Hayati Dkt. Magufuli hakuisaidia Chato

Hayati Dkt. Magufuli hakuisaidia Chato

Hayo unayosema ni kweli. Hakukuwa na haja ya kubadili kijiji kuwa mji. Alichotakiwa ni kuwainua watu wake ili waweze kuongeza productivity. Kufanya Chato kuwa mji ni kuleta wageni ambao ndiyo watakuwa wafaidikaji zaidi ya wenyeji ambao hawana kitu hivyo kuwafanya wawe servants kwenye ardhi yao.
Mkuu umeadimika sana
 
Muda si mrefu Chato itasahaulika kama mwenye Chato yake.

Hakuna Wilaya iliyopata umaarufu kwa ghafla kama Chato. Wengi hawajui wilaya walizotoka Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Jakaya wala Samia.

Bwana yule alikuwa mbinafsi, mbaguzi , dhalimu na fashisti sana.

Ahsante Mungu kwa matendo yako makuu. Sisi ni nani tusiushukuru uamuzi wako na mapenzi yako kwetu?
 
Unajiita doctor ila unaandika vitu kama mtoto mdogo alievaa pampas ambae hajui la kufanya!Unasema Magufuli kupenda kwao siyo kosa,unaelewa kuwa Magufuli alikuwa ni Rais wa nchi na wala siyo mwananchi wa kawaida?..
Nami nilishangaa sana kwa mwanzo huo wa mada yake.

Ilikuwa kidogo tu niishie njiani kuendelea kuisoma yote, kabla ya kuanza kuona inapoelekea mada yake.

Hata haya tunayoyaandika sasa kuhusu miradi mbadala ambayo ingewagusa watu moja kwa moja na ingekuwa ni endelevu; tunaandika juu yake baada ya kuona kwamba mhusika alikuwa hastuliwi na kelele za upendeleo wa kwao.

Ndiyo maana tukapendekeza haya tunayoyapendekeza hapa.

'In fact', kama angewekeza kwa wananchi wa wilaya ile, pengine hata makelele yasingekuwepo sana kwa upendeleo huo, na bila shaka angesifiwa sana kama maisha ya wananchi yangebadilishwa na kazi hiyo ya uwekezaji juu yao, badala ya uwekezaji kwa vitu.
 
Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita ni Tanzania. Kwahivyo, itakuwa furaha ya kila mzalendo wa Tanzania kuona maendeleo ya Chato kama itakavyokuwa kwa maendeleo ya sehemu nyingine ya Tanzania...
Ivi hii tabia yakuita mali za umma majina ya watu binafsi ipo kisheria au mimi ndo sielewi wakuu??? Haya majina mfugale,sijui kijazi huwa ni kwann inakuwa majina yao viongozi wakati pesa zina wananchi walipa kodi?

Ebu acheni hii tabia viongozi tz maana sisi ambao sio viongozi majina yetu ndo yaishie kwenye vitambulisho vya nida??!!! Acheni izi mambo kama haipo kisheria pesa niza wananchi buana
 
Mkuu ukiamini yanayosemwa na nyumbu wa Ufipa, utaamini kweli Mbowe ni "mwekezaji" Dubai na Chadema ni chama kikuu cha upinzani wakati hakina mwenyekiti wa mtaa, wala diwani wala mbunge nchi nzima!!
Unajua Mkuu mimi sijawahi kufika Chato,ila nimepita hiyo barabara kuu ya Mwanza-Geita nikaishia Geita,sikufika Chato.

Sasa waliowahi kufika kule watuambie Chato palikuwa mahala pa hovyo kabla JPM hajawa Rais wakipalinganisha na Wilaya zipi (wasipalinganishe na Majiji au Manispaa).

Mfano:waseme Chato ni pa ajabu ajabu tu afadhali ya kule alikozaliwa Mkapa,Mangula,Phillip Mpango,Nimrod Mkono,Sospeter Muhongo,Rostam Aziz, n.k.
 
Msingi imara ni muhimu katika ujenzi ila endapo ukakosea msingi ata nyumba iwe nzuri vipi ipo cku itapiga creck
 
Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita ni Tanzania. Kwahivyo, itakuwa furaha ya kila mzalendo wa Tanzania kuona maendeleo ya Chato kama itakavyokuwa kwa maendeleo ya sehemu nyingine ya Tanzania...
Hivi vitu vingine mnavyo shadadia utasema sehemu nyingine hamna..!! Yani ata uwanja wa mpira wa miguu nao nongwa? Au mnafikiri uo uwanja ungekuwa kama wa Benjamini?

Uwanja wenyewe sijui ulikuwa umetumia milion 200 tu mpaka ulipofikia hapo na ulikuwa una miaka kama mitatu tangia uanze kujengwa na badi zaidi ya milion 600 zinaitajika kuukamilisha alafu mnalalama tu..!!
 
Hivi vitu vingine mnavyo shadadia utasema sehemu nyingine hamna..!! Yani ata uwanja wa mpira wa miguu nao nongwa? Au mnafikiri uo uwanja ungekuwa kama wa Benjamini? Uwanja wenyewe sijui ulikuwa umetumia milion 200 tu mpaka ulipofikia hapo na ulikuwa una miaka kama mitatu tangia uanze kujengwa na badi zaidi ya milion 600 zinaitajika kuukamilisha alafu mnalalama tu..!!
Hivi umeisoma mada na kuielewa kweli?

Maanake wewe unakoroga kivyako tu.
Milioni 200 + milioni 600 = 800 milioni - uwanja wa mpira kijijini? Kuna timu gani maarufu sana hapo kijijini.

Sasa chukulia hiyo hela milioni 800 iwekezwe kwa wananchi, iwasaidie kwa mfano kulima zao la alizeti ili kuzalisha mafuta ya kula.

Wananchi hawa wapate huduma zote zinazohitajika kuwezesha kilimo bora cha zao hilo, hela hiyo hiyo ingetosha kuweka kiwanda cha kusindika zao hilo na kupata mafuta na mashudu ya kulisha mifugo.

Mbali ya faida ya kuongeza pato la wananchi hao katika miaka miwili na kuendelea, hawa wananchi wangepata kitu cha kudumu zaidi - elimu ya kuendelea kuzalisha kwa ufanisi zao hilo mwaka hadi mwaka, hata baada ya Magufuli kuondoka!
Na uwanja huo wangeujenga wananchi wenyewe bila hata ya msaada iwapo kama kipato chao kimeongezeka kutokana na hiyo mlilioni 800.

Huo uwanja hata kama utaendelea kujengwa (sidhani), utaleta manufaa hayo ya moja kwa moja kwa wananchi wa eneo hilo?

Na kama bado huelewi...
 
Aliisaidia sana, labda kama walikuwa hawabebeki tu.
 
Mkuu ukiamini yanayosemwa na nyumbu wa Ufipa, utaamini kweli Mbowe ni "mwekezaji" Dubai na Chadema ni chama kikuu cha upinzani wakati hakina mwenyekiti wa mtaa, wala diwani wala mbunge nchi nzima!!
Mbowe ni mfanyabiashara wa kuzaliwa. Baba yake Mzazi alikuwa anakula Meza moja na Nyerere. Ingawa aliumizwa Sana 5 years ago Mungu ameshamuonesha matendo yake Makuu. Mbowe hujazaliwa kwenye Njaa na hajakulia kwenye Njaa.
 
Wapinzani wametucheleweshea sana maendeleo, ila hayo magorofa tutafugia popo msijali, mwenda zake alipenda sana chatto iwe mkoa sasa wilaya ndo najiuliza n zipi
 
Mchango Safi kabisa. Kulikuwa na haja ya Jengo Geita Airport halafu kuliita Mfugale Tower?
Hi ilikuwa cyndicate ya jiwe na jinsi walivyokuwa wanapongezana!! Kumbukeni kalemane ni ndugu ya jiwe na walikuwa njiani kujenga kiwanja cha michezo cha kimataifa hapo kijijini!
 
Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita ni Tanzania. Kwahivyo, itakuwa furaha ya kila mzalendo wa Tanzania kuona maendeleo ya Chato kama itakavyokuwa kwa maendeleo ya sehemu nyingine ya Tanzania.

Lakini maendeleo ni nini?

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli alijitanabaisha kama mtu anayependa maendeleo, lakini kuna uwezekano mkubwa hakujua tafsiri ya maendeleo. Pamoja na mambo mengine, Magufuli alitamani maendeleo ya nyumbani kwao Chato, na hivyo alifanya mengi huko nyumbani kwao, lakini pengine hakupasaidia inavyotakikana.

Magufuli alijenga uwanja wa ndege wa kutua ndege kubwa wilayani Chato, wakati kuna majiji (mfano Tanga), manispaa na miji mikubwa kuliko Chato ambako hakuna viwanja vya ndege vya maana au vilivyopo havina hadhi ya maeneo hayo. Kwanini Chato?

Hoteli ya Nyota Tano ilikwisha anza kujengwa Chato. Uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa ulikuwa kwenye mpango wa kujengwa Chato. Alilazimisha CRDB wapeleke huduma wilayani Chato ingawa hakuna tija ya kibiashara. Na Jengo walilopangisha CRDB huko Chato ni jengo lake huyo Magufuli.

Je! Magufuli aliipenda Chato? Jibu ni Ndiyo. Na sio kosa kupenda kwenu, sio kosa kupenda maendeleo ya kwenu. Shida inakuja kwenye tafsiri ya maendeleo.

Magufuli angetambua maana ya maendeleo; Angeanza kuboresha elimu wilayani Chato kabla ya kujenga Hotel ya Nyota Tano. Moja kati ya wilaya zenye mazingira magumu kwa wanafunzi na walimu ni Wilaya ya Chato. Hoteli ya Nyota tano ya nini wakati wanafunzi wanamaliza darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika? Nani ataijenga Chato wakati idadi kubwa ya vijana hawapati elimu yenye tija katika dunia ya leo (Na hili ni kwa maeneo mengi ya Tanzania).

Kanda ya Ziwa kuna Ng'ombe wengi sana, lakini hawana afya. Pesa ya kujenga uwanja wa ndege ingetosha kutoa elimu kwa wafugaji juu ya namna ya kufuga kwa faida pamoja na kujenga viwanda vidogodogo vya kusindika Nyama na Maziwa ambavyo vingetoa ajira ya kudumu kwa vijana wa Chato. Wafanyabiashara wangemiminika Chato kutoka maeneo ya jirani kwa ajili ya biashara ya Nyama, na mazao ya maziwa. Kwanini mwenyeji wa Geita anunue maziwa ya Tanga Fresh, au Asas kutoka Iringa wakati kuna Ng'ombe wengi ndani ya kanda ya ziwa kuliko Iringa na Tanga kwa pamoja?

Kuna ardhi kubwa wilayani Chato. Magufuli angeweza kupeleka wataalamu wa kilimo kutoa mafunzo kwa vijana juu ya kilimo chenye tija ya kiuchumi na kibiashara. Wakulima wangelima kibiashara zaidi na kuvutia masoko kutoka mikoa jirani na nchi jirani. Watu wangemiminika Chato na kuchangamsha shughuli za maendeleo.

Kuna Ziwa Viktoria. Angeweza kuwekeza kwenye kilimo cha samaki (kuzalisha samaki ndani ya vitalu vya Ziwani) ambacho kingewanufaisha watanzania wanaoishi Chato. Ajira zingepatikana, wafanyabiashara kutoka mikoa jirani na hata nchi jirani za Rwanda, Burundi na DRC wangefika Chato kufungasha mizigo.

Angeweza kujenga Chuo Kikuu au hata matawi mawili matatu ya vyuo vikuu. Mji wa Iringa ni miongoni mwa miji iliyochangamshwa na uwepo vyuo vikuu. Chato ingechangamka pia.

Hayo yote yangewezekana kirahisi kutokana na nguvu aliyokuwa nayo kama Rais. Lakini nguvu ili iwe na tija sharti iambatane na akili.
Halafu yangefuata hayo ya kujenga uwanja wa ndege na mahoteli kwa kuwa sasa watu wenye uwezo wa kuvitumia (labda) wangekuwapo.

Lakini hawapo. Na sasa shirika la Ndege limesitisha safari za ndege Chato kwa sababu aliyekuwa anautumia uwanja wa ndege wa Chato hayupo. Nyasi zina tabia ya kuota hata juu ya zege. Baada ya muda kidogo ile hoteli ya nyota tano ambayo haijamalizika itabaki gofu. Uwanja wa mpira wa kisasa hautajengwa. Benki ya CRDB itaondoka kwa sababu wakazi wa Chato wanaoweka pesa benki ni walimu na watumishi wengine wa serikali - ambao wanatumia NMB. Majengo mazuri ya mahakama na vituo vya polisi hayawezi kuchochea maendeleo.

Kuna suala la Hospitali kubwa ya kanda iliyojengwa Chato. Huduma za afya ni suala zuri lakini jengo pekee halitoshi. Huduma zitakapoanza zitapaswa kufanana na jengo lenyewe. Hata hivyo haikuwa lazima kujenga hospitali kubwa Chato kabla ya kuboresha huduma za zahanati (Primary Health Care) vijijini. Hakuna maana ya kujenga hospitali kubwa eneo moja wakati zahanati katika vijiji mia au zaidi hazina ubora. Huduma za zahanati nyingi zikiwa bora, faida yake ni kubwa zaidi kuliko huduma ya hospitali kubwa moja. Kwahiyo, pamoja na hatua nzuri ya kujenga hospitali ile, naamini haikupaswa kuwa jambo la kwanza.

Magufuli hakuisaidia Chato kwasababu aliamini zaidi katika vitu (hardware) badala ya watu (Software). Angeanza kuwajenga watu kwa elimu na maarifa halafu akawajengea nyenzo za kuboresha elimu na maarifa yao; shule, vyuo, viwanda kwa ajili ya ajira, na mbinu zingine za kuvutia uwekezaji.

Lakini wapi! Aliwaza matokeo badala ya mchakato. Alichojenga Chato kitabaki kuwa makazi ya popo na mijusi kwa sababu hakuna wa kukitumia.

View attachment 1753858

Nawasilisha!

Dr Cyrillo
Wewe huijui Chato, unaifahamu kupitia vyombo vya vya Habari tu. Magufuli amefanya maendeleo makubwa sana wilayani Chato upande wa elimu.

Kiufupi safari za ndege za ATCL hazijasitishwa, bado zipo kama kawa. Sisi tunaopanda ndege tunajua.

Ungekuwa umeishi wilaya ya Chato usingeandika upuuzi huo ulioandika..Ulichoandika ni taka taka
 
Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita ni Tanzania. Kwahivyo, itakuwa furaha ya kila mzalendo wa Tanzania kuona maendeleo ya Chato kama itakavyokuwa kwa maendeleo ya sehemu nyingine ya Tanzania.

Lakini maendeleo ni nini?

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli alijitanabaisha kama mtu anayependa maendeleo, lakini kuna uwezekano mkubwa hakujua tafsiri ya maendeleo. Pamoja na mambo mengine, Magufuli alitamani maendeleo ya nyumbani kwao Chato, na hivyo alifanya mengi huko nyumbani kwao, lakini pengine hakupasaidia inavyotakikana.

Magufuli alijenga uwanja wa ndege wa kutua ndege kubwa wilayani Chato, wakati kuna majiji (mfano Tanga), manispaa na miji mikubwa kuliko Chato ambako hakuna viwanja vya ndege vya maana au vilivyopo havina hadhi ya maeneo hayo. Kwanini Chato?

Hoteli ya Nyota Tano ilikwisha anza kujengwa Chato. Uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa ulikuwa kwenye mpango wa kujengwa Chato. Alilazimisha CRDB wapeleke huduma wilayani Chato ingawa hakuna tija ya kibiashara. Na Jengo walilopangisha CRDB huko Chato ni jengo lake huyo Magufuli.

Je! Magufuli aliipenda Chato? Jibu ni Ndiyo. Na sio kosa kupenda kwenu, sio kosa kupenda maendeleo ya kwenu. Shida inakuja kwenye tafsiri ya maendeleo.

Magufuli angetambua maana ya maendeleo; Angeanza kuboresha elimu wilayani Chato kabla ya kujenga Hotel ya Nyota Tano. Moja kati ya wilaya zenye mazingira magumu kwa wanafunzi na walimu ni Wilaya ya Chato. Hoteli ya Nyota tano ya nini wakati wanafunzi wanamaliza darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika? Nani ataijenga Chato wakati idadi kubwa ya vijana hawapati elimu yenye tija katika dunia ya leo (Na hili ni kwa maeneo mengi ya Tanzania).

Kanda ya Ziwa kuna Ng'ombe wengi sana, lakini hawana afya. Pesa ya kujenga uwanja wa ndege ingetosha kutoa elimu kwa wafugaji juu ya namna ya kufuga kwa faida pamoja na kujenga viwanda vidogodogo vya kusindika Nyama na Maziwa ambavyo vingetoa ajira ya kudumu kwa vijana wa Chato. Wafanyabiashara wangemiminika Chato kutoka maeneo ya jirani kwa ajili ya biashara ya Nyama, na mazao ya maziwa. Kwanini mwenyeji wa Geita anunue maziwa ya Tanga Fresh, au Asas kutoka Iringa wakati kuna Ng'ombe wengi ndani ya kanda ya ziwa kuliko Iringa na Tanga kwa pamoja?

Kuna ardhi kubwa wilayani Chato. Magufuli angeweza kupeleka wataalamu wa kilimo kutoa mafunzo kwa vijana juu ya kilimo chenye tija ya kiuchumi na kibiashara. Wakulima wangelima kibiashara zaidi na kuvutia masoko kutoka mikoa jirani na nchi jirani. Watu wangemiminika Chato na kuchangamsha shughuli za maendeleo.

Kuna Ziwa Viktoria. Angeweza kuwekeza kwenye kilimo cha samaki (kuzalisha samaki ndani ya vitalu vya Ziwani) ambacho kingewanufaisha watanzania wanaoishi Chato. Ajira zingepatikana, wafanyabiashara kutoka mikoa jirani na hata nchi jirani za Rwanda, Burundi na DRC wangefika Chato kufungasha mizigo.

Angeweza kujenga Chuo Kikuu au hata matawi mawili matatu ya vyuo vikuu. Mji wa Iringa ni miongoni mwa miji iliyochangamshwa na uwepo vyuo vikuu. Chato ingechangamka pia.

Hayo yote yangewezekana kirahisi kutokana na nguvu aliyokuwa nayo kama Rais. Lakini nguvu ili iwe na tija sharti iambatane na akili.
Halafu yangefuata hayo ya kujenga uwanja wa ndege na mahoteli kwa kuwa sasa watu wenye uwezo wa kuvitumia (labda) wangekuwapo.

Lakini hawapo. Na sasa shirika la Ndege limesitisha safari za ndege Chato kwa sababu aliyekuwa anautumia uwanja wa ndege wa Chato hayupo. Nyasi zina tabia ya kuota hata juu ya zege. Baada ya muda kidogo ile hoteli ya nyota tano ambayo haijamalizika itabaki gofu. Uwanja wa mpira wa kisasa hautajengwa. Benki ya CRDB itaondoka kwa sababu wakazi wa Chato wanaoweka pesa benki ni walimu na watumishi wengine wa serikali - ambao wanatumia NMB. Majengo mazuri ya mahakama na vituo vya polisi hayawezi kuchochea maendeleo.

Kuna suala la Hospitali kubwa ya kanda iliyojengwa Chato. Huduma za afya ni suala zuri lakini jengo pekee halitoshi. Huduma zitakapoanza zitapaswa kufanana na jengo lenyewe. Hata hivyo haikuwa lazima kujenga hospitali kubwa Chato kabla ya kuboresha huduma za zahanati (Primary Health Care) vijijini. Hakuna maana ya kujenga hospitali kubwa eneo moja wakati zahanati katika vijiji mia au zaidi hazina ubora. Huduma za zahanati nyingi zikiwa bora, faida yake ni kubwa zaidi kuliko huduma ya hospitali kubwa moja. Kwahiyo, pamoja na hatua nzuri ya kujenga hospitali ile, naamini haikupaswa kuwa jambo la kwanza.

Magufuli hakuisaidia Chato kwasababu aliamini zaidi katika vitu (hardware) badala ya watu (Software). Angeanza kuwajenga watu kwa elimu na maarifa halafu akawajengea nyenzo za kuboresha elimu na maarifa yao; shule, vyuo, viwanda kwa ajili ya ajira, na mbinu zingine za kuvutia uwekezaji.

Lakini wapi! Aliwaza matokeo badala ya mchakato. Alichojenga Chato kitabaki kuwa makazi ya popo na mijusi kwa sababu hakuna wa kukitumia.

View attachment 1753858

Nawasilisha!

Dr Cyrilo

IMG-20210914-WA0018.jpg
 
Wilaya ya Chato iliyopo mkoani Geita ni Tanzania. Kwahivyo, itakuwa furaha ya kila mzalendo wa Tanzania kuona maendeleo ya Chato kama itakavyokuwa kwa maendeleo ya sehemu nyingine ya Tanzania.

Lakini maendeleo ni nini?

Aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Magufuli alijitanabaisha kama mtu anayependa maendeleo, lakini kuna uwezekano mkubwa hakujua tafsiri ya maendeleo. Pamoja na mambo mengine, Magufuli alitamani maendeleo ya nyumbani kwao Chato, na hivyo alifanya mengi huko nyumbani kwao, lakini pengine hakupasaidia inavyotakikana.

Magufuli alijenga uwanja wa ndege wa kutua ndege kubwa wilayani Chato, wakati kuna majiji (mfano Tanga), manispaa na miji mikubwa kuliko Chato ambako hakuna viwanja vya ndege vya maana au vilivyopo havina hadhi ya maeneo hayo. Kwanini Chato?

Hoteli ya Nyota Tano ilikwisha anza kujengwa Chato. Uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa ulikuwa kwenye mpango wa kujengwa Chato. Alilazimisha CRDB wapeleke huduma wilayani Chato ingawa hakuna tija ya kibiashara. Na Jengo walilopangisha CRDB huko Chato ni jengo lake huyo Magufuli.

Je! Magufuli aliipenda Chato? Jibu ni Ndiyo. Na sio kosa kupenda kwenu, sio kosa kupenda maendeleo ya kwenu. Shida inakuja kwenye tafsiri ya maendeleo.

Magufuli angetambua maana ya maendeleo; Angeanza kuboresha elimu wilayani Chato kabla ya kujenga Hotel ya Nyota Tano. Moja kati ya wilaya zenye mazingira magumu kwa wanafunzi na walimu ni Wilaya ya Chato. Hoteli ya Nyota tano ya nini wakati wanafunzi wanamaliza darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika? Nani ataijenga Chato wakati idadi kubwa ya vijana hawapati elimu yenye tija katika dunia ya leo (Na hili ni kwa maeneo mengi ya Tanzania).

Kanda ya Ziwa kuna Ng'ombe wengi sana, lakini hawana afya. Pesa ya kujenga uwanja wa ndege ingetosha kutoa elimu kwa wafugaji juu ya namna ya kufuga kwa faida pamoja na kujenga viwanda vidogodogo vya kusindika Nyama na Maziwa ambavyo vingetoa ajira ya kudumu kwa vijana wa Chato. Wafanyabiashara wangemiminika Chato kutoka maeneo ya jirani kwa ajili ya biashara ya Nyama, na mazao ya maziwa. Kwanini mwenyeji wa Geita anunue maziwa ya Tanga Fresh, au Asas kutoka Iringa wakati kuna Ng'ombe wengi ndani ya kanda ya ziwa kuliko Iringa na Tanga kwa pamoja?

Kuna ardhi kubwa wilayani Chato. Magufuli angeweza kupeleka wataalamu wa kilimo kutoa mafunzo kwa vijana juu ya kilimo chenye tija ya kiuchumi na kibiashara. Wakulima wangelima kibiashara zaidi na kuvutia masoko kutoka mikoa jirani na nchi jirani. Watu wangemiminika Chato na kuchangamsha shughuli za maendeleo.

Kuna Ziwa Viktoria. Angeweza kuwekeza kwenye kilimo cha samaki (kuzalisha samaki ndani ya vitalu vya Ziwani) ambacho kingewanufaisha watanzania wanaoishi Chato. Ajira zingepatikana, wafanyabiashara kutoka mikoa jirani na hata nchi jirani za Rwanda, Burundi na DRC wangefika Chato kufungasha mizigo.

Angeweza kujenga Chuo Kikuu au hata matawi mawili matatu ya vyuo vikuu. Mji wa Iringa ni miongoni mwa miji iliyochangamshwa na uwepo vyuo vikuu. Chato ingechangamka pia.

Hayo yote yangewezekana kirahisi kutokana na nguvu aliyokuwa nayo kama Rais. Lakini nguvu ili iwe na tija sharti iambatane na akili.
Halafu yangefuata hayo ya kujenga uwanja wa ndege na mahoteli kwa kuwa sasa watu wenye uwezo wa kuvitumia (labda) wangekuwapo.

Lakini hawapo. Na sasa shirika la Ndege limesitisha safari za ndege Chato kwa sababu aliyekuwa anautumia uwanja wa ndege wa Chato hayupo. Nyasi zina tabia ya kuota hata juu ya zege. Baada ya muda kidogo ile hoteli ya nyota tano ambayo haijamalizika itabaki gofu. Uwanja wa mpira wa kisasa hautajengwa. Benki ya CRDB itaondoka kwa sababu wakazi wa Chato wanaoweka pesa benki ni walimu na watumishi wengine wa serikali - ambao wanatumia NMB. Majengo mazuri ya mahakama na vituo vya polisi hayawezi kuchochea maendeleo.

Kuna suala la Hospitali kubwa ya kanda iliyojengwa Chato. Huduma za afya ni suala zuri lakini jengo pekee halitoshi. Huduma zitakapoanza zitapaswa kufanana na jengo lenyewe. Hata hivyo haikuwa lazima kujenga hospitali kubwa Chato kabla ya kuboresha huduma za zahanati (Primary Health Care) vijijini. Hakuna maana ya kujenga hospitali kubwa eneo moja wakati zahanati katika vijiji mia au zaidi hazina ubora. Huduma za zahanati nyingi zikiwa bora, faida yake ni kubwa zaidi kuliko huduma ya hospitali kubwa moja. Kwahiyo, pamoja na hatua nzuri ya kujenga hospitali ile, naamini haikupaswa kuwa jambo la kwanza.

Magufuli hakuisaidia Chato kwasababu aliamini zaidi katika vitu (hardware) badala ya watu (Software). Angeanza kuwajenga watu kwa elimu na maarifa halafu akawajengea nyenzo za kuboresha elimu na maarifa yao; shule, vyuo, viwanda kwa ajili ya ajira, na mbinu zingine za kuvutia uwekezaji.

Lakini wapi! Aliwaza matokeo badala ya mchakato. Alichojenga Chato kitabaki kuwa makazi ya popo na mijusi kwa sababu hakuna wa kukitumia.

View attachment 1753858

Nawasilisha!

Dr Cyrilo
Anthony Dialo alishasema, jamaa alikuwa mwehu. Nguvu nyingi, akili punje ya mchele
 
Tumsameheni na tusonge mbele jamani ndio keshatangulia na yake yamemaliza. Sasa kazi kwa walio Chato na TZ kwa ujumla. Kiufupi mambo mengi hata waliohai tunauliza masuali kinyume nyume kwa mfano ivi TZ tuna wataalamu wangapi wa afya, lakini unamsikia mtu akitoka povu kanisani akiuliza kwanini wazungu hawajatengeneza chanjo ya malaria ?

Suali zuri ni kwanini wataalamu wa ndani hawajavumbua chanjo, sio wazungu. Kwa bahati wao hawasumbuliwi na malaria, I can understand that its not in their prio-list.

TZ tuna tatizo la umeme tokea napata fahamu zangu liko vile vile hadi nadhani nitaondoka duniani. Wataalamu wetu wanafanya nini ? UDSM inazalisha vilaza ?
 
Tukiwa tunaandika hapa JF, mamilioni ya fedha yanatumika kuendesha kesi ya ugaidi. Mliwahi kujiuliza kuendesha kesi kama ile inagharimu kiasi gani ? Kila mwanasheria wa serekali analipwa kiasi gani kuendesha kesi n.k. Mashahidi, maofisa, majaji.

Hii itatupiliwa mbali aidha sio muda mrefu au baada muda mfupi ujao. Kamanda wa jeshi anatafuta magaidi ndani ya madrasa - ivi ulisikia wapi gaidi akatokea huko 🙄
 
Back
Top Bottom