kwa wahitimu wa mwaka jana. Poleni sana wa UDOM na wengine ambao hamjapewa vyeti. Tangazo hli haliwahusu
 
Utumishi ya wapi inayoajiri Walimu? Walimu wanafanyiwa Usaili wapi? Endelea tu kulalamika na ukipata transcript utaomba kwa wakati wako. Kama unajilinganisha na Walimu kwanini wewe bado upo mtaani na wenzio wapo kwenye ajira msani?
 
Last edited by a moderator:
Jamaa mmoja alikosa kazi kwa kuwa hakuwa na cheti orijino, alikuwa na akademiki
 
ahaa na nyie vijana sasa mnatuchosha. kwa nini hamshauriki? utata hapo uko wapi? sasa wewe unang'ang'ania uende na leaving/ academic results, za nini?

Ndio RPC na mbweta lako kama kawa kama dawa.
 
mtoa mada hana mantinki. kama vipi wewe nenda na unavyoona vinafaa hata madaftari na unifform na kitambulisho pia beba mkuuu halafu ndio utoe hizo mada zako.
 


Hakuna kati ya hivyo kinachoruhusiwa kulingana na tangazo.Au ni wapi hukuelewa?
 
Haha UDOM hawajatoa Transcript wala Vyeti kwa wahitimu wa mwaka jana. Poleni sana wa UDOM na wengine ambao hamjapewa vyeti. Tangazo hli haliwahusu
Sasa na wale wa UDOM ambao tayari wana ajira? au we unadhani walioko UDOM wote walia njaa?
 


Tafadhali MSANI ebu rudia kusoma hiyo sehemu yenye rangi ya bluu.....Nadhani hawataki viambatanisho vilivyotajwa hapo tuu...na si kwa level ya vyuo...Plz Nikosoe kama nimekosea kuisoma thread yako!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…